06/18/13

Historia yajirudia Miss Kanda ya Kati 2013

Maua Kimambo Karlstrom Miss Tabora namba mbili 2011.
Miss Tabora namba mbili Sabrina Juma.
 Historia imejirudia tena baada ya warembo wawili wa Redds Miss Tabora 2013 Sabrina Juma na Anastazia Donald kufanikiwa kuingia katika shindano la Taifa (Redds Miss Tanzani 2013) warembo hao wamefuata nyayo za warembo Maua Kimambo aka Maua Karlstrom na Delilah Patrick washiriki wa Miss Tabora 2011 ambao nao waliingia Miss Tanzania baada ya shindano kali la Miss kanda ya kati mwaka 2011. Katika shindano hilo la Redds Miss central zone 2013 lililofanyika mjini Dodoma katika ukumbi wa Kilimani club Ijumaa ya tarehe 14/06/2013 mrembo Happiness Ruta ambaye pia ni Miss Dodoma 2013 alifanikiwa kunyakua taji la Redds Miss Central zone akfuatiwa na mrembo Sabrina Juma aliyeshika nafasi ya pili, huku Miss Singida 2013 akishika nafasi ya tatu. Hata hivyo majaji wakiongozwa na Bw Hashim Lundenga mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania waliona wachukue warembo wanne kwenda Miss Tanzania badala ya watatu baada ya Miss Tabora Anastazia Donald ambaye alishika nafasi ya nne kuweka ushindani mkali na kuwalazimisha majaji kufikiri mara mbili na kuamua kuchukua warembo wanne kitu ambacho Chief Judge Hashim Lundenga alikiri haijawahi kutokea huko nyuma.

Top five.

Miss Tabora 2013 Anastazia Donald.

Delilah Patrick, Miss Tabora namba tatu mwaka 2011