05/19/13

Warembo wa Redds Miss Tabora 2013 waenda kuzuru tembe la Dr Livingstone

Mzee Hamisi 
Kamati ya Redds Miss Tabora 2013 jana iliwapeleka warembo wao katika kijiji cha Kwihara kilometa 12 hivi toka Tabora mjini ambako walizuru tembe la Dr David Livingstone ambaye alikuwa mvumbuzi wa mambo mbali mbali ikiwemo vyanzo vya mito barani Afrika. Washiriki hao walikieleza kituo cha tv cha Clouds kuwa wamefurahishwa na ziara hiyo kwani imewaongezea uelewa juu ya mambo ya kale husasan David Livingstone . Wikiendi ijayo warembo hao wamepangiwa kutembelea nyumba za watoto yatima na wodi ya watoto katika Hospitali ya Kitete ya mjini Tabora.


Bango hili linaonesha tarehe, siku na mwaka aliopita  Livingstone 

Mrembo Cornencia akijitwisha kibuyu

Mrembo Faidha Hamis akijaribu mkufu uliotengenezwa kwa simbi.

Hapa wakimsikiliza Mzee Hamisi

Mrembo Sabrina Juma

TABASAMU

Cornencia akihojiwa na TBC

Pili Issa (Matron) kushoto akimshikia Mic, Cornencia. aliyekuwa akihojiwa na Nidudu Iddy wa Clouds Tv

Anastazia akihojiwa na clouds Tv