November 2013

Shabiki wa Ajax ajeruhiwa vibaya baada ya kuanguka toka jukwaani

Watoa huduma ya kwanza wakimhudumia shabiki aliyeanguka akishangilia goli la pili.

Mshabiki wa timu ya Ajax Amsterdam ambaye hakutajwa jina, jana alianguka alipokuwa akishangilia bao la  pili la timu yake dhidi ya Fc Barcelona lililofungwa na Danny Hoesen. Inakadiriwa mtu huyo alianguka toka urefu wa futi 16 alikutwa kalala katika dimbwi la damu
Baadae watu wa huduma ya kwanza toka kwa magari mawili ya Ambulance na helikopta moja walimtibu mtu huyo na kumpeleka hospitali. Ajax ilifanikiwa kuifunga Barcelona katika mchezo huo wa Ubingwa wa Ulaya. Lakini haikufahamika hali ya mshabiki aliyeanguka ilikuwa ikiendeleaje.
Amsterdam Arena ionekanavyo kwa nje.


Tabora Funga mwaka Bash kuburudishwa wa na Belle9!

Msanii mkali wa Bongo Flava Belle9 atakuwa ni mmoja wa wasanii watatu watakaoburudisha Tamasha la Club Royal Funga Mwaka Bash litakalofanyika mjini Tabora katika ukumbi maarufu wa New Royal Garden. Akiongelea tamasha hilo mmoja wa wadhamini wa tamasha hilo Mashaka Chura aka Mzee wa maini na Figo mkurugenzi wa Chura Fashion alisema maandalizi yamekamilika, wapenzi wa muziki wa Bongo Flava wanaotarajia kwenda kujiachia Ijumaa hii wajitokeze kwa wingi dukani kwake ambapo kuna pamba mpya na kali za kila aina ili watakapoingia katika tamasha hili la kuuaga mwaka 2013 wawe wametisha. Tamasha hilo pia litashuhudia wasanii Squizer na Ziggy Dee aliyetamba na wimbo wa Eno Mic pia wakitumbuiza ukumbini Royal Garden. Tamasha hili limewajia kwa udhamini wa Serengeti Breweries Ltd, Clouds Media Group, Chura Fashion, Gonala Pharmacy, Millenium Barber shop, Tabora Rest House, Nbs Classic, Mtingoni Company Ltd, Mussoma Batteries, CgFm 89.5, VoT fm 89.0 na Clouds Media Group.

Mama Hawa Haji Kamanga kuzikwa kesho!

Marehemu Bibi Hawa Kamanga 1941-2013
Mama Hawa Kamanga ambaye alifariki leo hii asubuhi mnamo saa 2:40 katika hospitali maalum ya wagonjwa wa Saratani ya Ocean Road ya jijini Dar es Salaam ameacha watoto 6, wa kiume watano na wa kike mmoja. Kati ya hao watatu wanaishi marekani nao ni Haji, Kaela na Hizza. Wengine wawili wa kiume wanaishi Tanzania ambao ni  Zakaria (kaka mkubwa) na Pioka. Na mmoja wa kike  Anna Kange anaishi Holland, Marehemu ameacha wajukuu 11 na kitukuu mmoja. Baada ya wanafamilia kukaa kikao, imeamuliwa kuwa marehemu atazikwa kesho saa 10:00 jioni katika makaburi ya Kisutu na shughuli zote za msiba zipo Sinza Vatican. 

Blog hii imnesikitishwa sana na kifo hiki, mwandishi wa habari hii alipata kumtembelea marehemu alipokuwa amelazwa kwa Dk Mvungi wiki tatu zilizopita. Blog inawapa pole watoto,wajukuu, ndugu, jamaa na marafiki wote wa marehemu!

MUNGU AILAZE ROHO YAKE PEMA PEPONI! AMIN


Chanzo cha habari na picha Hizza Kamanga,Grace Mmari, Houston Texas/ Tausi Khalid Dar, Tanzania.

Bibi afariki saa 48 baada ya kujua wajukuu zake wamefika hospitali kumuona!

Katika hali ya kusikitisha Mama Hawa Haji Kamanga (71) alifariki leo hii saa 2.40 Hospitalini Ocean Road  baada ya kupigania uhai wake kwa siku kadhaa alizokuwa na hali mbaya sana lakini ilielekea alipigana kubaki hai mpaka pale wajukuu zake wawili walipofika toka America siku ya Jumamosi na kwenda moja kwa moja Ocean Rd Hospital kumuona Bibi yao. Wajukuu zake hao Kaela Jr (3)na Hadassah Bianca (1) walipofikishwa wodini Marehemu akaambiwa wajuu zako wamekuja kukuona inasemekana marehemu aliyekuwa na hali mbaya kwa wakati huo alitabasamu na kujaribu kusema kitu lakini hakuweza kutoa sauti, lakini bila shaka alifurahi kujua hatimaye wajukuu zake wamemkuta akiwa hai, na hatimaye akaamua muda ulikuwa sahihi kuacha kupigania uhai wake. Mama Hawa Kamanga ana watoto kadhaa wanaoishi nchini Marekani. Marehemu alilazwa Ocean Road wiki mbili hivi baada ya kuhamishiwa hapo kutokea katika hospitali ya Dk Mvungi ambako alilazwa kwa uchunguzi wa awali. Kwa sasa mipango ya mazishi inafanyika na tutaendelea kufahamishana humu na kwingineko.
    Inna Lillah wa inna illahi Rajiun!

Shabiki wa Arsenal apoteza nyumba baada ya Man United kuishinda Gunners!

Hali mbaya
Robin Van Persie akiwazamisha The Gunners
Shabiki mkereketwa wa timu ya Arsenal (the Gunners) Mganda Henry Dhabasani mkazi wa jijini Kampala alijikuta akipoteza nyumba yake  dhidi Rashid Yiga ambaye aliweka dau la gari ya Toyota Premio na mkewe baada ya kudai Man united ingeifunga Arsenal bila shaka na wazee wa kijadi walikuwepo na kushuhudia dau hilo likipitishwa kwa maandishi kabla ya mchezo huo amabao mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Robin Van Persie alifunga bao pekee la mchezo katika kipindi cha kwanza na kuwasimamisha The Gunners katika mbio zao za kutaka kujikita zaidi katika usukani wa ligi hiyo maarufu na yenye msisimko kuliko zote duniani. Gazeti la Observer la Uganda lilieleza kuwa shabiki huyo Dhabasani mwenye wake watatu na watoto watano alizirahi baaada ya mchezo kwisha. Hata hivyo aliondoshwa katika nyumba yake siku iliyofuata.

[Video] KISOMO CHA MWISHO CHA MAMAA NYAWANA FUNDIKIRA MDA MFUPI KABLA YA MAZISHI

UHARAKA WA MUDA WA KUHAKIKISHA MWILI WA MAREHEMU UNAZIKWA ULIZINGATIWA TU MARA BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUWASILI TABORA MNAMO SAA 12 JIONI. KISOMO CHA MWISHO NA MAOMBI YA MWISHO ILIFANYWA KISHA KUELEKEA KATIKA MAZIKO YA MWILI WA NYAWANA FUNDIKIRA KATIKA MAKABURI YA ITETEMYA AMBAKO IKO IKULU YA MACHIFU WA UKOO WA FUNDIKIRA. 
ILIPOFIKA MUDA WA SAA 1:10 USIKU SHUGHULI YA MAZIKO ILIENDELEA NA KUHAKIKISHA MWILI WA MAREHEMU UMEPUMZISHWA.

*UMATI MKUBWA WA WATU ULITANDA PEMBEZONI MWA BARABARA WAKISHUHUDIA MSAFARA WA KUELEKEA KATIKA MAZISHI, ILIKUWA NI MAAJABU HAIJAWAHI TOKEA HAPO MKOANI*
UMATI WA WATU NJIANI KUELEKEA MAZISHI YA NYAWANA 
[TUNAOMBA RADHI KWA VIDEO HII KWANI HAIJACHUKULIWA KATIKA MAZINGIRA BORA, VIKWAZO VILIKUWA VINGI IKIWEMO MWENDOKASI WA GARI NA GIZA]

PICHA ZA MAZISHI YA NYAWANA FUNDIKIRA

MAMAA NYAWANA AMEPUMZISHWA KATIKA MAKAZI YAKE YA MILELE KATIKA MAKABURI YA ITETEMYA HAPA MKOANI TABORA, NJE KIDOGO NA MJI
MAZISHI YAMECHELEWESHWA KUTOKANA NA KUCHELEWA KUWASILI KWA MWILI HUO WA MAREHEMU

Umati unaosubiri mwili wa Nyawana umevunja rekodi!


Kadri muda uendavyo ndivyo watu wamezidi kufika ulipo msiba wa Nyawana Fundikira, maeneo ya Gongoni, Tabora mjini. Hata hivyo mwili wake umechelewa kidogo kuwasili mjini hapa lakini watu wameendelea kujazana wakikaa juani bila taabu yeyote. Hii ni ishara kuwa watu wa Tabora walimkubali sana Nyawana ambaye wao walipenda kumwita Mamaa Nyawana au Jembe! kwani watu wapatao elfu moja wamejitokeza kushuhudia au kutoa heshima za mwisho kwa Nyawana.

Sheikh akitoa mawaidha mawili matatu kwa wahudhuriaji








Waombolezaji wakisubiri mwili wa Marehemyu Nyawana uwasili kutoka Dar es Salaam.






Chakula kikiandaliwa



Waombolezaji wakiwa katika hali ya huzuni kubwa kwa kuondokewa na kipenzi cha Tabora Mamaa Nyawana
Huzuni huzuni huzuni!

Voice of Tabora ( Vot fm 89.0fm) kurusha live shughuli za mazishi ya Nyawana Fundikira

Mac Denny akiwa na baadhi ya wafanyakazi wenzake wa VOT fm 89.0  redio walipokuwa wakiwasilisha ubani wao kwa Baba mdogo wa marehemu Bw Adam Fundikira
Kituo cha redio cha Voice of Tabora kimejitolea kurusha Live shuhuli zote za mazishi ya marehemu Nyawana Fundikira ambaye aliwahi kufanya kazi katika kituo hicho kwa miaka kadhaa. Kituo hicho cha redio kinamilikiwa na Mh Aden Rageh mbunge wa Tabora mjini. Familia ya marehemu imepongeza hatua hiyo ya VoT fm kwani wapenzi wengi wa Mamaa Nyawana ambao hawatoweza kufika Tabora kumzika wataweza kufuatilia mazishi yake bila wasiwasi. Hongera Voice of Tabora 89.0 fm
 Fundi mitambo Dj Faster akiandaa urushaji Live shuhuli ya maziko ya Nyawana

Gari la matangazo live la Vot fm 89.0

Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu wakimsikiliza ustaadh nyumbani kwa Baba mkubwa wa marehemu Nyawana Gongoni, Tabora.


SAFARI YA MWILI WA MAMAA NYAWANA FUNDIKIRA TOKA DAR KUELEKEA TABORA


Msanii wa kundi la taarabu la mashauzi classic Thabit Abdul akiwa amebeba jeneza la mwili wa marehemu msanii Nyawana Fundikila pamoja na wausika wengine kwa ajili ya kupereka kwenye gari iliyomsafirisha kwenda tabora kwa ajili ya maziko

Kisomo cha Marehemu Nyawana Leo Tabora!

Ndugu, Jamaa na Marafiki Wakiwa Katika Kisomo cha Marehemu Nyawana Leo Tabora
Shekhe Katika Kisomo cha Marehemu Nyawana Leo Tabora!
DJ Fimbo (aliyevaa prova ya njano)Mmoja wa wafanyakazi wa kituo cha redio VoT FM ambacho marehemu alishawahi fanyia kazi
Ndugu, jamaa na marafiki katika wakati mgumu wa maombolezo
majonzi mazito

Nyawana kuzikwa kesho Tabora!

NYAWANA |Mama wa matashititi enzi za uhai wake
MULARD | MUME WA ZAMANI WA NYAWANA [CHANZO CHA PICHA]

Mwanamuziki maarufu wa Taarabu marehemu Nyawana Fundikira anatarajiwa kuzikwa kesho mchana au jioni kutegemeana na uwasili wa mwili wa marehemu mkoani Tabora. Ambapo baada ya kufanyiwa yale yote muhimu mkoani Dar mwili wake utasafirishwa kwa njia ya gari mpaka mjini Tabora kwa mazishi.



Mazishi yake yatafanyika kijijini kwao Itetemya yalipo makaburi na Ikulu ya familia ya kichifu ya Fundikira na Mtemi Isike Mwana Kiyungi. Nyawana Fundikira ambaye ameacha watoto wawili Said Murad (22) na Queen Murad (15) ambao alijaliwa kuwapata katika ndoa yake yake ya kwanza na Bw. Omar Khamis Murad (pichani). Murad mwanamichezo maarufu sana mjini Tabora ni meneja wa uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.