Mfanyakazi wa SWISSPORT Dar es Salaam afariki ghafla!

Mfanyakazi wa SWISSPORT Dar es Salaam afariki ghafla!

Salustian Boniface Clement alizaliwa 07/4/1962 na kufariki 29/11/2013.
Familia ya Salustian inasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wao Bw Salustian Clement kilichotokea ghafla siku ya Ijumaa jijini Dar es Salaam. Taarifa za msiba huu ziwafikie Familia ya Oswald Ndibalema waliopo England na popote pengine walipo, familia ya Lwakatere popote walipo pamoja na ndugu na jamaa wote wa marehemu. Marehemu Salustian ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya SWISSPORT ameacha mke na watoto watatu. Mwili wake unatarajiwa kusafirishwa leo kwenda mjini Bukoba yatakayofanyika kesho mchana mjini hapo.
Habari na picha kwa hisani ya Edgar Oswald
Mwili wa Marehemu ulipokuwa ukisafishwa kwenda Airport.

Hapa ni kanisa Katoliki la Chang'ombe jijini Dar ambapo mwili wa marehemu uliagwa.Mungu ailaze roho yake pema peponi Ameen!