mkalamatukio: ENTERTAINMENTS
Showing posts with label ENTERTAINMENTS. Show all posts

Tabora Stand Up; Eid Mosi Wasanii Wafurika Hapatoshi.

Shangwe na burudani za kutosha zinatarajiwa kufanyika katika sikukuu ya Eid hapo kesho mkoani Tabora panapo majaaliwa ya M/Mungu. Mashabiki mbalimbali mjini Tabora watarajiwa kufurahia onesho hilo katika maeneo mawili tofauti ambapo mchana itakuwa Bwalo la Polisi kuanzia saa 8 mchana na Usiku katika viwanja vya Muungano Mesi kuanzia saa 2 usiku.
Wasanii wa kila nyanja wametua mjini hapo na kufanya mahojiano CG Fm Redio leo mchana; wasanii hao ni Kassim Mganga a.k.a tajiri wa mahaba, Ommy Dimpoz, Mkude Simba (Kitale) na rafiki yake Stan Bakora, Young Killer, na Baraka Da Prince.
Eid_Tabora (8)
Kassim Mganga akiwa CG Fm Redio, 89.5 The point of no Return
Eid_Tabora (11)
Ommy Dimpoz
Eid_Tabora (4)
Eid_Tabora (7)
Manoni (Mtangazaji CG Fm Redio 89.5 The Point of no Return) akifanya mahojiano na wasanii.
Eid_Tabora (13)
Mkudesimba Original (Kitale)
Eid_Tabora (14)
Kitale na Stani Bakora, ...eti "Tembo wa Ulaya mkubwa sana kama mbuzi"
Eid_Tabora (17)
Stan Bakora
Eid_Tabora (9)
Baraka Da Prince
Eid_Tabora (16)
Stephania (Mtangazaji CG FM)
Eid_Tabora (15)
Eid_Tabora (12)
Young Killer (Handsome aliyekosa matunzo) akishuka free style.
Eid_Tabora (5)
Mgalula Fundikira (Mkurugenzi wa Royal Nsyepa Entertainment) akizungumzia maandalizi ya onesho hilo aliloliandaa baada ya muda mrefu toka arudi kutoka Hispania
Eid_Tabora (3) Eid_Tabora (2) Eid_Tabora (18)
Kutoka kushoto, Kassim Mganga, Mubenga (Meneja wa Ommy Dimpoz), Stan Bakora na Abdul katika nyumba za Tabora Rest House walikofikia wasanii hao.
Eid_Tabora (19)  
Wakijipima uwezo wa ukali wa "SAUM"
Picha na Aloyson -TBN Kanda ya magharibi

Mpigie kura Ally Baucha ashinde Kili Music Awards!

Msani machachari Ally Baucha ambaye kupitia wimbo wake Kelele aliomshirikisha Ally Kiba ameteuliwa kushiriki katika kinyang'anyro cha kugombea tuzo za Msanii anayechipukia ambapo amepewa namba 23 na vile vile amepewa namba 26 katika kugombea tuzo ya msanii bora mtumbuizaji wa kiume. Ili kumpigia kura Baucha fuata maelekezo hapo juu.

Tabora Funga mwaka Bash kuburudishwa wa na Belle9!

Msanii mkali wa Bongo Flava Belle9 atakuwa ni mmoja wa wasanii watatu watakaoburudisha Tamasha la Club Royal Funga Mwaka Bash litakalofanyika mjini Tabora katika ukumbi maarufu wa New Royal Garden. Akiongelea tamasha hilo mmoja wa wadhamini wa tamasha hilo Mashaka Chura aka Mzee wa maini na Figo mkurugenzi wa Chura Fashion alisema maandalizi yamekamilika, wapenzi wa muziki wa Bongo Flava wanaotarajia kwenda kujiachia Ijumaa hii wajitokeze kwa wingi dukani kwake ambapo kuna pamba mpya na kali za kila aina ili watakapoingia katika tamasha hili la kuuaga mwaka 2013 wawe wametisha. Tamasha hilo pia litashuhudia wasanii Squizer na Ziggy Dee aliyetamba na wimbo wa Eno Mic pia wakitumbuiza ukumbini Royal Garden. Tamasha hili limewajia kwa udhamini wa Serengeti Breweries Ltd, Clouds Media Group, Chura Fashion, Gonala Pharmacy, Millenium Barber shop, Tabora Rest House, Nbs Classic, Mtingoni Company Ltd, Mussoma Batteries, CgFm 89.5, VoT fm 89.0 na Clouds Media Group.

BOB JUNIOR KUZINDUA WIMBO MPYA "BASHASHA" KAMSHIRIKISHA VANESSA MDEE

NYIMBO MPYA AMBAYO INAAMINIKA KUWA NI NZURI ZAIDI YA ULIZOWAHI KUZISIKIA ITAKWENDA KWA JINA LA "BASHASHA" 

MWANADADA MKALI VANESSA MDEE NAYE NDANI KASHIRIKISHWA KWENYE NYIMBO HIYO KALI UTAKAYOPATA KUISIKILIZA BAADA YA UZINDUZI WAKE.

SASA ISHU KUBWA NI UZINDUZI WA SINGLE HIYO HAPO TAREHE 27 OKTOBA 2013 JUMAPILI NDANI YA "ClubBilicanas".

********
WASANII KIBAO KUTUA HAPO NI HAWA WAFUATAO: 
BOB JUNIOR NA VANESSA MDEE 
QUEEN DARLEEN 
SAMIR 
CHID BENZ 
CYRIL 
MIRROR 
LINEX 
BONGE LA NYAU 

**********
COMEDY : KUTANA NA MASAI NYOTA MBOFU
TAG: 6,000/=

"MR CHOCOLATE AMEUTHIBITISHIA MTANDAO WA www.aloyson.com KUWA BASHASHA ZILIZOTIWA HUMO LAZIMA ZIWE CHAKULA BORA CHA MASIKIO YAKO KWA KUSUDI LA KUBORESHA MAPENZI YATAKAYOSTAHIKI KUTIWA MABASHASHI YA AINA YAKE..."

ENDELEA KUTEMBELEA MTANDAO HUU KUUPATA WIMBO HUO KUANZIA TAR 27.10.2013

BOB JUNIOR | MASAI NYOTAMBOFU | SAMIR NA MASELE CHA POMBE KUBURUDISHA SIKUKUU YA EID EL HAJ TABORA


Bob junior aka Mr Chocolate Flavor
BOB JUNIOR | MR CHOCOLATE | RAIS WA MASHAROBARO | MTAALAMU WA VIOUNO
NI MSANII NA PRODUCER ANAYETAMBA NA VIBAO KAMA KIMBIJI, ANDAZI  NA NYINGINE NYINGI, KWA MARA YA KWANZA ATADONDOSHA BONGE MOJA LA SHOO SIKU YA EID EL HAJ NDANI YA UWANJA WA ALLY HASSAN MWINYI KWA KIINGILIO CHA 3000 WAKUBWA NA 1000 WATOTO, KUANZIA SAA 8 MCHANA NA USIKU ITAKUWA KATIKA UKUMBI WA THEOFILO KISANJI UNIVERSITY (TEKU) KWA SH 5,000/= NA SH 10,000/= TU KWA V.I.P | NI TAREHE 15 OKTOBA, 2013
 MASAI NYOTAMBOFU MWANAMZIKI NA MSANII WA VICHEKESHO ANAYETAMBA KATIKA VITUKO SHOO YA CHANEL TEN, ATACHEKESHA NA KUIMBA NYIMBO ZAKE MBILI, HAPATATOSHA SIKU HIYO
 KUTANA NA MASELE CHA POMBE | MCHEKESHAJI MAHIRI WA VIYUKO SHOO, NJOO KUTANA NA SWAGA ZA KULEWA BILA KUNYWA LIVE KATIKA MAJUKWAA MAWILI MCHANA NDANI YA ALLY HASSAN MWINYI KWA KIINGILIO CHA SH 3,000/= WAKUBWA NA 1000/= WATOTO MA USIKU NDANI YA UKUMBI WA TEKU (DIAMOND TALKIES) KWA SH 5000/= NA 10,000/= V.I.P
NA SAMIR KUHAMISHIA BAHARI YAKE NA MCHEZO WA KINYULINYULI NDANI YA ARDHI YA WANYAMWEZI.
------------
SHOO INAENDA KWA UDHAMINI WA GONALA PHAMACY | FRANKMAN PALACE HOTEL | NBS CLASSIC (KAMPUNI YA USAFIRI) | CLOUDS FM NA CG FM 89.5
-------------

MSANII: ALLY NIPISHE amepania kuwaona live mashabiki wake wa Tabora

MSANII: ALLY NIPISHE
Msanii wa kizazi kipya anayetamba na vibao kama Ntalila, Nipulika, Daima na milele, Binadam (aliyoimba na AT) na kibao kikali kinachotamba hivi sasa cha MY amepania kuwaona live mashabiki wake wa Tabora huku akimtafuta "MY" siku ya shoo kali ya kumsaka Mrembo wa Chuo Cha Utumishi wa UMMA Tawi la Tabora.

NI TAREHE 27-09-2013
UKUMBI:  TPSC (UHAZILI )FUNCTION HALL
MUDA: MBILI USIKU MPAKA CHWEE
ALLY BAUCHA | PRODUCER, ACTOR NA DANCER
HAPATATOSHA JUKWAA LITAKAPOVAMIWA TENA KWA SUPRISE AMBAYO KILA ATAKAYE KUWEPO ATAJIVUNIA KUMWONA MSANII WA TOFAUTI SANA BONGO ANAYEBEBA SIFA YA NGULI MOJAWAPO NA MFALME WA DUNIA. 
#SUPRISE HAISEMWI WAZI FIKA JIONEE#
BAUCHA ATAKIPIGA KIBAO CHAKE KIPYA KWA MARA YA KWANZA TABORA HUKU AKIKELESHA MASHABIKI KWA KIBAO CHAKE MAARUFU CHA "KELELE"
----------
WADHAMINI:
------
GONALA PHAMACY,SCREENMASTERS,SALUM MCHELE ELECTRONICS|
 FRADO BUSINESS CARE| ALOY SON BLOG| GAMALO PUB|
ROYAL PRODUCTIONS| MKWABI ENTERPRISES LIMITED| MSWAPE ALUMINIUM WORKS| MILLARDAYO.COM|
CG FM 89.5| TABORA REST HOUSE| NBS CLASSIC| CLOUDS FM|
NDIBS COLLECTION| HOLIDAY PARK.
---------

Mapacha watatu wazindua albam Tabora!


UZINDUZI; Chokoraa kushoto na Jose Mara wakizindua album mpya katika ukumbi wa Frankman, Tabora.
Bendi ya Mapacha watatu usiku wa alhamisi katika ukumbi wa Frankman Place mijini Tabora, walizindua album yao mpya iendayo kwa jina la Yarabi nafsi yenye nyimbo nane ambamo kuna watunzi kadhaa akiwemo Jose Mara, Khalid Chokoraa na nyota wengine wakali wanounda bendi hiyo pia wametunga nyimbo kadhaa. Katika hali ya kujutia pengine Bendi hiyo iliwasili Tabora ikiwa na cd chache za albam hiyo mpya ambazo ziliisha bila wao kutegemea

Mdau wa mapacha watatu!

Jon Myuzik avamia Tabora!

Msanii Jon Myusik aki pose!
Kushoto; Mkala, Pili Issa, Jon Myuzik na Danny Kijumbe at Las Vegas pub Tabora
Msanii wa muziki wa kizazi kipya John Myuzik ambaye anatamba na track yake mpya "TONIGHT" yupo Tabora kwa masuala ya ki familia, jana alijumuika na kamati ya Miss Tabora 2013 kwa kubadilishana mawazo mawili matatu na kamati hiyo.

Kushoto;Pili Issa, Aloyson Mlawa, John Myuzik na Danny Kijumbe.

Dayna amtunza shabiki buku kumi!

Dyna na patna wake wa stejini.
Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Bongo Flava Dyna, wikiendi iliyopita alitoa mpya pale alipoamua kumtunza kijana mmoja ambaye yeye Dyna alimwita stejini ili asaidiane naye kuimba wimbo alioimba na Marlow (Mafungu ya nyanya). Kwa mshangao wa wengi kijana huyo pichani aliimba kwa umahiri mkubwa kiasi cha kushangiliwa na watu walioingia ukumbini Royal Garden. Wimbo huo ulipoisha Dayna aliamua kutoa pesa yake mfukoni sh elfu kumi na kumtunza kijana huyo ambaye aliigiza wimbo huo vizuri na kukonga mpaka moyo wa Dayna mwenyewe.
Kazini.
Ile ile.

Hapa Dyna akitoa sh 10,000/=

Majembe; Dj Kali, msanii Man Fley na Mshabiki wa Bongo Flava wakifuatilia show.

Msanii Man Fley na Mshabiki wake

Mmoja wa wamiliki wa klabu ya Royal Adam Fundikira na mkewe Joyce katikati wakifuatili onesho hilo