04/12/15

Siku Mh Al Shaymaar Kweigir alipoweka uheshimiwa pembeni na kusema IMETOSHA!


Mh Al Shaymaar akicheza wimbo wa Imetosha na balozi Mdimu pamoja na  baadhi ya watu waliohudhuria matembezi ya uhamasishaji wimbo huo uliimbwa na msanii wa reggae Jhikoman Manyika  .
Siku ya matembezi ya uhamasishaji dhidi ya mauaji ya watu wenye ualbino yaliyofanika kutoka viwanja vya Biafra mpaka viwanja vya leaders mbunge wa viti maalum Mh Al Shaymaar Kweigir aliamua kuuvua uheshimiwa kwa muda na kujichanganya na wadau wengine walijitokeza kiwanjani hapo kwa kucheza kwa hisia kubwa yenye kuinesha kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Imetosha foundation za kuelimisha na hatimaye kutokomeza kabisa unyanyapaa, ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino duniani! Matembezi na tamasha viliandaliwa na Imetosha foundation kwa dhamini toka IPTL, Legendary Music, EFM Radio, TDL, Coca Cola, Ultimate security na Flexible studios
Mwenyekiti wa Imetosha foundation akimpongeza Mh Al Shaymaar baada ya matembezi.










MC mkongwa Mzee Mdachi akiwa katika pose!

Nyie chukueni selfie mie nimevutiwa na ya jukwaani!
Rose Manumba na Jamila wakiwakilisha!
Monica Joseph kulia akiongea na baadhi ya wadau wa harakati za Imetosha

Emmanuel Masaka akijiuliza Nitumie camera gani hapa????

Kelvina na Jestina  wa Jestina George blog
Wajumbe  wa Imetosha foundation!
Picha zote na Mkala Fundikira wa keronyingi blog