09/10/13

Wachezaji nguli wa soka wahoji kutochezeshwa Carrick jana

Michael Carrick Pass master!
Wachezaji nguli wa soka wa zamani wakiongozwa na Gary Linneker jana walihoji ni vipi mcheza wa daraja la juu kiungo wa Man United hakupangwa katika mechi ya Ukrayne dhidi ya England pamoja na England kuonesha wazi kushindwa kumiliki mpira kwa vipindi virefu katika mchezo huo, Linneker ambaye alipata kuzichezea Fc Barcelona ya Spain na Totenham Hotspurs ya jijini London aliandika kupitia ukurasa wake wa Twitter kama hivi
Kana kwamba haikutosha Lineker kushangazwa naye Dietmar Hamman aliyekuwa kiungo wa Liverpool na Man City
  kupitia mtandao huo huo naye ali tweet
Hamann naye alishangazwa na kukosekana Carrick katika kikosi cha England jana, katika hali ya kushangaza zaidi hata Roy Hodgson alipoamua kumpumzisha Jack Wilshere na kuamua kumuingiza Ashley Young ambaye si kiungop wa kati wakati Carrick alikuwepo benchini na England ilimuhitaji kwa kushindwa kumiliki mpira. Hata hivyo England ilifanikiwa kutoka sare na hivyo kuendelea kuongoza kundi H kwa pointi 16.

Kula panya na zabibu kavu kwamnusuru kifo baada ya kukaa njaa miezi minne!

Raul Fernando Gomez (58) aliyepotea kwa miezi minne akiwa katika safari ya kutembea kwa miguu katika milima huko nchini Uruguay Amerika ya kusini akitokea nchini Chile aliokolewa jumapili na kundi la wa Argentina waliofika katika eneo hilo la milima wakifanya utafiti juu barafu (snow). Huku akiwa amepungua karibu kilo 3, na kupoteza virutubishi mwilini katika sakata hilo,madaktari wamesema atarudi katika hali yake ya kawaida baada muda mfupi?
Gomez akionesha jinsi alivyokonda
Gomez ambaye alisafiri kutoka Chile kwenda Argentina mnamo mwezi Mei kwa pikipiki kwa bahati mbaya pikipiki hiyo iliharibika njiani na hivyo kulazimika kutembea kwa miguu ambapo alipotea njia baada ya kimbunga kutokea. Maafisa toka jimbo la kaskazini magharibi mwa Argentina walimkuta akiwa katika kibanda kilichopo futi elfu 9318 kutoka usawa wa bahari, Gomez akiwa dhoofu wa hali alifanikiwa kutembea kwa taabu ambapo alifungua mlango wa kibanda hicho ndipo maafisa hao waliokuwa wakipita eneo hilo wakamuona. 

Akibebwa baada ya kuokolewa


Gavana wa San Juan aliliambia gazeti la Diario de cuyo "Huu ni muujiza, bado hatuamini kilichotokea, Tulimpatia simu akaongea na familia yake, pia nilimuuliza wewe ni mwenye kuamini? akajibu " sikuwa lakni sasa ni mwenye kuamini! Kwa muda wote huo Gomez alikuwa akila zabibu zilizokauka, sukari na panya. Madaktari wameeleza kuwa Gomez anatibiwa shinikizo la damu na ukosefu mkubwa wa virutubisho na maji mwilini.
Akipakiwa katika machela ili apelekwe hospitali

Matibabu; Akiwa amelazwa hospitali mjni San Juan.


Habari kwa hisani ya Dailymail, picha kwa hisani ya AP na Reuters.