12/04/13

Tom Daley asema yeye ni shoga!

Tom Daley(20)akionesha medali yake

Tom Daley Akiwa mchezoni
Mruka majini bingwa wa medali 2 za Olimpiki Muingereza Tom Daley(20) juzi alichukua uamuzi wa kujitangaza hadharani kupitia mtandao wa YUOTUBE kuwa yeye ni shoga. Kijana huyo mkazi wa Portsmouth, England anasemekana 
kuangukia katika penzi la mcheza sinema Dustin Lance Black ambaye ni muasisi wa chama cha kutetea haki cha American Foundation for Equal Rights ambacho kimekuwa mstari wa mbele kutetea ushoga na haki zake.
Dustin Lance Black(40) ndiye sugar daddy wa wa Kijana mtanashati Tom Daley.
Elton John na kidosho wake David Furnish
Hata hivyo si ajabu kwa nchi ya England kuwa na watu mashuhuri mashoga nao ni pamoja na Elton John, George Michael ambaye ameoana na David Furnish na hata viongozi wa seriikali hasa Dave Cameron alipata kusikika akitaka kuzishinikiza nchi zinazosaidiwa na England ziwape haki mashoga nchini ikiwemo Tanzania, baadae Cameron alikanusha habari hizo. 
Habari na picha kwa hisani ya mirroronline

Mfanyakazi wa SWISSPORT Dar es Salaam afariki ghafla!

Salustian Boniface Clement alizaliwa 07/4/1962 na kufariki 29/11/2013.
Familia ya Salustian inasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wao Bw Salustian Clement kilichotokea ghafla siku ya Ijumaa jijini Dar es Salaam. Taarifa za msiba huu ziwafikie Familia ya Oswald Ndibalema waliopo England na popote pengine walipo, familia ya Lwakatere popote walipo pamoja na ndugu na jamaa wote wa marehemu. Marehemu Salustian ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya SWISSPORT ameacha mke na watoto watatu. Mwili wake unatarajiwa kusafirishwa leo kwenda mjini Bukoba yatakayofanyika kesho mchana mjini hapo.
Habari na picha kwa hisani ya Edgar Oswald
Mwili wa Marehemu ulipokuwa ukisafishwa kwenda Airport.

Hapa ni kanisa Katoliki la Chang'ombe jijini Dar ambapo mwili wa marehemu uliagwa.Mungu ailaze roho yake pema peponi Ameen!