July 2013

Utamliliaje mtu leo, kesho umtukane?

OMMY Dimpoz akilia jukwaani baada ya kulemewa na majonzi ya kifo cha Ngwair tarehe 31/05/2013 Tabora.
Siku chache baada ya kifo cha Albert Mangwea (Ngwair) kulitokea  sintofahamu baada ya msanii Ommy Dimpoz kushutumiwa na gazeti moja la kidaku kuwa alimtukana Ngwair kuwa kafa masikini (kibwege) alipokuwa akipokea tunzo yake pale Milimani city katika kilele cha Kilimanjaro Music Awards. Ninachokumbuka alisema "Sisi wasanii wa Tanzania tumechoka kufa masikini huku tukiwa na majina makubwa" na akatoa wito kwa makampuni makubwa yawape kipaumbele wasanii wa Tanzania katika suala zima la promosheni za bidhaa zao kitu ambacho kitainua kipato cha wasanii wa Tanzania badala ya kutumia wacheza mpira wa nje kama Lionel Messi. Hali ilikuwa mbaya sana kwa Ommy Dimpoz huku akilaaniwa na kusiwa huku na kule na hasa katika mitandao ya kijamii. Kabla ya Kili Music Awards huko Tabora katika kilele cha Redds Miss Tabora 2013 Ommy alitoa kauli hiyo mbele ya Mh William Ngeleja na alimuomba awasaidie kupeleka kilio chao(wasanii) bungeni ili ziunde sheria nzuri zenye kulinda maslahi ya wasanii!


Totenham wawastaajabisha Real Madrid kwa dau la kumuuza Gareth Bale!

Gazeti la michezo lenye ukaribu na kilabu cha Real Madrid leo hii limedai kuwa Mwenyekiti wa Totenham Hotspurs ya jijini London, Uingereza Bw Daniel Levy amewapa bei ya kumnunua mshambuliaji Gareth Bale kuwa ni Euro145 Milioni au kwa maneno mengine ni Pauni 125 Milioni ya Malkia wa Uingereza. Bei hiyo imewastua sana Madrid kwani hawakutegemea kabisa Bw Levy anaefahamika vema kutoa bei zisizoendana na uhalisia ambapo awali aliwasumbua sana Man United kuwanunua Michael Carrick na Dimitar Bernatov. Bei hiyo pia imelistua sana gazeti la Marca ambalo limetoa kichwa cha habari UNA LOCURA ikiwa na maana Crazy au "wazimu"



Wakati huo huo ripoti toka Spain katika gazeti la Marca zimeeleza kuwa Daniel Levy ameshapokea ofa ya Pauni 85 milioni toka klabu ya PSG ya ufaransa inayomilikiwa na matajiri wa kiarabu. Pia taarifa hiyo ilisema katika ofa zote Muhimu ni ile iliyotolewa na klabu ya Manchester United ya England ingawa chanzo hicho hakikueleza ni kiasi gani Man United wameofa kwa klabu hiyo yenye makazi yake kaskazini mwa jiji la London.