08/23/15

Jumuiya ya marafiki wa Kinondoni yapata uongozi wa muda

Toka kushoto waliosimama ni Abdul Kazembe (mjumbe) Mahmoud Kamusi(Mjumbe)Adam Tuga Bush (mjumbe)
Toka kushoto waliokaa Florah Samuel (mweka hazina msaidizi) Suzane Bagilla (katibu mkuu) Yahya Poli (Mwenyekiti) Mkala Fundikira (makamu wa mwenyekiti) na Jully Kitundu (mjumbe)
Jumuiya ya marafiki wa Kinondoni (Kinondoni Group) jana ilifankiwa kufanya mkutano wa kujadili na kuipitisha rasimu ya katiba na kuteua viongozi wa muda ambao walipewa jukumu la kuhakkisha jumuiya inapata usajili katika kipindi cha mwezi mmoja. 

Kikao hicho kilichoendeshwa na mwenyekiti wa kikao Bw Yahaya Poli kilikuwa na ajenda mbili 

1. Kuijadili na kuipitisha rasimu ya katiba ya jumuiya hiyo.
2. Kuteua viongozi wa na kamati tendaji ya muda.

Mkutano huo ulifanikiwa kuijadili na kuipitisha katiba hiyo pia mkutano uliwateua Bw Yahaya Poli kuwa mwenyekiti, Mkala Fundikira kuwa makamu wa mwenyekiti, Suzzane Bagila kuwa katib mkuu, Bw Ivan Minja kuwa katibu msaidizi na Ismail Kagambo kuwa mhazini mkuu akisaidiwa na Anna Samuel, vile wanajumuiya wanne waliteuliwa kuwa wajumbe wa kamati ya utendaji ambao ni Abdul Kazembe, Jully Kitundu, Adam Bush na Mahmoud Kamusi. Hawa wanaungana na uongozi na kuwa 10 wanaunda kamati ya utendaji itakayokuwa chini ya Mwenyekiti Yahaya Poli. Dhumuni la kuanzisha jumuiya hiyo ni kujiunga pamoja na kusaidiana na kuwekeza katika fursa mbali mbali zitakazojitokeza

Akizungumzia uteuzi wake Bw Poli alisema"Napenda niwashukuru wajumbe wote wa mkutano huu kwa kuniamini na kunipa fursa ya kuiongoza jumuiya ya Kinondoni, naahidi kuitendea haki fursa hii na kuiongoza jumuiya kuelekea maendeleo ya ki uchumi na kijamii. Na naahidi kujitoa kwa hali na mali ili kuona tunapiga hatua za ki maendeleo siku hadi siku. Vile niwashukuru waratibu wetu Bw Ivan Minja na Bw Mkala Fundikira kwa kutukutanisha hapa leo, nitawaomba waendelee na moyo huo huo na jumuiya itafika mbali ki maendeleo.Alimaliza.

Jumuiya hiyo ina wanachama zaidi 2300 katika mtandao wa Facebook inakojulikana kama Kinondoni Group, ambapo iliasisiwa na Bw Ivan Minja huku Bw Mkala Fundikira akiendesha kundi la Telegram kupitia simu za mkononi. Makamu mwenekiti wa jumuiya hiyo alisema kamati tendaji imepewa kazi ya kuhakikisha jumuiya inasajiliwa ili wanachama wengi zaidi wa Kinondoni Group katika mtandao wa kijamii wa Facebook waweze pia kupata fursa ya kujiunga na jumuiya yao ya marafiki wa Kinondoni na wafaidike na matunda yote yatakayotokana na kuwa mwanajumuiya hai. Kikao hicho kilichofanyika Mamaz Tavern(Mamaz pub zamani) kilihudhuriwa na wanajumuiya 16 huku wengine wengi wakitoa udhuru kadhaa.
Mwenyekiti mteule Yahaya Poli akisisitiza jambo katika mkutano wa jana.
Makamu wa mwenyekiti (katikati) Mkala Fundikira na katibu Suzzy Bagilla (kulia) wakimsikiliza mwenyekiti.

Toka kushoto ni Fatyy Dula, Dada Rukia, Emmy Stephen, Dada Mariam, Ivan Minja na Kaka Poli

Toka kushoto ni Adam Bush, Florah Samuel, Mahmoud Kamusi na Abdul Kazembe.


Mudrikati Swedi kulia na suzzy Bagila.

Dax kushoto na Issa Mndeme wakifuatilia kikao.
Makofi kidogo.
Dada Jully Kitundu na Adam Bush.
Rukia Mussa na Emmy Stephen.
Picha ya pamoja





Picha na Camilius Kamili wa mkalamatukio blog