02/03/15

Mfereji mpya wa maji wahatarisha watumia barabara ya Boma Tabora!

Kushoto unaonekana mfereji wa maji.


Baada ya mfereji huo kuchimbwa na kujengewa kwa mawe, udongo uliotokana na uchimbaji wa mfereji huo umeachwa kando kando ya Boma Road nje ya Holiday Park Guest house na kusababisha adha katika upishanaji wa magari hasa makubwa yapitayo katika barabara hiyo ambayo kabla ya kuachwa vifusi hivyo vya udongo tayari ni nyembamba. Haikuweza kufahamika mara moja ni nani muhusika na huo mfereji lakini huenda ikawa mfereji huo ukawihusu Manispaa ya mkoa wa Tabora. Blogu hii ingependa kuwakumbusha wahusika kuondosha vifusi hivyo ili kuepusha ajali zinazoweza kuotoa eneo hilo.


Barabara ya Boma inavyoonekana pichani