08/27/15

Hatimaye baba wa Gary na Phil Neville azikwa kijijini kwao Bury!


Gary na Phil Neville wakiwa wamebeba jeneza la baba yao pichani chini!
Neville Neville (65) alifariki  wikinchini Australia kwa shambulizi la moyo.
 Baba wa wachezaji malejendari wa kilabu cha Manchester United Gary na Phil Neville, Neville Neville (65) alifariki kwa shambulizi la moyo mapema mwezi huu huko Australia ambako alikuwa na binti yake Tracey Neville katika mashindano ya Kombe la dunia ya mpira wa pete binti huyo ambaye ni kocha wa timu ya taifa ya netball ya Uingereza.

David Beckham ambaye alicheza mpira na ndugu hao wawili alikuwa ni mmoja wa watu mashuhuri waliohudhuria mazishi hayo, wengine ni Sir Alex Ferguson, Dennis Law, Sam Alardyce, Steve Bruce, Ryan Giggs, Nicky But, Paul Scholes, Bryan Robson, Sandra Beckham(mama wa David Becham) Phil Jagielka(Kapteni wa Everton)

Kundi dogo la watu walikusanyka nje ya kanisa la parish mjini Bury kutoa heshima zao za mwisho kwa Neville Neville. Nevile Neville (65) alizikwa jana kijijni kwake Bury nje kidgo ya jiji la Manchester.
Steve Bruce kocha wa Hull city akiwasili kanisani
Meneja msaidizi wa Man united Ryan Giggs akiwasili na mkewe.
Paul Scholes na mkewe.
Meneja wa zamani wa West Ham United Sam Alardyce
David Beckham na mama yake Sandra.
Ryan Giggs, Nicky Butt na Steve Bruce wakijadili jambo.
Gary Neville akiwaliwaza mama na dada yake baada ya mazishi.
Tracy Neville akilia baada ya kumzika baba yao Neville Neville.
Malejendari wa Man united kushoto Sir Alex na Dennis Law


Phil Jagielka wa Everton.


Kanisa la Parish kijini Bury
Habari na picha kwa hisani ya themirronline