mkalamatukio

Kalapina aunguruma Mtambani kata ya Mzimuni!

Karama Masoud aka Kalapina akihutubia wakazi wa eneo la Mtamba kata ya Mzimuni leo jioni







Mwanaharakati Kalapina akimwaga sera kwa wakazi wa Magomeni Mikumi leo

Picha na Hassan Kachloul

Zetrida Ezekiel atoka na Ringa na Yesu!


Zetrida Ezekiel ni mwanamuziki mahiri wa muziki wa injili aishiye mkoani Kigoma, amekuwa mwanamuziki wa nyimbo za injili ambaye ni mwana kwaya wa  kikundi maarufu na kikongwe cha nyimbo za injili cha MKE MWEMA cha mjni Kigoma. Zetrida ameolewa na ni mama wa watoto wanne, wa kike wawili na wa kiume wawili.

Lakini baada ya kupata rai nyingi na kwa muda mrefu toka kwa wachungaji wake na watu mbali mbali kuwa atengeneze albamu yake kama mwanamuziki wa kujitegemea,hatimae mwezi wa August mwaka huu Zetrida alikuja Dar es Salaam na kuanza kazi ya kutengeneza albam yake binafsi.
Zetrida Ezekiel akiwa katika pozi.



Album yake inayoitwa Ringa na Yesu ina nyimbo nane na nyimbo zote amezifanyia Tika records chini ya mtayarisha muziki maarufu nchini aitwaye Ephraim Kameta ambapo nyimbo sita katika albam yake hiyo zilitengenezwa na Kameta na mbili zikitengenezwa mtayarisha muziki machachari PG zote katika studio za Tika records pia. Katika albam hiyo kuna nyimbo kama Ringa na yesu liyobeba jina la albam Malaika, waombee maadui zako na nyingine nyingi zenye kiwango cha hali ya juu.

Akiongea na mtandao huu kwa njia ya simu Zetrida alipoulizwa ana mipango gani ya kufanya video ya albam hiyo Zetrida alisema "Natamani sana hata leo nianze kuandaa video lakini pesa inagomba kwa saa hasa baada ya kutoka kuandaa albam hii ya audio ambaye imechukua pesa nyingi kuandaa, inabidi nijpange tena kwanza"
Na alipoulizwa nini mipango yake ya baadae baada ya lutoa albamhiyo alisema "Mipango yangu ya baadae ni kumtangaza Yesu ndani na na nje ya Tanzania kwa kuwa ni kitu kilicho ndani ya damu yangu" Pia alielezea changamoto alizokutana nazo wakati akitayarisha albam hiyo ni pamoja kutofanya kazi kwa wakati uliopangiwa jambo ambalo hutokana na sababu mbali mbali ikiwemo katikizo la umeme, ambapo inatokea kazi iliyokuwa ifanyike jana inahamishiwa leo na wa leo ama utafanya kazi mida mibaya au kupangiwa siku nyingine. Lakini nashukuru sana kuwa nimeeza kumaliza albam hiyo bila tatizo.

Mwisho kabisa Zetrida alipenda kutoa shukurani zake akisema "Napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa ujasiri wa kufanya albam yangu mwenyewe na pili mume wangu kwa kuniruhusu kufanya kazi hii ya uimbaji pia kujitoa kwake kwa hali na mali, vile vile bila kumsahau Mchungaji Joseph Malumbu wa Kijichi Mtongani ambaye alihusika katika usimamaizi wa albam ya Ringa kwa Yesu. Pia niwaombe tu wapenzi wa muziki wa injili waipokee albam yangu na wainunue kwa wingi kwani humo kuna nyimbo nzuri sana zenye kumtukuza Bwana Yesu hivyo kila mmoja ajipatie nakala yake sasa kwani tayari albami ipo madukani.
Kwa mialiko popote ndani na nje ya Tanzania wasiliana naye kwa nambari
+255675 406917/ +255756823477
au kwa barua pepe
zetridaezekiel@yahoo.com 

Nipeni mwaka mmoja tu muone mabadiliko Kinondoni!- Karama (Kalapina) Masoud

Mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bw Karama Masoud aka Kalapina akiwahutubia wakazi wa Kinondoni Moscow kituo cha polisi jijini Dar es Salam leo jioni.
Msanii maarufu wa muziki wa kufoka foka nchini Bw Karama Masoud (Kalapina) leo hii aliendelea na kampeni zake za kutafuta kura katika jimbo la Kinondoni ambapo leo alifanya mkutano Kinondoni Moscow kituo cha polisi mkutano ambao ulihudhuriwa na wagombea udiwani wa kata za Ndugumbi, Magomeni, Mzimuni na Kigogo.



Awali wasanii wa muziki wa kizazi kipya Domokaya, TID, KR Mullah wa TMK Family walitoa burudani safi kwa wakazi wa eneo hilo waliohudhuria mkutano huo wa kampeni. Hata hivyo katika hali ya kustaajabisha ilitokea sintofahamu katika mkutano huo baada ya generator mbili kushindwa kufanya kazi na kuufanya mkutano huo kusimama kwa muda, ambapo ilifuatwa generator nyingine ya tatu ambayo nayo ilichukua muda mpaka ilipoweza kufanya kazi. 

Akiongea kwa hisia kali na wapiga kura hao, Kalapina alisema "Nikiwa mzaliwa na niliyekulia Kinondoni naelewa matatizo yenu kuanzia mazingira machafu, mafuriko ya mara kwa mara na gonjwa hatari la kipindupindu  na mengineyo mkinipa kura za kuniwezesha kwenda bungeni nitahakikisha katika kipindi cha mwaka mmoja tu mtaona mabadiliko ya mazingira hapa Kinondoni na ninawaruhusu nisipotekeleza mje mnifanyie fujo nyumbani kwangu na hata polisi wakija nitawaambia wananchi wangu wana haki ya kufanya wafanyalo kwa kuwa sijatimiza ahadi zangu.

Akimuelezea mbunge aliyepo sasa Mh Idi Azan alisema "Kwa miaka 10 sasa hali ya mazingira ya Kinondoni imedorora, Idi Azan hana lolote alifanyalo yani yupo yupo tu" aliongeza kusema "Kama kuna mtu yupo hapa alipata kumsikia Idi Azan akiongea chochote aje hapa aniambie nitampa sh elfu 10, jambo ambalo lilizua kelele za watu wakisema hawajawahi kumsikia akiongea chichote bungeni"
  

Baadhi ya wakazi wa Kinondoni Moscow wakimsikiliza mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bw Kalapina leo jioni.
Mbgombea ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bi Asma (mwenye kilemba cha zambarau) akifuatilia hotuba mbali mbali mbali katika mkutano wa kampeni ya ubunge leo.
Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama cha ACT Bw Nixon Tugara akihutubia wakazi wa Kinondoni Moscow
Mgombea ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bi Asma akiwasalim wakazi wa Kinondoni Moscow waliojitokeza kumsikiliza mgombea ubunge wa jimbo hilo Bw Karama Masoud. 

Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Q Chillah (fulana nyeupe) na TID (mwenye miwani na balaghashia) wakifuatilia mkutano baada ya kufanya maonesho kabla ya mkutano huo kuanza.
Baaadhi wa wafuasi wa Bw Kalapina ambaye ni mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni wakifuatilia mkutano.
Wagombea udiwani kwa tiketi ya ACT Wazalendo wa kata za Ndugumbi, Mzimuni, Kigogo na Magomeni wakitambulishwa kwa wapiga kura wa Kinondoni Moscow.
Mshabiki wa mgombea wa ACT Wazalendo ubunge wa jimbo la Kinondoni akishangilia huku akiwa kabeba bango lenye picha ya mgombea huyo.

Mgombea wa udiwani kata ya Hananasif wa ACT Wazalendo Bw Baruani aka Komandoo akiwasalim wapiga kura wake.







Mkurugenzi wa uchaguzi wa chama cha ACT wazalendo Bw Nixon Tugara kulia na Bi Asma wakiwa jukwaani


Mgombea wa ubunge kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo Bw Karama Masoud Kalapina katikati akifuatilia mkutano huo wa kampeni.
Bi Asma akimtambulisha Kalapina kwa wapiga kura wa Kinondoni Moscow kituo cha polisi.

Kalapina akimwaga sera makini
Picha na habari na Mkala Fundikira

Mamia wafariki katika mkanyagano Saudi Arabia

Eid al-Adha

Image copyrightSaudi Civil Defence Directorate
Image captionWatu zaidi ya 717 waliokuwa wakishiriki sherehe za hija wamefariki kwenye mkanyagano uliotokea karibu na mji mtakatifu wa Kiislamu wa Mecca, maafisa nchini Saudi Arabia wamesema.
Idara ya ulinzi wa raia nchini humo imesema watu wengine 863 wamejeruhiwa katika kisa hicho kilichotokea eneo la Mina, takriban kilomita tano kutoka mji wa Mecca.
Maafa hayo yalitokea mahujaji takriban milioni mbili walipokuwa wakishiriki moja ya kaida muhimu za mwisho katika ibada za hija.
Ndio mkasa mbaya zaidi kutokea wakati wa hija katika kipindi cha miaka 25.
Mahujaji husafiri hadi Mina wakati wa kuhiji kurusha mawe saba kwenye nguzo saba zijulikanazo kama Jamarat, ambazo huwakilisha shetani.
Nguzo hizo zimo katika eneo ambalo inaaminika Nabii Ibrahim alijaribiwa na shetani.
Ramani ya eneo la Mecca
Watu walikuwa wakielekea eneo la kurushia mawe, na wengine wakitokea huko pale ghafla watu walipoanza kuanguka.
Kulikuwa na raia wa Nigeria, Niger, Chad na Senegal miongoni mwa mataifa mengine.
Idara ya ulinzi wa raia Saudi Arabia imesema mkanyagano huo ulitokea pale kulipotokea "ongezeko la ghafla" la watu waliokuwa wakielekea kwenye kwenye nguzo za kurushiwa mawe.
Waziri wa afya wa Saudi Arabia Khaled al-Falih amesema mkanyagano huo ulitokea kwa sababu mahujaji walikosa kufuata maagizo.
"Wengi wa wahamiaji huenda bila kufuata ratiba iliyowekwa," amesema.
Mwandishi wa BBC Hausa Tchima Illa Issoufou aliyekuwa ameenda kuhiji ni mmoja wa walioathirika. Anasema shangazi yake alifariki na baadhi ya watu alioandamana nao hawajulikani waliko.
"Watu walikuwa tu wakiimba jina la Allah, huku wengine wakilia, wakiwemo watoto. Watu walianguka sakafuni na hakukuwa na wa kuwasaidia. Ni kana kwamba kila mtu alikuwa anajijali mwenyewe," amesema.
Mkanyagano huo umetokea siku ya kwanza ya sherehe za Eid al-Adha.
Idara ya ulinzi wa raia Saudi Arabia imesema maafisa 4,000 wametumwa eneo hilo kusaidia pamoja na wahudumu 200 wa huduma za dharura.
Kurusha maweImage copyrightAP
Image captionMahujaji hukusanyika kurushia mnara mawe kama ishara ya kumrushia shetani mawe
Maandalizi ya ibada hizo za hija yalikuwa yamekumbwa na mkasa baada ya kreni kuanguka katika msikiti mkuu wa Mecca mwezi huu na kuua watu 109.
Hii si mara ya kwanza kwa mikasa kutokea wakati wa hija.
Mikasa mingine iliyotokea wakati wa kuhiji:
2006: Mahujaji 364 walifariki wakati wa kurushia mawe mnara unaoashiria shetani
1997: Mahujaji 343 walifariki na 1,500 kujeruhiwa kwenye mkasa wa moto
1994: 270 waliuawa katika mkanyagano
1990: Mahujaji 1,426 waliuawa katika mkanyagano njia za kupitia chini za kuelekea maeneo matakatifu
1987: Watu 400 walifariki maafisa wa serikali walipokabiliana na waandamanaji waliounga mkono Iran.
Habari na picha kwa hisani ya BBCswahili

RAIS DK. JAKAYA KIKWETE ATOA ZAWADI YA IDD EL HAJI KWA MAKUNDI MBALIMBALI


 Kamshna Msaidizi Kitengo cha Walemavu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Beatrice Fungamo (kulia), akimkabidhi Mwakilishi wa Mahabusu ya Watoto Upanga, Regina Kuname msaada wa vyakula na kitoweo cha mbuzi na mafuta ya kula kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya ya Idd El Haji Dar es Salaam leo asubuhi.
 Kamshna Msaidizi Kitengo cha Walemavu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Beatrice Fungamo (kulia), akimkabidhi Katibu Mtendaji wa Chama cha kulea Watoto Mayatima (Chakuwama) cha Sinza, Hassan Hamisi kwa ajili ya sherehe hiyo.
 Mbuzi wakiingizwa kwenye gari baada ya wahusika kukabidhiwa.
 Vyakula vilivyotolewa na Rais Jakaya Kikwete vikiwa eneo la tukio vikisubiri kuchukuliwa.
Mwakilishi wa Kituo cha Wazee na Wasiojiweza cha Nunge kilichopo Kigamboni, David Mpangala akiwa na mbuzi waliotolewa kwa ajili ya kituo hicho.

Na Dotto Mwaibale

RAIS Jakaya Kikwete ametoa zawadi ya vyakula na kitoweo kwa makundi mbalimbali kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Idd El Haji ambayo inaadhimishwa duniani kote leo.

Zawadi hiyo imekabidhiwa kwa makundi hayo kwa niaba yake na Kamshna Msaidizi Kitengo cha Walemavu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Beatrice Fungamo Dar es Salaam leo asubuhi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukabidhi zawadi hiyo, Fungamo alisema Rais ametoa zawadi hiyo kwa ajili ya Sikukuu ya Idd El Haji kama anavyofanya siku zote wakati wa sikukuu mbalimbali.

Fungamo alitaja vituo vilivyopata zawadi hiyo kuwa ni Mahabusu ya Watoto ya Upanga iliyopo Manispaa ya Ilala, Makazi ya Wazee wasiojiweza ya Nunge, Kigamboni, Chuo cha Watu wenye Ulemavu cha Yombo Temeke na Kituo cha Kulelea Watoto Mayatima (Chakuwama) cha Sinza.

Alitaja vituo vingine kuwa ni Kituo cha Makao ya Watoto Yatima cha Mburahati, Ilala, Kituo cha Makao ya Watoto-Kurasini, Kituo cha Full Gospel, Temeke na Kituo cha Watoto Alsaad Children House Kurasini.

Alivitaja vituo vingine kuwa ni cha Vosa Mission cha Kongowe, Temeke na Kituo cha Kijiji cha Furaha kilichopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Fungamo alitaja vituo vilivyopata zawadi hiyo ya Idd El Haji kwa upande wa Zanzibar kuwa ni Kituo cha Mabaoni kilichopo Pemba na Makazi ya Wazee Sebleni yaliyopo Unguja.

Alitaja vituo vingine vilivyopo mikoani vilivyopata zawadi hiyo kuwa ni kituo cha The Village of Home cha Dodoma, kituo cha Moyo Mmoja cha Bagamoyo mkoani Pwani, kituo cha watoto cha Tosamaganga kilichopo mkoani Iringa na Mahabusu ya Watoto Arusha na Tanga.

SWALA YA IDD EL HAJI ILIVYOFANYIKA VIWANJA VYA MWEMBE YANGA TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM LEO


 Sheikh Abdu Kadri akiongoza swala ya Idd El Haji katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es Salaam leo asubuhi. Waislam wa Tanzania leo waliungana na wenzao duniani kote kusherehekea Sikukuu ya Idd El Haji.
 Sheikh Nurdin Kishki alipohotuba baada ya swala hiyo.
 Sheikh  Othman Dishi akitoa maelekezo kabla ya kuanza kwa swala hiyo.
 Waumini wa dini ya kiislam wakiwa katika swala.
 Wanawake na watoto wakiwa kwenye swala hiyo.
 Mazuria ya kuswalia yakitandikwa kabla ya kuanza ibada.
 Hapa wakitawaza kabla ya kuinza kwa swala hiyo.
Abdurahi Suleiman (kulia), akiuza mafuta na manukato mbalimbali katika viwanja hivyo.
 Ibada ya swala ya Idd El Haji ikiendelea.
 Biashara ya Balaghashia ikiendelea katika viwanja vyao.
 Swala ikiendelea katika viwanja hivyo.
 Pikipiki na baiskeli zikiwa zimewekwa kwa pamoja kwa ajili ya usalama.
 Mwanahabari akichukua picha katika ibada hiyo.
 Waumini wa kiislam wakiwa katika viwanja hivyo wakati wa ibada hiyo.
 Hapa salamu zikiendelea.
 Sheikh Othmani Dishi (kushoto), akisalimiana na Sheikh Abdu Kadri kabla ya kuanza kwa swala hiyo.
 Swala ikifanyika katika viwanja hivyo.
 Swala ikifanyika kwa unyenyekevu mkubwa.
Swala ikiendelea.