02/25/14

Mama Agnes Matle Ngula afariki leo asubuhi!

Bibi Agnes Matle Ngula enzi za uhai wake
Aliyekuwa naibu waziri wa fedha  Bw Venance Ngula leo hii asubuhi amempoteza mkewe Bibi Agnes Matle Ngula ambaye alikuwa akiugua kwa muda sasa. Mtoto wa kwanza wa marehemu Wali Francis Ngula anayeishi New Jearsey America anatarajia kuwasili jijini Dar kwa mazishi ya mama yake mpendwa siku ya Alhamisi. Tutaendelea kujuzana mipango ya mazishi hpa na kwingine. Mungu ailaze pema peponi roho ya mama yetu mpendwa Mama Agnes Ngula.
AMEN!
Bw na Bibi Venance Ngula wakiteta jambo enzi za uhai wa Bibi Agnes Matle Ngula
Mama Ngula akibandikwa mabusu na mwanae Wali Francis Ngula na mkewe Enika Kombe Ngula muda mfupi baada ya harusi yao mwaka juzi .
Mtoto wa mwisho wa mama Agnes, Nancy Ngula akiwa na marehemu 
Bibi Agnes Matle Ngula enzi za ujana wake.
Francis Wali Ngula
Habari na picha kwa hisani ya Francis na Nancy Ngula