September 2015

Harusi ya mwana TBN Dickson Busagaga ilivyofana!


dickson busagaga & salome mhozya wedding (9)
Dickson Busagaga na Salome Mhozya katika picha baada ya kufunga ndoa iliyowafanya kuungana na kuwa mwili mmoja tukio lililofanyika katika kanisa la Mt. Teresia wa Mtoto Yesu jimbo kuu la Tabora mnamo tarehe 23 Sep, 2015.
dickson busagaga & salome mhozya wedding (8)
Waharusi (Dickson na Salome) wakionesha pete zao mara baada ya kuungana na kuwa kitu kimoja.
dickson busagaga & salome mhozya wedding (2)
Hakika ilikuwa ni siku ya furaha sana kwao, hata walipoingia ukumbini katika sherehe ya usiku walidhihirisha kuto kubahatisha kuungana kwao.
dickson busagaga & salome mhozya wedding (3)
Furaha ilitawala sana miongoni mwao na waalikwa wote.
dickson busagaga & salome mhozya wedding (4)
dickson busagaga & salome mhozya wedding (5)
dickson busagaga & salome mhozya wedding (6)
MC Ndagula katika ubora wake wa kazi.
dickson busagaga & salome mhozya wedding (7)
ZIFUATAZO NI PICHA ZA SENDOFF ILIYOFANYIKA TAREHE 19/09/2015 ORION

(TABORA HOTEL)

salome_mhozya_sendoff (1)
Picha ya pamoja ya maids, matron na aliyekuwa bibi harusi mtarajiwa
salome_mhozya_sendoff (2)
salome_mhozya_sendoff (3)
Mrs Patrick na Salome (aliyekuwa bibi harusi mtarajiwa) wakiingia ukumbini
salome_mhozya_sendoff (4)
salome_mhozya_sendoff (5)
salome_mhozya_sendoff (6)
salome_mhozya_sendoff (7)
salome_mhozya_sendoff (8)
Wazazi wa Salome wakisalimia waalikwa katika sherehe za kumuaga mtoto wao Salome.
salome_mhozya_sendoff (9)
salome_mhozya_sendoff (10)
Wanakamati katika ubora wao wa kukabidhi zawadi za kamati
salome_mhozya_sendoff (11)
Dickson Busagaga, Mume halala wa Salome.
salome_mhozya_sendoff (12)
Bw. Patrick (Best man)
salome_mhozya_sendoff (13)
salome_mhozya_sendoff (14)
salome_mhozya_sendoff (15)
salome_mhozya_sendoff (16)
salome_mhozya_sendoff (17)
salome_mhozya_sendoff (18)
salome_mhozya_sendoff (19)
Picha na aloyson.com -TBN Tabora

Kalapina aunguruma Mtambani kata ya Mzimuni!

Karama Masoud aka Kalapina akihutubia wakazi wa eneo la Mtamba kata ya Mzimuni leo jioni







Mwanaharakati Kalapina akimwaga sera kwa wakazi wa Magomeni Mikumi leo

Picha na Hassan Kachloul

Zetrida Ezekiel atoka na Ringa na Yesu!


Zetrida Ezekiel ni mwanamuziki mahiri wa muziki wa injili aishiye mkoani Kigoma, amekuwa mwanamuziki wa nyimbo za injili ambaye ni mwana kwaya wa  kikundi maarufu na kikongwe cha nyimbo za injili cha MKE MWEMA cha mjni Kigoma. Zetrida ameolewa na ni mama wa watoto wanne, wa kike wawili na wa kiume wawili.

Lakini baada ya kupata rai nyingi na kwa muda mrefu toka kwa wachungaji wake na watu mbali mbali kuwa atengeneze albamu yake kama mwanamuziki wa kujitegemea,hatimae mwezi wa August mwaka huu Zetrida alikuja Dar es Salaam na kuanza kazi ya kutengeneza albam yake binafsi.
Zetrida Ezekiel akiwa katika pozi.



Album yake inayoitwa Ringa na Yesu ina nyimbo nane na nyimbo zote amezifanyia Tika records chini ya mtayarisha muziki maarufu nchini aitwaye Ephraim Kameta ambapo nyimbo sita katika albam yake hiyo zilitengenezwa na Kameta na mbili zikitengenezwa mtayarisha muziki machachari PG zote katika studio za Tika records pia. Katika albam hiyo kuna nyimbo kama Ringa na yesu liyobeba jina la albam Malaika, waombee maadui zako na nyingine nyingi zenye kiwango cha hali ya juu.

Akiongea na mtandao huu kwa njia ya simu Zetrida alipoulizwa ana mipango gani ya kufanya video ya albam hiyo Zetrida alisema "Natamani sana hata leo nianze kuandaa video lakini pesa inagomba kwa saa hasa baada ya kutoka kuandaa albam hii ya audio ambaye imechukua pesa nyingi kuandaa, inabidi nijpange tena kwanza"
Na alipoulizwa nini mipango yake ya baadae baada ya lutoa albamhiyo alisema "Mipango yangu ya baadae ni kumtangaza Yesu ndani na na nje ya Tanzania kwa kuwa ni kitu kilicho ndani ya damu yangu" Pia alielezea changamoto alizokutana nazo wakati akitayarisha albam hiyo ni pamoja kutofanya kazi kwa wakati uliopangiwa jambo ambalo hutokana na sababu mbali mbali ikiwemo katikizo la umeme, ambapo inatokea kazi iliyokuwa ifanyike jana inahamishiwa leo na wa leo ama utafanya kazi mida mibaya au kupangiwa siku nyingine. Lakini nashukuru sana kuwa nimeeza kumaliza albam hiyo bila tatizo.

Mwisho kabisa Zetrida alipenda kutoa shukurani zake akisema "Napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa ujasiri wa kufanya albam yangu mwenyewe na pili mume wangu kwa kuniruhusu kufanya kazi hii ya uimbaji pia kujitoa kwake kwa hali na mali, vile vile bila kumsahau Mchungaji Joseph Malumbu wa Kijichi Mtongani ambaye alihusika katika usimamaizi wa albam ya Ringa kwa Yesu. Pia niwaombe tu wapenzi wa muziki wa injili waipokee albam yangu na wainunue kwa wingi kwani humo kuna nyimbo nzuri sana zenye kumtukuza Bwana Yesu hivyo kila mmoja ajipatie nakala yake sasa kwani tayari albami ipo madukani.
Kwa mialiko popote ndani na nje ya Tanzania wasiliana naye kwa nambari
+255675 406917/ +255756823477
au kwa barua pepe
zetridaezekiel@yahoo.com 

Nipeni mwaka mmoja tu muone mabadiliko Kinondoni!- Karama (Kalapina) Masoud

Mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bw Karama Masoud aka Kalapina akiwahutubia wakazi wa Kinondoni Moscow kituo cha polisi jijini Dar es Salam leo jioni.
Msanii maarufu wa muziki wa kufoka foka nchini Bw Karama Masoud (Kalapina) leo hii aliendelea na kampeni zake za kutafuta kura katika jimbo la Kinondoni ambapo leo alifanya mkutano Kinondoni Moscow kituo cha polisi mkutano ambao ulihudhuriwa na wagombea udiwani wa kata za Ndugumbi, Magomeni, Mzimuni na Kigogo.



Awali wasanii wa muziki wa kizazi kipya Domokaya, TID, KR Mullah wa TMK Family walitoa burudani safi kwa wakazi wa eneo hilo waliohudhuria mkutano huo wa kampeni. Hata hivyo katika hali ya kustaajabisha ilitokea sintofahamu katika mkutano huo baada ya generator mbili kushindwa kufanya kazi na kuufanya mkutano huo kusimama kwa muda, ambapo ilifuatwa generator nyingine ya tatu ambayo nayo ilichukua muda mpaka ilipoweza kufanya kazi. 

Akiongea kwa hisia kali na wapiga kura hao, Kalapina alisema "Nikiwa mzaliwa na niliyekulia Kinondoni naelewa matatizo yenu kuanzia mazingira machafu, mafuriko ya mara kwa mara na gonjwa hatari la kipindupindu  na mengineyo mkinipa kura za kuniwezesha kwenda bungeni nitahakikisha katika kipindi cha mwaka mmoja tu mtaona mabadiliko ya mazingira hapa Kinondoni na ninawaruhusu nisipotekeleza mje mnifanyie fujo nyumbani kwangu na hata polisi wakija nitawaambia wananchi wangu wana haki ya kufanya wafanyalo kwa kuwa sijatimiza ahadi zangu.

Akimuelezea mbunge aliyepo sasa Mh Idi Azan alisema "Kwa miaka 10 sasa hali ya mazingira ya Kinondoni imedorora, Idi Azan hana lolote alifanyalo yani yupo yupo tu" aliongeza kusema "Kama kuna mtu yupo hapa alipata kumsikia Idi Azan akiongea chochote aje hapa aniambie nitampa sh elfu 10, jambo ambalo lilizua kelele za watu wakisema hawajawahi kumsikia akiongea chichote bungeni"
  

Baadhi ya wakazi wa Kinondoni Moscow wakimsikiliza mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bw Kalapina leo jioni.
Mbgombea ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bi Asma (mwenye kilemba cha zambarau) akifuatilia hotuba mbali mbali mbali katika mkutano wa kampeni ya ubunge leo.
Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama cha ACT Bw Nixon Tugara akihutubia wakazi wa Kinondoni Moscow
Mgombea ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bi Asma akiwasalim wakazi wa Kinondoni Moscow waliojitokeza kumsikiliza mgombea ubunge wa jimbo hilo Bw Karama Masoud. 

Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Q Chillah (fulana nyeupe) na TID (mwenye miwani na balaghashia) wakifuatilia mkutano baada ya kufanya maonesho kabla ya mkutano huo kuanza.
Baaadhi wa wafuasi wa Bw Kalapina ambaye ni mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni wakifuatilia mkutano.
Wagombea udiwani kwa tiketi ya ACT Wazalendo wa kata za Ndugumbi, Mzimuni, Kigogo na Magomeni wakitambulishwa kwa wapiga kura wa Kinondoni Moscow.
Mshabiki wa mgombea wa ACT Wazalendo ubunge wa jimbo la Kinondoni akishangilia huku akiwa kabeba bango lenye picha ya mgombea huyo.

Mgombea wa udiwani kata ya Hananasif wa ACT Wazalendo Bw Baruani aka Komandoo akiwasalim wapiga kura wake.







Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama cha ACT wazalendo Bw Nixon Tugara kulia na Bi Asma wakiwa jukwaani


Mgombea wa ubunge kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bw Karama Masoud Kalapina katikati akifuatilia mkutano huo wa kampeni.
Bi Asma akimtambulisha Kalapina kwa wapiga kura wa Kinondoni Moscow kituo cha polisi.

Kalapina akimwaga sera makini
Picha na habari na Mkala Fundikira