06/26/15

George Nganda afariki dunia!


George Nganda (38) mkazi na mzaliwa wa Kinondoni B Mtaa wa Isere alifariki dunia juzi usiku kuamkia jana baada ya kuugua mapafu. Akiongea na mtandao huu Bw Ivan Minja ratibu wa Kundi la wakazi na waliokuwa wakazi wa Kinondoni ameeleza kusikitishwa na kifo cha ghafla cha kijana mwenzao ambaye wamekuwa wote katika mitaaa ya Kinondoni, Bw Minja alisema "Kama jumuiya ya wana Kinondoni tunatoa pole nyingi kwa wafiwa nikimaanisha familia ya marehemu lakini pia pole ziende kwa wanachama wote wa Kundi la Kinondoni katika  mitandao ya Facebook na Telegram. aliendelea kuesma "George alikuwa rafiki yetu na tutamkosa sana baada ya kututoka. aliongeza "Kama jumuiya tumekuwa tukihimizana kuchanga pesa kidogo ili tumzike mwenzetu aliyetangulia mbele za haki na kwa kweli michango inaenda vizuri sana, labda nichukue fursa hii kuwapongeza wanachama wote ambao wametoa michango na miwahimize ambao hawajatoa watoe ili pesa hizo zisaidie shughuli za msiba na hatimaye mazishi.

Marehemu George Nganda ambaye hakuacha mke wala mtoto atazikwa kesho saa kumi katika makaburi ya Mwembe jini