07/03/14

Over pass yaporomoka na kuua watu wawili Brazil!

Barabara  mpya ya juu (over pass) iliyokuwa ikijengwa mjini Belo Horizonte nchini Brazil iliporomoka jana (Alhamisi) na kuanguakia malori matatu, gari dogo na basi la kusafirishia abiria na kusababisha vifo vya watu wawili na majeruhi 19. Hata hivyo maafisa wa uokoaji wameeleza kuna nafasi kubwa ya miili mingine kupatikana chini ya barabara hiyo. Barabara hiyo ilijengwa ili kupunguza msongamano katika kipindi hiki cha world cup nchini Brazil ambapo mjini Belo Horizonte ambapo pana uwanja wa Mineirao ambao utatumika kwa mchezo wa nusu fainali siku ya jumanne katika mfululizo wa fainali za kombe la dunia 2014. 
Kwa juu inaonekana over pass hiyo ikiwa imelala ardhini baada ya kuporomoka
Basi lililoangukiwa na barabara ambamo dereva wake ni mmoja wa watu wawili waliokufa papo hapo hapo jana.
Gari dogo lililoangukiwa na over pass mijini Belo Horizonte, nchini Brazil.
Malori mawili yanaonekana kubanwa na over pass hiyo huku waokoaji wakishauriana 
Uwanja wa Mineirao utakaochezewa mchezo nusu fainali mjini Belo Horizonte uliopo Km 3 toka eneo la ajali.
Picha kwa hisani ya AFP/ habari na mirror online