mkalamatukio: MATUKIO
Showing posts with label MATUKIO. Show all posts

Pombe Yahusishwa, Ajali Mbaya ya Bodaboda..! Askari Nao Jee..?

Kamera ya mtandao huu imelimulika tukio baya la ajari iliyohusisha pikipiki mbili eneo la Club Royal karibu na lango la kuingilia chuo cha Utumishi wa Umma cha Tabora zamani UHAZILI.

Mfuatiliaji wa tukio alibainisha dereva mmoja alikuwa anatokwa na harufu ya pombe kitu kilichodhihirisha kuwa alikuwa amelewa huku kamchukua abiria na akiendesha chombo cha moto.

Mashuhuda waliuambia mtandao huu kuwa wanalalamikia jeshi la polisi kuto kujitokeza mapema eneo la tukio licha ya kuwa hapana umbali unaozidi mita 100 kutoka eneo la tukio, mfuatiliaji wa tukio aliwahoji kama kuna yeyote aliyetoa taarifa kituoni dhidi ya tukio hilo lakini hakupata majibu.
Kasendeka, mhanga wa ajali iliyohusisha pikipiki mbili maarufu kama bodaboda.
Kasendeka, mhanga wa ajali iliyohusisha pikipiki mbili maarufu kama bodaboda eneo ilipo Club Royal karibu na lango kuu la kuingilia Chuo Cha Utumishi cha Tabora zamani kikifaahamika kama UHAZILI.
Kasendeka akiwa anazinduka ziduka, akili inakuja baada ya kuzimia kwa muda kidogo kufuatia ajali iliyohusisha pikipiki mbili eneo la ilipokuwa Club Royal.
Kasendeka akiwa anazinduka ziduka, akili inakuja baada ya kuzimia kwa muda kidogo kufuatia ajali iliyohusisha pikipiki mbili eneo la Club Royal karibu na lango/ geti la kuingilia Chuo Cha Utumishi wa Umma zamani UHAZILI.
Ajali-bodaboda-tabora (5)
Abiria na mhanga wa ajali hiyo akiwa anaugulia maumivu baada ya ajali iliyotokea muda mfupi maeneo ya Club Royal karibu na geti kuu la kuingilia Chuo Cha Utumishi wa Umma zamani UHAZILI
Abiria na mhanga wa ajali hiyo akiwa anaugulia maumivu baada ya ajali iliyotokea muda mfupi maeneo ya Club Royal karibu na geti kuu la kuingilia Chuo Cha Utumishi wa Umma zamani UHAZILI
Ajali-bodaboda-tabora (2)
Ajali-bodaboda-tabora (3)
Mashuhuda wa tukio la ajali iliyohusisha pikipiki mbili maeneo ya Club Royal
Mashuhuda wa tukio la ajali iliyohusisha pikipiki mbili maeneo ya Club Royal
Kasendeka akiwa anaangalia pikipiki yake baada ya ajali hiyo muda mfupi alipozinduka.
Kasendeka akiwa anaangalia pikipiki yake baada ya ajali hiyo muda mfupi alipozinduka.
Askari wa Jeshi la usalama barabarani akijongea eneo la tukio. Inakadiriwa ni zaidi ya dakika 15 au zaidi zilipita ndipo askari alijitokeza eneo la tukio licha ya tukio hilo kutokea umbali wa mita za makadirio zisizozidi 100.
Askari wa Jeshi la usalama barabarani akijongea eneo la tukio. Inakadiriwa ni zaidi ya dakika 15 au zaidi (Kwa mujibu wa mashuhuda) zilipita ndipo askari alijitokeza eneo la tukio licha ya tukio hilo kutokea umbali wa mita za makadirio zisizozidi 100 kutoka kituo kukuu cha Polisi mjini Tabora.
Askari akifuatilia tukio hilo baada ya dakika zinazokadiriwa na mashuhuda wa tukio kuwa ni zaidi ya 15 toka ajari imetokea.
Askari akifuatilia tukio hilo baada ya dakika zinazokadiriwa na mashuhuda wa tukio kuwa ni zaidi ya 15 toka ajari imetokea.
Askari akimhoji Kasendeka kabla ya kwenda naye kituoni huku mhanga mmojawapo kuwa tayari alishakimbia eneo la tukio na kuisaliti pikipiki eneo la tukio.
Askari akimhoji Kasendeka kabla ya kwenda naye kituoni huku mhanga mmojawapo kuwa tayari alishakimbia eneo la tukio na kuisaliti pikipiki eneo la tukio.
Ajali-bodaboda-tabora (1)
Picha na Aloyson

Over pass yaporomoka na kuua watu wawili Brazil!

Barabara  mpya ya juu (over pass) iliyokuwa ikijengwa mjini Belo Horizonte nchini Brazil iliporomoka jana (Alhamisi) na kuanguakia malori matatu, gari dogo na basi la kusafirishia abiria na kusababisha vifo vya watu wawili na majeruhi 19. Hata hivyo maafisa wa uokoaji wameeleza kuna nafasi kubwa ya miili mingine kupatikana chini ya barabara hiyo. Barabara hiyo ilijengwa ili kupunguza msongamano katika kipindi hiki cha world cup nchini Brazil ambapo mjini Belo Horizonte ambapo pana uwanja wa Mineirao ambao utatumika kwa mchezo wa nusu fainali siku ya jumanne katika mfululizo wa fainali za kombe la dunia 2014. 
Kwa juu inaonekana over pass hiyo ikiwa imelala ardhini baada ya kuporomoka
Basi lililoangukiwa na barabara ambamo dereva wake ni mmoja wa watu wawili waliokufa papo hapo hapo jana.
Gari dogo lililoangukiwa na over pass mijini Belo Horizonte, nchini Brazil.
Malori mawili yanaonekana kubanwa na over pass hiyo huku waokoaji wakishauriana 
Uwanja wa Mineirao utakaochezewa mchezo nusu fainali mjini Belo Horizonte uliopo Km 3 toka eneo la ajali.
Picha kwa hisani ya AFP/ habari na mirror online

Hali ya hewa ilivyotesa Huko kaskazini mashariki mwa Marekani wikiendi iliyopita!

Gari dogo likiwa imeacha barabara baada ya theluji nyingi kudondoka na kupelekea dereva wa gari hilo kupoteza mwelekeo na kutumbukia pembezoni mwa barabara(Free way)
Wikiendi iliyopita ilikuwa ni ya heka heka kubwa katika miji iliyo Kaskakazini mashariki mwa nchi ya Marekani ambapo barabara nyingi zilipitka ama kwa taabu au kutopitika kabisa katika majimbo ya Pennsylyvania na New Jersey ambapo pia imeelezwa kulikuwa na uchelewesho katika usafiri wa anga ambapo baadhi ya wasafiri walishindwa kuelekea waendako kwa takribani masaa matano hivi. Hata hivyo hali ilielekea kurudi katika ukawaida wake kuanzia j3 kwa maeneo ya Philadelphia na kwingineko.
Hali ya hewa ikiwa tata katika barabara hii ambapo kama ionekanavyo gari kadhaa zimepatwa na ajali hivyo kushindwa kuendelea na safari na pia kuziba kabisa upitikaji wa barabara hiyo wikiendi iliyopita.
Watoto nao walipata muda wa kuchezea snow
Misururur mikubwa ya magari ilionekana maeneo mengi huko America wikiendi iliyopita
Hata mitaani pia hapakusamehwa na hali mbaya ya hewa
Ramani hii ilionesha maeneo yaliyoathirika zaidi.
Picha na habari kwa hisani ya kijana mpole Francis Wali Ngula aka Baba Wamali kutoka Mount Laurel, New Jersey

Tom Daley asema yeye ni shoga!

Tom Daley(20)akionesha medali yake

Tom Daley Akiwa mchezoni
Mruka majini bingwa wa medali 2 za Olimpiki Muingereza Tom Daley(20) juzi alichukua uamuzi wa kujitangaza hadharani kupitia mtandao wa YUOTUBE kuwa yeye ni shoga. Kijana huyo mkazi wa Portsmouth, England anasemekana 
kuangukia katika penzi la mcheza sinema Dustin Lance Black ambaye ni muasisi wa chama cha kutetea haki cha American Foundation for Equal Rights ambacho kimekuwa mstari wa mbele kutetea ushoga na haki zake.
Dustin Lance Black(40) ndiye sugar daddy wa wa Kijana mtanashati Tom Daley.
Elton John na kidosho wake David Furnish
Hata hivyo si ajabu kwa nchi ya England kuwa na watu mashuhuri mashoga nao ni pamoja na Elton John, George Michael ambaye ameoana na David Furnish na hata viongozi wa seriikali hasa Dave Cameron alipata kusikika akitaka kuzishinikiza nchi zinazosaidiwa na England ziwape haki mashoga nchini ikiwemo Tanzania, baadae Cameron alikanusha habari hizo. 
Habari na picha kwa hisani ya mirroronline

Mfanyakazi wa SWISSPORT Dar es Salaam afariki ghafla!

Salustian Boniface Clement alizaliwa 07/4/1962 na kufariki 29/11/2013.
Familia ya Salustian inasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wao Bw Salustian Clement kilichotokea ghafla siku ya Ijumaa jijini Dar es Salaam. Taarifa za msiba huu ziwafikie Familia ya Oswald Ndibalema waliopo England na popote pengine walipo, familia ya Lwakatere popote walipo pamoja na ndugu na jamaa wote wa marehemu. Marehemu Salustian ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya SWISSPORT ameacha mke na watoto watatu. Mwili wake unatarajiwa kusafirishwa leo kwenda mjini Bukoba yatakayofanyika kesho mchana mjini hapo.
Habari na picha kwa hisani ya Edgar Oswald
Mwili wa Marehemu ulipokuwa ukisafishwa kwenda Airport.

Hapa ni kanisa Katoliki la Chang'ombe jijini Dar ambapo mwili wa marehemu uliagwa.Mungu ailaze roho yake pema peponi Ameen!

Shabiki wa Ajax ajeruhiwa vibaya baada ya kuanguka toka jukwaani

Watoa huduma ya kwanza wakimhudumia shabiki aliyeanguka akishangilia goli la pili.

Mshabiki wa timu ya Ajax Amsterdam ambaye hakutajwa jina, jana alianguka alipokuwa akishangilia bao la  pili la timu yake dhidi ya Fc Barcelona lililofungwa na Danny Hoesen. Inakadiriwa mtu huyo alianguka toka urefu wa futi 16 alikutwa kalala katika dimbwi la damu
Baadae watu wa huduma ya kwanza toka kwa magari mawili ya Ambulance na helikopta moja walimtibu mtu huyo na kumpeleka hospitali. Ajax ilifanikiwa kuifunga Barcelona katika mchezo huo wa Ubingwa wa Ulaya. Lakini haikufahamika hali ya mshabiki aliyeanguka ilikuwa ikiendeleaje.
Amsterdam Arena ionekanavyo kwa nje.


Mama Hawa Haji Kamanga kuzikwa kesho!

Marehemu Bibi Hawa Kamanga 1941-2013
Mama Hawa Kamanga ambaye alifariki leo hii asubuhi mnamo saa 2:40 katika hospitali maalum ya wagonjwa wa Saratani ya Ocean Road ya jijini Dar es Salaam ameacha watoto 6, wa kiume watano na wa kike mmoja. Kati ya hao watatu wanaishi marekani nao ni Haji, Kaela na Hizza. Wengine wawili wa kiume wanaishi Tanzania ambao ni  Zakaria (kaka mkubwa) na Pioka. Na mmoja wa kike  Anna Kange anaishi Holland, Marehemu ameacha wajukuu 11 na kitukuu mmoja. Baada ya wanafamilia kukaa kikao, imeamuliwa kuwa marehemu atazikwa kesho saa 10:00 jioni katika makaburi ya Kisutu na shughuli zote za msiba zipo Sinza Vatican. 

Blog hii imnesikitishwa sana na kifo hiki, mwandishi wa habari hii alipata kumtembelea marehemu alipokuwa amelazwa kwa Dk Mvungi wiki tatu zilizopita. Blog inawapa pole watoto,wajukuu, ndugu, jamaa na marafiki wote wa marehemu!

MUNGU AILAZE ROHO YAKE PEMA PEPONI! AMIN


Chanzo cha habari na picha Hizza Kamanga,Grace Mmari, Houston Texas/ Tausi Khalid Dar, Tanzania.

Bibi afariki saa 48 baada ya kujua wajukuu zake wamefika hospitali kumuona!

Katika hali ya kusikitisha Mama Hawa Haji Kamanga (71) alifariki leo hii saa 2.40 Hospitalini Ocean Road  baada ya kupigania uhai wake kwa siku kadhaa alizokuwa na hali mbaya sana lakini ilielekea alipigana kubaki hai mpaka pale wajukuu zake wawili walipofika toka America siku ya Jumamosi na kwenda moja kwa moja Ocean Rd Hospital kumuona Bibi yao. Wajukuu zake hao Kaela Jr (3)na Hadassah Bianca (1) walipofikishwa wodini Marehemu akaambiwa wajuu zako wamekuja kukuona inasemekana marehemu aliyekuwa na hali mbaya kwa wakati huo alitabasamu na kujaribu kusema kitu lakini hakuweza kutoa sauti, lakini bila shaka alifurahi kujua hatimaye wajukuu zake wamemkuta akiwa hai, na hatimaye akaamua muda ulikuwa sahihi kuacha kupigania uhai wake. Mama Hawa Kamanga ana watoto kadhaa wanaoishi nchini Marekani. Marehemu alilazwa Ocean Road wiki mbili hivi baada ya kuhamishiwa hapo kutokea katika hospitali ya Dk Mvungi ambako alilazwa kwa uchunguzi wa awali. Kwa sasa mipango ya mazishi inafanyika na tutaendelea kufahamishana humu na kwingineko.
    Inna Lillah wa inna illahi Rajiun!

[Video] KISOMO CHA MWISHO CHA MAMAA NYAWANA FUNDIKIRA MDA MFUPI KABLA YA MAZISHI

UHARAKA WA MUDA WA KUHAKIKISHA MWILI WA MAREHEMU UNAZIKWA ULIZINGATIWA TU MARA BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUWASILI TABORA MNAMO SAA 12 JIONI. KISOMO CHA MWISHO NA MAOMBI YA MWISHO ILIFANYWA KISHA KUELEKEA KATIKA MAZIKO YA MWILI WA NYAWANA FUNDIKIRA KATIKA MAKABURI YA ITETEMYA AMBAKO IKO IKULU YA MACHIFU WA UKOO WA FUNDIKIRA. 
ILIPOFIKA MUDA WA SAA 1:10 USIKU SHUGHULI YA MAZIKO ILIENDELEA NA KUHAKIKISHA MWILI WA MAREHEMU UMEPUMZISHWA.

*UMATI MKUBWA WA WATU ULITANDA PEMBEZONI MWA BARABARA WAKISHUHUDIA MSAFARA WA KUELEKEA KATIKA MAZISHI, ILIKUWA NI MAAJABU HAIJAWAHI TOKEA HAPO MKOANI*
UMATI WA WATU NJIANI KUELEKEA MAZISHI YA NYAWANA 
[TUNAOMBA RADHI KWA VIDEO HII KWANI HAIJACHUKULIWA KATIKA MAZINGIRA BORA, VIKWAZO VILIKUWA VINGI IKIWEMO MWENDOKASI WA GARI NA GIZA]

PICHA ZA MAZISHI YA NYAWANA FUNDIKIRA

MAMAA NYAWANA AMEPUMZISHWA KATIKA MAKAZI YAKE YA MILELE KATIKA MAKABURI YA ITETEMYA HAPA MKOANI TABORA, NJE KIDOGO NA MJI
MAZISHI YAMECHELEWESHWA KUTOKANA NA KUCHELEWA KUWASILI KWA MWILI HUO WA MAREHEMU

Umati unaosubiri mwili wa Nyawana umevunja rekodi!


Kadri muda uendavyo ndivyo watu wamezidi kufika ulipo msiba wa Nyawana Fundikira, maeneo ya Gongoni, Tabora mjini. Hata hivyo mwili wake umechelewa kidogo kuwasili mjini hapa lakini watu wameendelea kujazana wakikaa juani bila taabu yeyote. Hii ni ishara kuwa watu wa Tabora walimkubali sana Nyawana ambaye wao walipenda kumwita Mamaa Nyawana au Jembe! kwani watu wapatao elfu moja wamejitokeza kushuhudia au kutoa heshima za mwisho kwa Nyawana.

Sheikh akitoa mawaidha mawili matatu kwa wahudhuriaji








Waombolezaji wakisubiri mwili wa Marehemyu Nyawana uwasili kutoka Dar es Salaam.






Chakula kikiandaliwa



Waombolezaji wakiwa katika hali ya huzuni kubwa kwa kuondokewa na kipenzi cha Tabora Mamaa Nyawana
Huzuni huzuni huzuni!