05/13/13

Warembo wa Redds Miss Tabora 2013 wakijfua vikali

Najifua mpaka kieleweke
Warembo watakaoshiriki shindano la kumtafuta Redds Miss Tabora 2013 litakalofanyika katika ukumbi wa Frankman Palace  mnamo tarehe 31.Mei.2013 wamekuwa wakiendelea na mazoezi makali chini ya mwalimu wao Miss Pili Issa ambaye ni Miss Tabora 2010 katika ukumbi wa Club Royal mjini Tabora. Katika onesho hilo ambalo linatarajiwa kuhudhuriwa na mkuu wa mkoa wa Tabora Mh Fatma Mwassa kama mgeni rasmi, kiingilio kitakuwa sh elfu 10 kwa viti vya kawaida na sh elfu 20 kwa viti maalum VIP.



Nina asili ya Tabora! - Ommy Dimpoz!

Msanii anayekuja juu kwa kasi kama moshi wa kifuu Ommy Dimpoz ambaye hivi juzi alihojiwa na kituo maarufu cha redio mkoani Tabora CG fm 89.5, alisema pamoja na kuimba katika wimbo wa wasanii wa Kigoma lakini yeye pia ana asili ya Tabora kwa kuwa Mama yake mzazi aliziliwa na kukulia hapa kabla ya kuhamia Dar, na pia aliweka wazi kuwa baba yake ndio mtu wa Kigoma. Ommy Aliyekuwa akihojiwa na Ibrahim Haruna na DJ Kessy wa CGfm 89.5 ambao ni wadhamini wa Redds Misss Tabora 2013.