04/15/15

Kamati ya imetosha yatuma ujumbe mzito kanda ya ziwa!


Balozi Henry Mdimu akiongea na vyombo vya habari
Taasisi isiyo ya ki serikali ya Imetosha Foundation inayopinga unyanyapaa, ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino kwa njia ya elimu, inatarajia kutuma ujumbe mzito kanda ya ziwa hapo kesho kwa maandalizi ya ujio wa timu nzima ya taasisi hiyo iliyojikita kwenye kubadilisha mtazamo (mind set) wa watu juu ya janga hili. Ujumbe huo utaongozwa na mwenyekiti wa taasisi hiyo Bw Masoud Kipanya, Balozi Henry Mdimu Mgaya na katibu Salome Gregory,wajumbe watakaongozana na viongozi hao ni pamoja na Mkala Fundikira, Isaya Mwakilasa (wakuvwanga aka Baba Andunje) Zaytun Biboze, Kelvina John na msanii wa muziki wa reggae Jhikoman Manyika.

Mwenyekiti Masoud Kipanya akiongea katika kilele cha matembezi ya hamasa yaliyofanyika jijini Dar
Dhumuni la safari hiyo itakayoupeleka ujumbe huo mpaka mkoani Shinyanga ni kwenda kujitambulisha kwa viongozi wa serikali na usalama wa mikoa na za kanda hiyo iliyoathiriwa sana na janga la ukatili na mauaji ya watu wenye ualbino. Taasisi ya Imetosha imepanga kwenda kanda ya ziwa baadaye mwezi ujao ambapo timu itaenda maeneo yaliyoathiriwa na kutoa elimu kwa wakazi wa maeneo hayo kuwa si kweli kwamba ukiwa na kiungo cha mtu mwenye ualbino utapata mafanikio, elimu hizo zitatolewa kwa njia ya filamu mbali mbali, michezo ya kuigiza na matamasha ya muziki.
Hoteli ya Green Palm utakapofikia ujumbe wa Imetosha Foundation jijini Mwanza aka the Rock City.
Ujumbe huu ukiwa mjini Mwanza utakuwa chini ya udhamini wa hoteli ya Green Palm iliypo maeneo ya Bwiru, vile vile kampuni ya Mwananchi communication ltd (MCL) inayozalisha gazeti bora la Mwananchi na mengineyo itachapisha habari zote kuhusiana na msafara huo wa Imetosha kanda ya ziwa. Meneja wa hotel 

Isaya Mwakilasa wa (Orijino komedi) Henry Mdimu na familia ya Isaya aka Wakuvwanga
ya Green Palm Bw Juma Herman ameuambia mtandao huu kuwa "imekuwa rahisi kwetu (Green Palm Hotel) kudhamini makazi na usafiri kwa taasisi hiyo kwa kuwa inachofanya ni kitu chema basi nasi tumeona ni vema tuwatie nguvu kwa kuwapatia malazi na usafiri wa ndani kwa kipindi chote watakachokuwa jijini Mwanza, kwa kweli sasa imetosha ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino" aliongeza.
Wakiongea na mtandao huu kwa nyakati tofauti Mwenyekiti Masoud Kipanya na Balozi Henry Mdimu walisema  wanashukuru sana kwa kitendo cha Green Palm na Mwananchi communictaion na kuwa ni vya kuigwa na makampuni mengine ili kuiwezesha taasisi hiyo kufikia malengo yake. Taasisi ya Imetosha haina vyanzo vya fedha hivyo kutegemea wahisani kama Green Palm Hotel na Mwananchi communication.
Maktaba Baadhi ya wajumbe wa Imetosha wakijiandaa kwenda katika mchezo wa Simba na Yanga