July 2015

Tabora Wanufaika na Mafunzo ya ULINGO – Tanzania Women Crossparty Platform (TWCP)

ULINGO WA WANAWAKE WANASIASA – Tanzania Women Crossparty Platform (TWCP) ni shirika lisilo la kiserikali lililoendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo watia nia wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu katika nyadhifa mbalimbali za uongozi wa nchi ikiwa ni kuchangia kutoa elimu inayolenga kuleta usawa kama haki msingi ya Mtanzania. Mafunzo hayo yamedhaminiwa na UNWomen.

Mafunzo hayo yamewanufaisha walengwa husika kwa kujipatia elimu hiyo huku wawezeshaji wakiwa ni Hilda Stuart Dadu na Emmiliana Msaguka waliohakikisha wanawafikia watiania katika mkoa wa Tabora na kuendesha mafunzo hayo pale Student Center.
t-wcp (2)
Wanufaika na watia nia za kugombea nafasi mbalimbali na wa vyama tofauti tofauti wakifuatila mafunzo hayo yaliyotolewa na Hilda Stuart Dadu kutoma TWCP
t-wcp (3)
Watia nia wakichukua kumbukumbu za mafunzo hayo mapema leo hii
t-wcp (4)
Miongoni mwa wanufaika wa mafunzo hayo akifuatilia jambo kwa umakini.
t-wcp (5)
Wakti mafunzo yakiendelea na maswali yakiulizwa kwa ufafanuzi zaidi kutoka kwa wawezeshaji.
t-wcp (6)
Hilda Stuart Dadu wa ULINGO (aliyesimama) akisisitiza jambo wakati mafunzo yakiendelea.
t-wcp (1)
t-wcp (7)

t-wcp (8)
Hawa, mgombea wa ubunge wa viti maalumu kwa tiket ya chadema akiuliza swali kwa muwezeshaji t-wcp (12)

t-wcp (11)
Muwezeshaji Emmiliana akitoa zoezi kwa wanafunzi wake ili kukazia zaidi kile walichofundishwa na kukifanya kwa vitendo.
t-wcp (13)
Miongoni mwa wanakundi wakijadiliana jambo baada ya kupewa zoezi na muwezeshaji wa mafunzo.
t-wcp (10)

t-wcp (9)
Picha ya pamoja ya wanufaika wa mafunzo ya ULINGO na wawezeshaji wa mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo watia nia za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi. Mafunzo hayo yamekuja wakati huu ambao ndiyo haswa muda mwafaka wa uchaguzi mkuu wa ngazi za udiwani, ubunge na Urais.

Wanaowania kuteuliwa kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM Tabora mjini wajinadi Itetemia!

Mh Aden Rageh kushoto na Bandora Mirambo wakifuatilia mkutano.

Makada wa CCM Wanaowania kuteuliwa kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM Tabora mjini leo hii mchana walijinadi kwa wapiga kura wao wa kata ya Itetemia, ambao wakiungana na wengine kwa jimbo la Tabora mjini watapiga kura siku ya tar 1/8/2015kumchagua mmoja wao ili aikiwakilishe chama hicho kayika uchaguzi mkuu baadae mwaka huu.

Wagombea hao ambao kila mmoja wao alijieleza mbele ya wajumbe hao kwa dakika 5 walitoa maelezo yao mbele ya wajumbe ya kuwa wakichaguliwa wataboresha hali za maisha, uchumi, elimu na kilimo.

Siku ya kesho wagombea hao wataelekea Ntalikwa ambako pia watajinadi kwa wajumbe wa mkutano mkuu maalumu katika kuelekea kura za maoni mapema mwezi ujao.
Bandora Mirambo akibadilishana mawazo na mgombea mwenzie Emmanuel Mwakasaka mara baada ya kujinadi.
Mwenyekiti wa CCM kata ya Itetemia (Kushoto) Rashid Kamanda Tall(kiongozi wa msafara) na katibu wa CCM kata ya Itetemia.




Wajumbe
Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa CCM wilaya ambao watapiga kura tarehe 1/8/2015 kumchagua mgombea wa kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao.
Bw  Bandora Salum Mirambo.
Bw Emmanuel Mwakasaka
Amon Mkoga.
Mh Aden Rageh.
Bw William Masubi Chimaguli.
Ramadhani Mauli Mkangara mgombea akijinadi na kuomba kura kwa wajumbe wa mkutano mkuu maalum.
Viongozi wa mkutano toka kushoto ni Rashid Tall, Ali Kazikupenda na Mohamed Kazete.



Mkaziwa Kipalapala Thomas Mwiniko aliyeuliza baadhi ya maswali kwa wagombea.
Amon Mkoga kushoto na Salum Mkangara wakifuatilia mkutano
 Habari na picha na mkalamatuio blog

Tabora Stand Up; Eid Mosi Wasanii Wafurika Hapatoshi.

Shangwe na burudani za kutosha zinatarajiwa kufanyika katika sikukuu ya Eid hapo kesho mkoani Tabora panapo majaaliwa ya M/Mungu. Mashabiki mbalimbali mjini Tabora watarajiwa kufurahia onesho hilo katika maeneo mawili tofauti ambapo mchana itakuwa Bwalo la Polisi kuanzia saa 8 mchana na Usiku katika viwanja vya Muungano Mesi kuanzia saa 2 usiku.
Wasanii wa kila nyanja wametua mjini hapo na kufanya mahojiano CG Fm Redio leo mchana; wasanii hao ni Kassim Mganga a.k.a tajiri wa mahaba, Ommy Dimpoz, Mkude Simba (Kitale) na rafiki yake Stan Bakora, Young Killer, na Baraka Da Prince.
Eid_Tabora (8)
Kassim Mganga akiwa CG Fm Redio, 89.5 The point of no Return
Eid_Tabora (11)
Ommy Dimpoz
Eid_Tabora (4)
Eid_Tabora (7)
Manoni (Mtangazaji CG Fm Redio 89.5 The Point of no Return) akifanya mahojiano na wasanii.
Eid_Tabora (13)
Mkudesimba Original (Kitale)
Eid_Tabora (14)
Kitale na Stani Bakora, ...eti "Tembo wa Ulaya mkubwa sana kama mbuzi"
Eid_Tabora (17)
Stan Bakora
Eid_Tabora (9)
Baraka Da Prince
Eid_Tabora (16)
Stephania (Mtangazaji CG FM)
Eid_Tabora (15)
Eid_Tabora (12)
Young Killer (Handsome aliyekosa matunzo) akishuka free style.
Eid_Tabora (5)
Mgalula Fundikira (Mkurugenzi wa Royal Nsyepa Entertainment) akizungumzia maandalizi ya onesho hilo aliloliandaa baada ya muda mrefu toka arudi kutoka Hispania
Eid_Tabora (3) Eid_Tabora (2) Eid_Tabora (18)
Kutoka kushoto, Kassim Mganga, Mubenga (Meneja wa Ommy Dimpoz), Stan Bakora na Abdul katika nyumba za Tabora Rest House walikofikia wasanii hao.
Eid_Tabora (19)  
Wakijipima uwezo wa ukali wa "SAUM"
Picha na Aloyson -TBN Kanda ya magharibi

Bandora Mirambo alipochukua fomu ya ubunge wa Tabora mjini mapema leo.



Bandora Salum Mirambo akionesha fomu yake ya ubunge kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi
Mama Hidaya Rashid Amani katibu msaidizi wilaya akimuandikia risiti Bw Bandora.
Bandora Mirambo akitia sahihi katika kitabu cha kuchukulia fomu ya ubunge wa Tabora mjini.

Ada ya fomu!
Maelekezo!
Saidi Zaidi kulia na Juma Mgawe wakifuatilia kwa makaini makabidhiano ya fomu.

Mama Hidaya Rashid Amani akitoa maelekezo ya ujazaji fomu
Bandora akisalimiana na mdau nje ya ofisi za CCM Wilaya.
Apolo (kushoto) akiwa na Bandora Mirambo mara baada ya Bandora kuchukua fomu.
Bandora akipongezwa na kada wa chama baada ya kuchukua fomu ya ubunge kwa jimbo la Tabora mjini.
Bandora Mirambo akiwa na baadhi ya wapiga kura wa jimbo hilo waliomsindikiza kuchukua fomu katika ofisi za CCM  wilaya ya Tabora mjini.