mkalamatukio

Wachezaji nguli wa soka wahoji kutochezeshwa Carrick jana

Michael Carrick Pass master!
Wachezaji nguli wa soka wa zamani wakiongozwa na Gary Linneker jana walihoji ni vipi mcheza wa daraja la juu kiungo wa Man United hakupangwa katika mechi ya Ukrayne dhidi ya England pamoja na England kuonesha wazi kushindwa kumiliki mpira kwa vipindi virefu katika mchezo huo, Linneker ambaye alipata kuzichezea Fc Barcelona ya Spain na Totenham Hotspurs ya jijini London aliandika kupitia ukurasa wake wa Twitter kama hivi
Kana kwamba haikutosha Lineker kushangazwa naye Dietmar Hamman aliyekuwa kiungo wa Liverpool na Man City
  kupitia mtandao huo huo naye ali tweet
Hamann naye alishangazwa na kukosekana Carrick katika kikosi cha England jana, katika hali ya kushangaza zaidi hata Roy Hodgson alipoamua kumpumzisha Jack Wilshere na kuamua kumuingiza Ashley Young ambaye si kiungop wa kati wakati Carrick alikuwepo benchini na England ilimuhitaji kwa kushindwa kumiliki mpira. Hata hivyo England ilifanikiwa kutoka sare na hivyo kuendelea kuongoza kundi H kwa pointi 16.

Kula panya na zabibu kavu kwamnusuru kifo baada ya kukaa njaa miezi minne!

Raul Fernando Gomez (58) aliyepotea kwa miezi minne akiwa katika safari ya kutembea kwa miguu katika milima huko nchini Uruguay Amerika ya kusini akitokea nchini Chile aliokolewa jumapili na kundi la wa Argentina waliofika katika eneo hilo la milima wakifanya utafiti juu barafu (snow). Huku akiwa amepungua karibu kilo 3, na kupoteza virutubishi mwilini katika sakata hilo,madaktari wamesema atarudi katika hali yake ya kawaida baada muda mfupi?
Gomez akionesha jinsi alivyokonda
Gomez ambaye alisafiri kutoka Chile kwenda Argentina mnamo mwezi Mei kwa pikipiki kwa bahati mbaya pikipiki hiyo iliharibika njiani na hivyo kulazimika kutembea kwa miguu ambapo alipotea njia baada ya kimbunga kutokea. Maafisa toka jimbo la kaskazini magharibi mwa Argentina walimkuta akiwa katika kibanda kilichopo futi elfu 9318 kutoka usawa wa bahari, Gomez akiwa dhoofu wa hali alifanikiwa kutembea kwa taabu ambapo alifungua mlango wa kibanda hicho ndipo maafisa hao waliokuwa wakipita eneo hilo wakamuona. 

Akibebwa baada ya kuokolewa


Gavana wa San Juan aliliambia gazeti la Diario de cuyo "Huu ni muujiza, bado hatuamini kilichotokea, Tulimpatia simu akaongea na familia yake, pia nilimuuliza wewe ni mwenye kuamini? akajibu " sikuwa lakni sasa ni mwenye kuamini! Kwa muda wote huo Gomez alikuwa akila zabibu zilizokauka, sukari na panya. Madaktari wameeleza kuwa Gomez anatibiwa shinikizo la damu na ukosefu mkubwa wa virutubisho na maji mwilini.
Akipakiwa katika machela ili apelekwe hospitali

Matibabu; Akiwa amelazwa hospitali mjni San Juan.


Habari kwa hisani ya Dailymail, picha kwa hisani ya AP na Reuters.

Breaking news! Jaji wa Redds Miss Tabora afariki asubuhi hii!

Marehemu Terry Mbaika siku ya shindano la Redds Miss Tabora 2013
Aliyekuwa jaji katika shindano la Redds Miss Tabora 2013 Miss Terry Mbaika (pichani kushoto) amefariki leo hii asubuhi katika hospitali ya Jeshi ya Mirambo mjini Tabora. Taarifa zimeeleza kuwa Madame Terry ambaye ni Mkenya ki uraia alikuwa Mc maarufu mjini hapo na alikuwa akimiliki duka la virutubishi liitwalo TIENS, alilazwa katika hospitali hiyo na baadaye kuruhusiwa lakini hali yake ikawa mbaya na kurudishwa hospitalini hapo na hatimaye kufariki asubuhi ya leo. Nikiwa mwenyekiti wa kamati ya Redds Miss Tabora 2013 natoa salamu za rambi rambi kwa famila yake, kwani Marehemu Terry akishirikana na majaji wenzie waliwezesha kwa kiasi kikubwa kulifanya shindano hilo kupata washindi watatu ambao walikubalika na watu wote waliodhuria shindano hilo mapema mwaka huu katika ukumbi wa Frankman Palace mnamo tarehe 31/05/2013. Tumepoteza mdau muhimu na daima tutamkumbuka Terry MbaikaMungu ailaze roho yake pema peponi. Amen!
Kutoka kushoto Majaji Evans, Terry Mbaika, Mkala Fundikira, Irene Madumba na Wendy Charles.
Majaji kazini kwa umakini.
Hapa jaji Terry Mbaika akimfuatilia kwa umakini na ukaribu mshiriki wa Redds Miss Tabora 2013 katika shindano la kipaji. 

Azam yailaza Rhino Fc!

Timu ya Azam Fc ya jijini Dar es Salaam leo hii imeilaza timu ya Rhino Rangers ya mjini Tabora kwa goli 2 kwa sifuri kwa magoli ya Gaudence Mwaikimba kwa shuti kali lililopita kulia mwa lango la kipa wa Rhino Fc mnamo dakika ya 56,baada ya kazi nzuri ya wachezaji wa Azam Fc upande wa kulia mwa uwanja.
Baadhi ya maelfu  ya mashabiki wa soka mjini Tabora wakifuatilia kwa makini mchezo kati ya Azam Fc na Rhino Rangers uliofanyika jioni ya leo katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.
Huku Rhino Rangers ikijaribu kusawazisha bao hilo la Mwaikimba ilijikuta ikongezwa bao la pili kupitia mchezaji wa kiungo Seif Kalihe mnamo dakika ya 77 ya mchezo huo uliodorora. Timu ya Rhino Rangers itabidi ijilaumu kwa kutocheza kwa kujituma kama ambavyo ilicheza katika mchezo dhidi ya Simba ambapo waliweza kuibana Simba na kutoka nayo sare ya goli 2-2. Mchezo ujao wa Rhino utakuwa dhidi ya JKT Oljoro wikiendi ijayo mjini Arusha katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid.   
Patashika langoni mwa Azam
Basi la wachezaji wa Rhino Rangers likitoka uwanjani baada ya mchezo wao dhidi ya Azam Fc kwisha.

Utamliliaje mtu leo, kesho umtukane?

OMMY Dimpoz akilia jukwaani baada ya kulemewa na majonzi ya kifo cha Ngwair tarehe 31/05/2013 Tabora.
Siku chache baada ya kifo cha Albert Mangwea (Ngwair) kulitokea  sintofahamu baada ya msanii Ommy Dimpoz kushutumiwa na gazeti moja la kidaku kuwa alimtukana Ngwair kuwa kafa masikini (kibwege) alipokuwa akipokea tunzo yake pale Milimani city katika kilele cha Kilimanjaro Music Awards. Ninachokumbuka alisema "Sisi wasanii wa Tanzania tumechoka kufa masikini huku tukiwa na majina makubwa" na akatoa wito kwa makampuni makubwa yawape kipaumbele wasanii wa Tanzania katika suala zima la promosheni za bidhaa zao kitu ambacho kitainua kipato cha wasanii wa Tanzania badala ya kutumia wacheza mpira wa nje kama Lionel Messi. Hali ilikuwa mbaya sana kwa Ommy Dimpoz huku akilaaniwa na kusiwa huku na kule na hasa katika mitandao ya kijamii. Kabla ya Kili Music Awards huko Tabora katika kilele cha Redds Miss Tabora 2013 Ommy alitoa kauli hiyo mbele ya Mh William Ngeleja na alimuomba awasaidie kupeleka kilio chao(wasanii) bungeni ili ziunde sheria nzuri zenye kulinda maslahi ya wasanii!


Totenham wawastaajabisha Real Madrid kwa dau la kumuuza Gareth Bale!

Gazeti la michezo lenye ukaribu na kilabu cha Real Madrid leo hii limedai kuwa Mwenyekiti wa Totenham Hotspurs ya jijini London, Uingereza Bw Daniel Levy amewapa bei ya kumnunua mshambuliaji Gareth Bale kuwa ni Euro145 Milioni au kwa maneno mengine ni Pauni 125 Milioni ya Malkia wa Uingereza. Bei hiyo imewastua sana Madrid kwani hawakutegemea kabisa Bw Levy anaefahamika vema kutoa bei zisizoendana na uhalisia ambapo awali aliwasumbua sana Man United kuwanunua Michael Carrick na Dimitar Bernatov. Bei hiyo pia imelistua sana gazeti la Marca ambalo limetoa kichwa cha habari UNA LOCURA ikiwa na maana Crazy au "wazimu"



Wakati huo huo ripoti toka Spain katika gazeti la Marca zimeeleza kuwa Daniel Levy ameshapokea ofa ya Pauni 85 milioni toka klabu ya PSG ya ufaransa inayomilikiwa na matajiri wa kiarabu. Pia taarifa hiyo ilisema katika ofa zote Muhimu ni ile iliyotolewa na klabu ya Manchester United ya England ingawa chanzo hicho hakikueleza ni kiasi gani Man United wameofa kwa klabu hiyo yenye makazi yake kaskazini mwa jiji la London.

Twanga yazindua albam ya 12 na kuadhimisha miaka 15 ya kuzaliwa!


Dansa Mandela akifanya yake jukwaani.
 Bendi kongwe ya jijini Dar es Salaam, The African Stars (Twanga pepeta sugu) Kisima cha burudani nchini Tanzania, jana katika viwanja vya leaders club walizindua albam yao ya 12 iendayo kwa jina Nyumbani ni nyumbani, vile vile bendi hiyo iliadhimisha miaka 15 tangu kuzaliwa rasmi mwaka 1998.


Rapa Diof na Dogo Rama wakiwasha moto
Vipaji vingi; Kalala Junior akiimba moja ya nyimbo wlizozindua jana.

Saleh Kupaza akpaaza sauti yake jukwaaani
Na Hadija Kalili wa Bongo weekend Blog
Mope akiwa na shabiki mtasha wa Twanga
Hadija na Matinda
Hapo sasa hapo.........




AMigo Las Baba naa Sofii

Kiongozi wa bendi Mamaa Luiza Mbutu aki pose!