05/03/13

Siku Mapacha watatu walipovamia Tabora!

Bendi machachari ya Mapacha watatu toka jijini Da re Salaam ilifanya onesho kabambe mjini Tabora katika ukumbi wa Frankman Palace usiku wa   alhamisi. Bendi hiyo ikiwa china ya mkurugenzi wake Jose Mara(Mzee wa Kimara) na rapa machachari Khalid Chokoraa ilikuwa njiani kueleka Kahama na ambako walifanya onesho siku ya Ijumaa na leo Jumamosi watakuwa jijini Mwanza.

Mkurugenzi wa Bendi ya Mapaha watatu akifanya vitu vyake jukwaani

Wanenguaji wakimwaga vimbwanga!

Shughulikaaaa!

Mariam Zidane akinengua!

Mikono mbele, twende!


Washabiki wa Mapacha watatu wakiongozwa na Benny Ngwasuma wakila bata ndefuuuu!