02/12/14

Shabiki wa Liverpooll auawa kwa kumkejeli shabiki wa Arsenal!

Raha iliyoje 5-1????
Shabiki wa miaka mingi wa Liverpool Anthony Mutheiya alikufa muda mfupi baada ya firimbi ya mwisho katika mchezo kati ya Liverpool dhidi ya Arsenal jumamosi iliyopita baada ya kuchomwa kwa kisu na shabiki wa Arsenal aliyetambulika kama David Mwangi ambaye anadaiwa alikimbia eneo la tukio Marethe Bar mjini Meru, Kenya ambapo wawili hao walitazama mchezo huo pamoja, ilisemekana Mutheiya alimkejeli Mwangi kupita kiasi na kwa muda mrefu juu ya matokeo ya mchezo huo ambapo Mwangi akashindwa kuvumilia na ndipo alipochomoa kisu na kumchoma nacho Mutheiya ambaye alikimbizwa hospitali lakini akafariki baadaye.