02/09/14

Kwani timu yako ikifungwa goli tano lazima uanguke?

Baada ya timu ya Arsenal (The Gunners) jana kupokea kipigo kikali kilichoendana na maumivu makali cha goli 5-1 toka kwa timu ya Liverpool (Bwawa la maini) aka (Liverfools) kocha Arsene Wenger aliteleza na kuanguka nje ya stesheni ya treni ya LIVERPOOL LIME STREET akiwa anaelekea kupanda treni kuelekea London baada ya mchezo huo wa Barclays Premier league ambapo askari wawili walikimbilia kumuinua kutoka hapao alipoangukia. Wenger alionekana mwenye maumivu makali kufuatia mwereka huo ambapo mashabiki wengi wa Manchester United wamedhihaki wenzao wa Arsenal kuwa mwereka huo ni kiwewe cha kufungwa na Liverpool na hatimaye kupoteza uongozi wa ligi hiyo maarufu duniani.


Ouch!

Maumivu makali!
Pole baba,haya simama!

Picha kwa hisani ya Twitter/TSBible, habari kwa hisani ya mailonlne