mkalamatukio

Tabora Stand Up; Eid Mosi Wasanii Wafurika Hapatoshi.

Shangwe na burudani za kutosha zinatarajiwa kufanyika katika sikukuu ya Eid hapo kesho mkoani Tabora panapo majaaliwa ya M/Mungu. Mashabiki mbalimbali mjini Tabora watarajiwa kufurahia onesho hilo katika maeneo mawili tofauti ambapo mchana itakuwa Bwalo la Polisi kuanzia saa 8 mchana na Usiku katika viwanja vya Muungano Mesi kuanzia saa 2 usiku.
Wasanii wa kila nyanja wametua mjini hapo na kufanya mahojiano CG Fm Redio leo mchana; wasanii hao ni Kassim Mganga a.k.a tajiri wa mahaba, Ommy Dimpoz, Mkude Simba (Kitale) na rafiki yake Stan Bakora, Young Killer, na Baraka Da Prince.
Eid_Tabora (8)
Kassim Mganga akiwa CG Fm Redio, 89.5 The point of no Return
Eid_Tabora (11)
Ommy Dimpoz
Eid_Tabora (4)
Eid_Tabora (7)
Manoni (Mtangazaji CG Fm Redio 89.5 The Point of no Return) akifanya mahojiano na wasanii.
Eid_Tabora (13)
Mkudesimba Original (Kitale)
Eid_Tabora (14)
Kitale na Stani Bakora, ...eti "Tembo wa Ulaya mkubwa sana kama mbuzi"
Eid_Tabora (17)
Stan Bakora
Eid_Tabora (9)
Baraka Da Prince
Eid_Tabora (16)
Stephania (Mtangazaji CG FM)
Eid_Tabora (15)
Eid_Tabora (12)
Young Killer (Handsome aliyekosa matunzo) akishuka free style.
Eid_Tabora (5)
Mgalula Fundikira (Mkurugenzi wa Royal Nsyepa Entertainment) akizungumzia maandalizi ya onesho hilo aliloliandaa baada ya muda mrefu toka arudi kutoka Hispania
Eid_Tabora (3) Eid_Tabora (2) Eid_Tabora (18)
Kutoka kushoto, Kassim Mganga, Mubenga (Meneja wa Ommy Dimpoz), Stan Bakora na Abdul katika nyumba za Tabora Rest House walikofikia wasanii hao.
Eid_Tabora (19)  
Wakijipima uwezo wa ukali wa "SAUM"
Picha na Aloyson -TBN Kanda ya magharibi

Bandora Mirambo alipochukua fomu ya ubunge wa Tabora mjini mapema leo.



Bandora Salum Mirambo akionesha fomu yake ya ubunge kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi
Mama Hidaya Rashid Amani katibu msaidizi wilaya akimuandikia risiti Bw Bandora.
Bandora Mirambo akitia sahihi katika kitabu cha kuchukulia fomu ya ubunge wa Tabora mjini.

Ada ya fomu!
Maelekezo!
Saidi Zaidi kulia na Juma Mgawe wakifuatilia kwa makaini makabidhiano ya fomu.

Mama Hidaya Rashid Amani akitoa maelekezo ya ujazaji fomu
Bandora akisalimiana na mdau nje ya ofisi za CCM Wilaya.
Apolo (kushoto) akiwa na Bandora Mirambo mara baada ya Bandora kuchukua fomu.
Bandora akipongezwa na kada wa chama baada ya kuchukua fomu ya ubunge kwa jimbo la Tabora mjini.
Bandora Mirambo akiwa na baadhi ya wapiga kura wa jimbo hilo waliomsindikiza kuchukua fomu katika ofisi za CCM  wilaya ya Tabora mjini.

Binti wa Michuzi Ajitoa Kimasomaso; Achukua Form ya Ubunge wa Viti Maalum

 
 Zahara Michuzi alipowasili katika ofisi za CCM mkoa wa Tabora ili kuchukua form ya kugombea viti maalum kwa vijana.

Zahara Michuzi ni binti wa Issa Michuzi blogger na mpiga picha hodari wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye anamalizia muda wake sasa.

Binti wa Michuzi mara baada ya kuhitimu elimu yake ya shahada yake ya uchumi UDOM ameona ni vyema akawatumikua wananchi wa nyumbani kwake mkoani Tabora kwa kutangaza nia ya kugombea ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
 Zahara Michuzi (kushoto) na Mwasham Hashim karani wa UVCCM Tabora akitoa maelekezo ya uchukuaji wa fomu hizo.
 Binti huyo wa Michuzi akikabidhiwa form yake leo katika ofisi za UVCCM mkoa-Tabora
 Zahara akiifurahia form yake ya Ubunge wa viti maalum Tabora.
 Zahara (kushoto) akilipia fedha halali ya form hiyo huku mama yake mlezi (katikati) akishuhudia kitendo hicho.
 Zahara sasa akianza safari yake ya kuufukuzia ubunge wa viti maalum huku akiipitia fomu
Mwasham (kushoto) akitoa baadhi ya ufafanuzi kwa baadhi ya vipengele vilivyomo katika form hiyo.
Picha zote na aloyson.com TBN

VYUO VYATAKIWA KUTOA ELIMU KULINGANA NA MAHITAJI YA AJIRA HAPA NCHINI



Na Woinde Shizza,Arusha
VIJANA wengi  wanaohitimu vyuo hawapati kazi mara tu ya kuhitimu

masomo yao kutokana na kutokuwepo kwa vyanzo vya ajira vinavyokwenda
sambamba na ongezeko la wahitimu na kuchangia kuwepo kwa wimbi la
wahitimu wasiokuwa na ajira nchini.



Hayo yalisemwa    na Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya maliasili na
utalii ,Selestini Gesimba alipokuwa akizungumza katika mahafali ya
tano ya Chuo cha Taifa cha Utalii(NCT) ,kampasi ya Arusha ambapo jumla
la wanafunzi 55  walihitimu fani za mapishi, uokaji,mapokezi,na huduma
ya vyakula na vinywaji katika ngazi ya cheti.



Alivitaka vyuo mbalimbali kutoa elimu kulingana na mahitaji ya ajira
ili kuwezesha wanafunzi wanaohitimu kupata ajira  kwa haraka na
hatimaye kuondokana na changamoto ya wimbi kubwa la wanafunzi
wanaohitimu na kukaa mtaani bila ajira.



Gesimba alitoa rai kwa vijana wa kitanzania kujiunga na Chuo cha Taifa
cha Utalii ili wapate ujuzi ambao utatoa fursa ya kufanya kazi kwenye
sekta ya utalii na pia fursa ya kuweza kujiajiri wenyewe.



‘sekta ya utalii nchini ni ya muhimu sana na inapaswa kudhaminiwa
kwani imekuwa ikichangia asilimia 17.5 kwenye pato la Taifa na
kuifanya kuwa ya kwanza kwa kuingizia Taifa Dola bilioni mbili
ikifuatiwa na sekta ya madini ambayo imeliingizia Taifa Dola bilioni
1.7 mwaka 2004 .’alisema Gesimba.



Alisema kuwa, sekta hiyo ni miongoni mwa sekta inayokuwa kwa kasi
kubwa duniani ambapo imekuwa ikikua kwa  asilimia 4.5 hadi 5 kwa mwaka
ambapo imekuwa chachu ya kukuza na kuendeleza sekta nyingine za
kiuchumi kama kilimo, miundombinu , mawasiliano na usafiri pamoja na
kuwa kichochea kikubwa cha kupunguza umaskini katika jamii.



Naye Mtendaji Mkuu wa wakala wa chuo cha Taifa cha Utalii ,Rosada
Msoma alisema kuwa,chuo hicho kimekuwa kikijitahidi kutoa mafunzo na
kuwaunganisha wanafunzi wake na fursa mbalimbali za ajira ambapo kwa
mwaka huu kati ya wanafunzi hao 55 tayari wanafunzi 21 wameshapata
ajira huku wengine wakiendelea kuitwa kwenye usahili maeneo
mbalimbali.



Akisoma risala kwa niaba ya wanafunzi wenzake,Neema Mollel alisema
kuwa chuo hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu
wa jenereta pindi umeme unapokatika chuoni hapo, ukosefu wa hostel
changamoto inayosababisha wanafunzi wanaosoma mbali kutoweza
kuhudhuria kozi mbalimbali chuoni hapo.



Aidha waliomba chuo hicho kuwezeshwa zaidi na kuweza kutoa kozi
mbalimbali kwa ngazi ya diploma ili kuwawezesha wanafunzi wake kupata
elimu ya juu zaidi ambapo itawawezesha kukabiliana na changamoto ya
ajira ndani na nje ya nchi.



Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha ,Adoh  Mapunda alisema kuwa,serikali
mkoani Arusha wapo tayari kushirikiana na chuo hicho katika kuboresha
huduma mbalimbali za masomo ili kuwezesha chuo hicho kukua zaidi na
kuendelea kutoa elimu iliyo bora zaidi.



Mapunda alikitaka chuo hicho kuboresha zaidi maswala ya hoteli ili
kuwavutia wateja wengi zaidi kuweza kujiunga chuoni hapo kutokana na
elimu nzuri ,na kuwataka wanafunzi hao kuwa mabalozi wazuri wa
kukitangaza chuo hicho ndani na nje ya nchi kwa ujumla.

Bandora uso kwa uso na Mh Aden Rageh ubunge Tabora mjini!

Bandora Salum Mirambo akiwasilia katika ofisi za CCM wilaya ya Tabora kuchukua fomu za ubunge wa Tabora mjini
Wagombea ubunge wa jimbo la Tabora mjini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mh Aden Rageh na Bandora Mirambo leo 
hii walikutana uso kwa uso walipofika ofisi za CCM wilaya kuchukua fomu za kuwania kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge wa wa Tabora mjini. Wote wawili katika kuonesha siasa si chuki wala ugomvi walilakiana na kusalimiana kwa uzuri kabisa.


Wawania kuteuliwa na CCM wakisabahiana
 Mh Aden Rageh ndiye mbunge aliyemaliza muda wa ubunge wa Tabora mijni ambapo alishinda ubunge huo mwaka 2010 kwa kumuangusha  kwenye kura za maoni ndani ya CCM aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kuanzia mwaka 2005 marehemu Siraju Kaboyonga ambaye naye alimshinda Henry Mgombelo mwaka 2005 aliyekuwa mbunge mwaka 2000 . Hali hii imeonesha kuwa wapiga kura wa Tabora wamekuwa na tabia ya kutorudisha mbunge katika kiti hicho kwa mara ya pili mfululizo, Mh Rageh ambaye alipata kuwa mwenyekiti kilabu cha Simba cha jijini Dar bila shaka atakuwa na kibarua kigumu cha kuuvunja mwiko huo.

Bandora Mirambo ni mkurugenzi wa kampuni ya ulinzi ya Salu Security yenye makao yake makuu mjini Sinyanga na matawi kadhaa mikoa ya kanda ya ziwa.

Tabasamu kubwa!

Kauli ya Sergio Ramos kuiambia Real Madrid anataka kujiunga na Manchester United yawakuna wengi!



Mlinzi mahiri wa kilabu cha Real Madrid Sergio Ramos amuambia uongozi wa kilabu hicho nguli kuwa anataka kujiunga na Manchester United na si vinginevyo kitendo hicho kimewapendeza mashabiki wengi wa soka hasa nchini England ambao wanaichukulia Real Madrid kama klabu onevu yaani inajiona yenye haki ya kuchukua mchezaji yeyote toka kilabu chochote na wakati wowote, kitu ambacho kimekuwa kikivikwaza vilabu vingine na hata mashabiki wao.
Kitendo cha mchzaji wao wa kutumainiwa Sergio Ramos kuamua kuondoka tena basi ili akajiunge na Man united ambao tayari wana machungu na Madrid kwa kuwachukulia Christiano Ronaldo na mbaya zaidi kumtaka goilikipa wao David de Gea. Vyombo kadhaa vya habari na magazeti ya michezo hasa ya England yameeleza kuudhiwa mno Louis Van Gaal kwa kwa kitendo cha Madrid kugoma kulipa pesa ambayo Man united ingependa Madrid wailipe kwa kuwaoka kipa bora zaidi duniani De Gea, lakini Madrid nao wanaona kwa nini walipe pesa nyingi kumnunua mchezaji ambaye mkataba wake umebakiza miezi 12 tu. Imeelezwa kuwa Man united wanataka Madrid iwalipe pauni milioni 33 huku Real Madrid wakiofa kulipa pauni milioni 10 tu. Kitu ambacho kimewaudhi Man united na wameelezwa kuwa tayari kumlazimisha De Gea amalize mkataba wake na aondoke bure kiangazi kijacho.

Real Madrid na wao sasa wanaonja joto ya jiwe toka kwa mchezaji wao, na Man united wanaitumia nafasi hiyo kuiteteresha Real Madrid. Duru zingine za habari zinaeleza kuwa hiyo ni janja ya Ramos kupata mkataba mpya na mnono toka Los Bloncos, imefahamika Ramos si mmoja wa wachezaji wanaolipwa vinono na Real Madrid hivyo anatumia mwanya huu ili kujipatia mshahara mnono.
Haya ni baadhi ya maoni ya baadhi wasabiki wa soka wengine si washabiki wa Man united lakini wanaonesha kukasirisha na kitendo cha Real kutaka wachezaji wa vilabu vingine huku wao wakigoma kuuza wao wanapotakiwa.

Habari na picha kwa hisani ya 
mailonline imefasiriwa na Mkala Fudikira

Wana jumuiya ya Kinondoni kuteua viongozi baada ya mfungo wa Ramadhani!


Wanajumuiya wa kikundi cha Kinondoni wakibadilishana mawazo baada ya mazishi ya marehemu George Nganda

Mratibu wa kikundi cha wana Kinondoni Bw Ivan Minja amesema kikundi hicho kitateua vingozi wa muda katika kikao kitakachofanyika jijini Dar es Salaam baada ya mfungo wa Ramadhan, kikao hicho kitakachoteua uongozi wa muda wakati kitafanyika siku ya Jumapili ya tarehe 26/7/2015 pale Mango Garden Kinondoni Vijana kuanzia saa 10 za jioni. Akielezea ajenda kuhusuku kikao jicho Minja alisema ajenda kuu itakuwa kwanza kuteua viongozo wa muda kisha wajumbe wote wataijadili rasimu ya katiba yao ambayo imetungwa na Bw Yahya Pori ambaye ni mwanachama katika jumuiya hiyo. Jumuiya ambayo imeanzishwa kwa dhumuni kuu la kusaidiana katika dhiki na faraja inaundwa na wakazi nawalikuwa wakazi wa maeneo ya kinondoni na si wilaya ya Kinondoni.

Vidole viwili, maana yake nini Jamila Kaimika?
Ivan Minja (Mratibu) Anna Dada na Esther Shayo. Aliyesimama ni Goodsense.



Toka kushoto Esther, Mkala Fundikira(Mratibu) Evelyn Minja na Emmy Stephen.




Picha ya pamoja

Vijana wa Kino Group wakiwa katika pose!

Picha na Abdul Kazembe