mkalamatukio: Michezo
Showing posts with label Michezo. Show all posts

Bilionea Dangote bado anataka kuinunua Arsenal!

Uwanja wa the Emirate London ya kaskazini
Bilionea mNigeria mfanyabiashara wa saruji Bw Aliko Dangote ameeleza nia yake ya kuinunua klabu ya Arsenal ya England. Dangote ambaye ndiye mtu tajiri kuliko wote katika bara la Afrika ambaye ana utajiri wa dola za kimarekani bilioni 15 aliuambia mtandao wa bloomberg kuwa "Naweza kuinunua Arsenal lakini si kwa bei ya kiwazimu ila kwa bei ambayo wamiliki watashawishika kuniuzia"

Dangote ambaye ana pesa nyingi kuliko mmiliki wa sasa wa Arsenal Stan Kroenker mwenye 67% ya hisa na mwanahisa mwingine Mrusi Alisher Usmanov.
Aliko Dangote(58) bilionea m Nigeria, mwenye mapenzi na Arsenal Football club ya jijini London, England.

Lakini Dangote alibainisha kuwa mpango wa kununua kilabu hicho maarufu kama the gunners haupo hivi karibuni, alisema "Tunawekeza kiasi cha dola bilioni 16 katika miradi tofauti miaka michache ijayo, kwani nataka kupeleka biashara zangu katika kiwango fulani, na nikimaliza hilo ndipo ofa ya kuinunua Arsenal itafuata" Pia Dangote amepata kukaririwa akisema kocha Arsene Wenger anatakiwa kubadili mfumo wa timu yake. Arsenal imekuwa na sifa ya kutandaza soka safi na la kuvutia lakini wameshindwa kushinda ubingwa wa England kwa karibu miaka 11 na kabla ya mwaka jana ambapo walishinda kombe la FA walikuwa hawajashinda kikombe chochote kwa miaka 9.

Mwanahisa mkuu wa Kilabu hicho Bw Stan Kroenker amenunua hisa zaidi hivi karibuni na haielekei ana mpango wa kukiuza kilabu hicho katika miaka ya karibuni.

Dangote pia anajenga kiwanda cha saruji mjini Mtwara ambapo wakazi wengi wa mkoa huo watapata ajira za muda na za kudumu.
Stan Kroenker (67) bilionea Mmarekani ndiye mbia mwenye hisa kubwa katika kilabu cha Arsenal kwa sasa
Kocha Wenger amatakiwa kubadili mfumo wa timu yake na Dangote
source Mirroronline

MASHINDANO YA LUCY OWENYA CUP YAZINDULIWA JIMBO LA MOSHI VIJIJINI.


Mbunge wa viti Maalumumkoa wa Kilimanjaro,Lucy Owenya akiwasili katika uwanja wa michezo wa shule ya sekondari Singhiti kwa ajili ya ufunguzi wa mashindano ya Lucy Owenya Cup 2015 yanayofanyika katika jimbo la Moshi vijijini na kushirikisha kata 16 za jimbo hilo.
Baadhi ya wananchi waliohudhulia ufunguzi wa mashindano ya Lucy Owenya Cup 2015.
Mbunge Owenya akicheza ngoma katika shrehe za ufunguzi wa mashindano ya Lucy Owenya Cup.
Baadhi ya timu zinazoshiriki mashindano hayo zikiwakatika uwanja wa shule ya sekondari Singhiti kwa ajili ya uunguzi wa mashindano ya Lucy Owenya Cup 2015.
Mratibu wa mashindano hayo,Charles Mchau akizungumza jambo katika ufunguzi wa mashindano hayo.
Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Kilimanjaro, Lucy Owenya akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Lucy Owenya Cup 2015 ,Mashindano yaliyoanza katika jimbo la Moshi vijijini yakishirikisha kata za Jimbo hilo.
Mbunge wa Viti Maalum Lucy Owenya akisalimianana mwamuzi Batista Mihafu wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo.
Mbunge wa Viti maalumu ,Lucy Owenya akikagua baadhi ya timu zinazpshiriki mashindano hayo .
Mbunge Lucy Owenya akipiga mpira kuashiria ufunguzi rasmi wa mashindano ya Lucy Owenya Cup.
Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Kilimanjaro ,Lucy Owenya akisalimiana na mmoja wa wachezaji wanaoshiriki mashindano ya Lucy Owenya Cup 2015 yaliyozinduliwa juzi katika jimbo la Moshi vijijini na kushirikisha timu kutoka kata 16 za jimbo hilo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

WATANZANIA WAFANYA VIZURI MBIO ZA NGORONGORO MARATHONI 2015


Waziri mkuu Mstaafu , Fredrick Sumaye akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine mbalimbali wakiwemo waandaji buda mfupi kabla ya kuanza kwa mbio za Km 21 Katika gate la kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro,
Waziri mkuu Msaatfu Fredirick Sumaye akikimbia sambamba na rais wa shirikisho la riadha Tanzania,RT,Athony Mtaka(Kushoto kwake) mkuu wa mkoa wa Arusha ,Daud Ntibenda,pamoja na mkuu wa wilaya ya Karatau Omary Kwaang kuashiria kuanza kwa mbio za Ngorongoro Marathoni.
Maratibu wa Mbio , Meta Paul akiwa na mmoja wa wasiamamizi ,Leila wakati wakiwaandaa wanariadha kuanza mbio za Km 21 katika lango la kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro.
Mbio zikianza rasmi.
Baaadhi ya washiriki katika mbio hizo ,walikuwemo pia wadhamini kama Maremga Investment,hapa Marenga mwenye truck suit nyeusi akijaribu kukimbiza upepo.
Awawli mbio zikiwa bado ndio zimeanza kundi la wakimbiaji lilionekana wote wanakimbia kwa karibu.
Muda ulivyosonga na hatua ndivyo zilivyo ongezeka.
Hatimaye wakaanza kuachana mmoja baada ya mmoja,
Wengine wakaamua kwenda pamoja ili kupeana moja.
wengine wakafunguka zaidi.
Hatimaye wakapatikana wakimbiaji watatu wakaongoza hadi mwisho wa mbio na hawa ni ,Joseph Theofily(katikati),George Gerald (kulia) na Emanuel Giniki.
Mkimbiaji raia wa Kenya ambaye jina lake halikufahamika mara moja akijaribu kuonesha umahiri wake katika mbio hizo.
Msichana pekee aliyekuwa akiongoza ni Failuna Abdi .
Nyuma ya Failuna alikuwepo Nathalia Elisante.
Mshindi wa kwanza katika Mbio za Ngorongoro Maratahoni 2015 ,Joseph Theofily akimaliza mbio hizo katika uwanja wa Mazingira Bora akitumia muda wa 1:03:09.
Mshindi wa Pili katika mbio hizo ,George Gerald akihitimisha mbio hizo akitumia muda wa 1:03:36
Mshindi wa tatu ,Emanuel Giniki akikalimilisha mbio kwa muda wa 1:03:42.
Giniki akijaribu kupoza koo mara baada ya kumaliza mbio.
Mkimbiaji wa klabu ya riadha ya Holili,Osward Moris akihitimisha mbio.
Mshindi wa kwanza kwa kina dada Failuna Abdi akihitimisha mbio katika nafasi ya kwanza baada ya kutumia muda wa 1 :10:25
Mgeni rasmi katika mbio hizo ,Waziri mkuu Mstaafu ,Fredirck Sumaye akiingia uwanjani huku akihitimisha mbio za km 21 .

WANARIADHA wa Tanzania Joseph Theofily wa klabu ya riadha ya Holili ya mkoani Kilimanjaro na Failuna Abdi wa klabu ya riadha ya Winning Spirit ya jijini Arusha wamefanikiwa kupeperusha vyema Bendera ya taifa baada ya kuibuka washindi wa kwanza katika mbio za kimataifa za
Ngorongoro Marathoni kwa upande wa wanaume na wanawake.

Mwanariadha Theofily alifanikiwa kumaliza mbio za km 21 akitumia muda wa saa 1:03:09 na kujinyakulia kitita cha sh Mil, 1. mbele ya wakongwe wengine kutoka nchi za Kenya ,Uganda na Malawi huku Gabriely Gerald wa klabu ya Winning Spirit ya jijini Arusha akishika nafasi ya pili akimaliza mbio akitumia saa 1:03:36 na kujinyakulia kitita cha sh laki 5.

Emanuel Giniki alifanikiwa kushika nafasi ya tatu na kujinyakulia zawadi ya sh 250,000,nafasi ya nne ikichukuliwa na Ezekiel Therop huku mwanariadha Mohamed Msenduki wa klabu ya Wining Spirit ya jijini Arusha akimaliza nafasi ya tano.

Mwanariadha wa kike Failuna aliyerejea hivi karibuni kutoka nchini Brazil kushiriki mashindano ya mbio za Km 15 ambazo alifanikiwa kumaliza mbio hizo katika nafasi ya saba,aliwaongoza wakongwe kama Banuelia Bryton ,Marry Naali Jackline sakilu na Catherine Range akimaliza mbio katika nafasi ya kwanza kwa kutumia muda wa saa
1:10:25.

Failuna aliyejinyakulia zawadi ya kitita cha kiasi cha sh Mil,1. alifuatiwa kwa karibu na mpinzani wake Nathalia Elisante aliyetumia muda wa 1:14:40 na kuzawadiwa kitita cha sh 500,000 huku nafasi ya tatu  ikichukuliwa na Magdalena Crispine aliyetumia muda wa 1:15:56, nafasi ya nne na tano ikienda kwa Anjelina Tsere na Merry Naali.

Mbio za kimataifa Ngorongoro Marathoni zinafanyika zikiwa na lengo la kuwawezesha watoto wa jamii ya kimasai kupata elimu ikiwemo kumalizia shule ya Endulen iliyoko Ngorongoro na kutangaza urithi wa utalii kupitia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro huku ikishirikisha pia mbio za Kilomita tano kwa wafanyakazi wa taasisi mbalimbali pamoja na  Km 2.5 kwa wanafunzi.


Kwa picha zaidi ingia hapa,

www.dixonbusagaga.blogspot.com

Homa ya mchezo kati ya Coastal union na Simba sports club yapamba moto!

Wakazi wa jiji la Tanga, viunga vya vyake na mikoa ya jirani leo hii watapata burudani inayotarajiwa kuwa ya kupendeza leo hii jioni mnamo saa 10.15 za jioni wakati Wekundu wa Msimbazi Simba SC itakapoingia katika stadia ya Mkwakwani kucheza mchezo wa Vodacom Premier league 2014/15 dhidi ya Coastal union ya jijini hapa kuwania pointi 3  muhimu hasa kwa Simba ambayo imekua ikifanya vibaya msimu huu na kupelekea hofu kwa washabiki wake kuwa uenda ikateremka daraja. Mpambano huo bila shaka utaoneshwa LIVE na kituo cha Televisheni cha AZAM ambacho mitambo yake imeonekana mje ya uwanja wa Mkwakwani, kama ionekanavyo hapo chini.
OB Van ya Azam Tv ikiwa tayai kurusha matangazo ya moja kwa moja toka Mkwakwani stadium.
Sare za Simba SC zikiwa zimeanikwa kwa mauzo nje ya uwanja wa Mkwakwani
Mshabiki wa Simba kushoto akijadili bei ya fulana ya timu hiyo ya jijini Dar es Salaam karibu na uwanja wa Mkwakwani.
Picha na habari keronyingi blog

Roy Keane amshambulia vikali Ferguson!

Nyakati za furaha:Sir Alex na nahodha wa zamani wa Man united Roy Keane wakibeba juu moja ya makombe ya EPL waliyoyashinda pamoja
Katika hali isiyoshangaza wengi Roy Keane amemshambulia kocha wake wa zamani Sir Alex Ferguson kuwa anapenda nguvu na utawala hata sasa ingawa si meneja tena wa Man united. Keane anayefahamika vema kwa utata wake ndani na nje ya uwanja amefikia kusema kuwa Brian Clough ndiye kocha bora aliyewahi kufundishwa naye na si Sir Alex kocha mwenye rekodi bora kuliko yeyote katika historia ya ligi ya Uingereza na ambaye yeye Keane aliwezeshwa kushinda mataji 7 ya premier league, makombe manne ya FA, kombe moja la ulaya na kombe 1 la klabu bingwa ya dunia na ngao za hisani zisizohesabika. Lakini Keane ambaye Alex Ferguson amemuelezea kuwa ni mwenye ulimi mchafu kuliko kingine chochote na kuwa anaweza kumfanya mtu mwenye kujiamini sana kunyong'onyea na kuwa kama mtoto mdogo asiyeweza kujitetea kwa kutumia ulimi wake mchafu(maneno) bado anaumizwa na kitendo cha Ferguson kumtimua Old Trafford baada ya yeye Keane kuwasema vibaya wachezaji wadogo wakiwemo Rio Ferdinand, Darren Fletcher kuwa hawapaswi kuichezea Man United alisema maneno hayo baada ya Man united kufungwa bao 4-1 Mwaka 2005 dhidi ya Middlesborough. Ndipo Ferguson akaamua kumfukuza Roy Keane pamoja na kuwa Fergie alihakikisha Roy Keane analipwa mshahara wake wote uliobaki na pia Roy Keane akapewa mechi ya Testimonial amabzo hupewa mchezaji aliyecheza timu moja kwa muda usiopungua miaka 10. Roy Keane aliichezea Man united kwa miaka 12 na nusu.
Alex Ferguson, ameelezwa na Roy Keane kuwa ni mwenye kupenda nguvu na kutawala.
Habari na picha kwa hisani mirroronline