02/20/15

Msanii Moses Bushagama aka Mez B afariki dunia leo!

Mez B enzi za uhai wake!
Msanii Moses Bushagama aka Mez B aliyewahi kung’ara na ngoma ya kikuku cha mama Roda ambayo mimi Mkala Fundikira nilimfanyia video yake katika miaka ya 2000 katika studio za Royal Productions, pamoja na nyimbo zingine nyingi amefariki dunia leo mjini Dodoma ambako mama yake huishi baada ya kuugua kifua kikuu(TB). Binafsi nimeshtushwa na kifo chake hasa baada ya kupata habari za kifo chake bila kufahamu kama alikuwa akiugua kwa muda.Mez alikuwa na kipaji cha aina yake na sauti laini, tutamkumbuika daima.
                           Mungu ilaze pema roho yake!
Picha kwa hisani ya Dj Choka