02/08/14

Hanifa Fundikira ahitimu uzamili!

Mwanadada Hanifa Mdemu Fundikira leo hii katika chuo kikuu cha Northampton amehitimu shahada ya uzamili katika utalii  (Masters in Tourism management) Blog hii na blog mama Keronyingi blog zinachukua fursa hii kumpongeza bibi Fundikira kwa mafanikio haya makubwa ki elimu. Tunamtakia afya njema na mafanikio katika yote ayafanyayo.

Bibi Hanifa Mdemu Fundikira akipozi nje ya Chuo kikuu cha Northampton nchini England baada ya kuhitimu.