02/11/14

Obama na Beyonce wazushiwa jambo!

Mtandao wa dailystar.co.uk wa nchini Uingereza ambao ni maarufu kwa habari za kidaku, leo hii umechapisha habari ilizodaiwa na mwandishi wa habari Mfaransa Paschal Rostain kuwa gazeti linaloheshimika nchini Marekani la Washinton Post linatarajiwa kuandika habari kuwa the most powerful man in the world, Rais wa Amerika Bw Barack Obama ana mahusiano ya kimapenzi na mwimbaji Byonce Knowles ambaye ni mke wa mwanamuziki Jay-Z. Rostain alikaririwa akisema "Unajua katika siku hizi kuna habari kubwa inatarajiwa kuchapishwa na gazeti la Washington Post kuwa Obama na Beyonce wana uhusiano usiofaa, na akaongeza "Dunia nzima italiongelea hili sana" 

Lakini msemaji wa gazeti hilo Wasington Post Bw Kriss Coratti alipoulizwa juu ya habari hiyo akasema hana habari yeyote juu ya hilo ila akaongeza Rais Obama na mkewe wamekuwa na matatizo hivi karibuni, "Lakini sijui zaidi ya hapo"

Baada ya yote hayo Paschal Rostain sasa ameeleza kuwa hajawahi kusema kitu chochote ya Rais Obama na mkewe.

Beyonce  kupitia msemaji wake alikanusha madai hayo na kusema "Ni kichekesho". Hata hivyo inafahamika kuwa familia ya Obama ni rafiki na familia ya Beyonce Knowles ambapo Beyonce aliimba siku ya kuapishwa Barack Obama na vile vile aliimba katika maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Michelle Obama kutimiza miaka 50.
Ahsante sana kwa wimbo mzuri. Obama akimshukuru Beyonce siku ya kuapishwa kwake.
Siku ya kuapishwa Obama
Happily married; Beyonce na mumewe Jay-Z