05/04/13

Ilikuwa balaaaa!

Keyboy na Dj maarufu Ommy Composer
 Siku ya Alhamisi tarehe ya tarehe 2/04/2013 bendi maarufu ya Mapacha Watatu ilitumbuiza mjini Tabora katika ukumbi wa Frankman Palace ambapo mambo mengi yalijiri ikiwemo vituko hebu jionee mwenyewe!
Kanyaga twende!
Meneja wa bendi Hamis Dakota akijimwaga na mmoja wa washabiki waliohudhuria onesho hilo
Mwango aka Benny Ngwasuma akiserebuka na Mariam Zidane
Hamis Dakota, tena akijiachia na mdada mwenye makeke mengi!
Sichezi na shemeji: Jose Mara aligoma kucheza na mwanadada ambaye ilidaiwa ni shemeji yake.
Wadau wakimcheka Jose Mara wa Kimara kwa kugoma kukamatia.

Baunsa Muddy naye alionja raha ya kukamatia,  Duh sijui Muddy alilpata usingizi?
Duh cheki! Juma Kapipi aduwaa!

Mbona hujaniimba Khalid?
Uuuuuuuh! Ngoma inogile! Mikono juu!
Papaa Biggie na Mariam Zidane waki pozi kwa snap!
Uzinduzi wa albam Yarabi nafsi!

Mapacha watatu wazindua albam Tabora!


UZINDUZI; Chokoraa kushoto na Jose Mara wakizindua album mpya katika ukumbi wa Frankman, Tabora.
Bendi ya Mapacha watatu usiku wa alhamisi katika ukumbi wa Frankman Place mijini Tabora, walizindua album yao mpya iendayo kwa jina la Yarabi nafsi yenye nyimbo nane ambamo kuna watunzi kadhaa akiwemo Jose Mara, Khalid Chokoraa na nyota wengine wakali wanounda bendi hiyo pia wametunga nyimbo kadhaa. Katika hali ya kujutia pengine Bendi hiyo iliwasili Tabora ikiwa na cd chache za albam hiyo mpya ambazo ziliisha bila wao kutegemea

Mdau wa mapacha watatu!