03/26/14

Semina ya mawakala wa Redds Miss Tanzania yafanyika

Mkurugenzi wa Lino International inayoratibu shindano la Miss Tanzania Bw Hashim Lungenga akisisitiza jambo alipokuwa akifungua semina ya mawakala wa Miss Tanzania 2014.
Semina ya kuwafunda mawakala wa Redds Miss Tanzania 2014 ilifanyika kuanzia jana arehe 25/03/2014 katika Hoteli ya Regency ya jijini Dar es Salaam, semina hiyo ambayo hukutanisha kamati ya Miss Tanzania, mawakala na wadhamini hufanyika kila mwaka baada ya uzinduzi rasmi wa shindano hilo kubwa la urembo nchini. Kampuni ya TBL kupitia kinywaji chake baridi cha Redds Premium cold ndiye mdhamini mkuu wa shindano hilo ambalo mchakato wake huanzia katika vituo, wilaya, mkoa na hatimaye na shindano la Taifa yaani Redds Miss Tanzania
Kutoka kushoto ni katibu wa Miss Tanzania Bw Bosco Majaliwa, Mshauri wa ufundi Bw Ramesh Patel, Hashim Lundenga, Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa na mshindi wa pili wa shindano hilo.


Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa

Kutoka kushoto Bw Bosco Majaliwa, Ramesh Patel na Bw Hashim Lundenga
Wakala wa kituo cha Dar na Awetu wa gazeti la KIU

Baadhi ya mawakala wa Miss Higher Learning

Muandaaji wa Redds Miss Njombe, Miss Sylvia

Kutoka kushoto ni Miss Jacky, Tom Chilala wa star T na Khadija kalili wa Tanzania Daima