Breaking news! Jaji wa Redds Miss Tabora afariki asubuhi hii!

Breaking news! Jaji wa Redds Miss Tabora afariki asubuhi hii!

Marehemu Terry Mbaika siku ya shindano la Redds Miss Tabora 2013
Aliyekuwa jaji katika shindano la Redds Miss Tabora 2013 Miss Terry Mbaika (pichani kushoto) amefariki leo hii asubuhi katika hospitali ya Jeshi ya Mirambo mjini Tabora. Taarifa zimeeleza kuwa Madame Terry ambaye ni Mkenya ki uraia alikuwa Mc maarufu mjini hapo na alikuwa akimiliki duka la virutubishi liitwalo TIENS, alilazwa katika hospitali hiyo na baadaye kuruhusiwa lakini hali yake ikawa mbaya na kurudishwa hospitalini hapo na hatimaye kufariki asubuhi ya leo. Nikiwa mwenyekiti wa kamati ya Redds Miss Tabora 2013 natoa salamu za rambi rambi kwa famila yake, kwani Marehemu Terry akishirikana na majaji wenzie waliwezesha kwa kiasi kikubwa kulifanya shindano hilo kupata washindi watatu ambao walikubalika na watu wote waliodhuria shindano hilo mapema mwaka huu katika ukumbi wa Frankman Palace mnamo tarehe 31/05/2013. Tumepoteza mdau muhimu na daima tutamkumbuka Terry MbaikaMungu ailaze roho yake pema peponi. Amen!
Kutoka kushoto Majaji Evans, Terry Mbaika, Mkala Fundikira, Irene Madumba na Wendy Charles.
Majaji kazini kwa umakini.
Hapa jaji Terry Mbaika akimfuatilia kwa umakini na ukaribu mshiriki wa Redds Miss Tabora 2013 katika shindano la kipaji.