mkalamatukio

Wana jumuiya ya Kinondoni kuteua viongozi baada ya mfungo wa Ramadhani!


Wanajumuiya wa kikundi cha Kinondoni wakibadilishana mawazo baada ya mazishi ya marehemu George Nganda

Mratibu wa kikundi cha wana Kinondoni Bw Ivan Minja amesema kikundi hicho kitateua vingozi wa muda katika kikao kitakachofanyika jijini Dar es Salaam baada ya mfungo wa Ramadhan, kikao hicho kitakachoteua uongozi wa muda wakati kitafanyika siku ya Jumapili ya tarehe 26/7/2015 pale Mango Garden Kinondoni Vijana kuanzia saa 10 za jioni. Akielezea ajenda kuhusuku kikao jicho Minja alisema ajenda kuu itakuwa kwanza kuteua viongozo wa muda kisha wajumbe wote wataijadili rasimu ya katiba yao ambayo imetungwa na Bw Yahya Pori ambaye ni mwanachama katika jumuiya hiyo. Jumuiya ambayo imeanzishwa kwa dhumuni kuu la kusaidiana katika dhiki na faraja inaundwa na wakazi nawalikuwa wakazi wa maeneo ya kinondoni na si wilaya ya Kinondoni.

Vidole viwili, maana yake nini Jamila Kaimika?
Ivan Minja (Mratibu) Anna Dada na Esther Shayo. Aliyesimama ni Goodsense.



Toka kushoto Esther, Mkala Fundikira(Mratibu) Evelyn Minja na Emmy Stephen.




Picha ya pamoja

Vijana wa Kino Group wakiwa katika pose!

Picha na Abdul Kazembe

Picha mbali mbali katika mazishi ya George Nganda!


Toka kushoto ni Dada July Kitundu, Dada Rita na Mama Desouza


Majonzi yatawala makaburini!

Kamanda wa CCM tawi la Kinondoni Bwawani Bw Steve Nyerere kulia akiwa na wadau wengine

Msanii Hard Mad naye alihudhuria mazishi

Wadau wa Pazi club











Issa Mndeme na Mratibu wa Kundi la wana Kinondoni Ivan Minja wakiweka shada la maua ktk kaburi

Florah Mwakpesile na Florah Samuel




Picha na Abdul Kazembe na Mkala Fundikira

Hatimaye George Nganda azikwa na mamia ya watu!


Mama wa marehemu(mwenye nguo nyeupe)
Kijana George Nganda aliyefariki majuzi kuamkia juzi hatimaye leo hii majira ya saa 9 mchana alipumzishwa katika nyumba yake ya milele katika makaburi ya Kinondoni Fm. Mazishi hayo yaliyohudhuriwa na mamia ya watu wakiwemo wana jumuiya ya Kinondoni ambao katika umoja wao walijitolea kumsitiri kijana mwenzao rafiki yao mpendwa wao Bw George Nganda (38) kwa kuchangia sanduku, sanda na mashada. Akiongea na mtandao huu mmoja wa wajumbe wa jumuiya hiyo Bi Anna Samuel (Dada) alisema inasikitisha kumpoteza rafiki yetu mpendwa lakini tunakubali kuwa sisi tulimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi. 

Akizungumzia jumuiya yao ya wana Kinondoni mjumbe Abdul Kazembe alisema "Jumuiya imefarijika kuchangia mazihi ya mwenzetu aliyetutoka ghafla lakini huu ni mwanzo tu jumuiya inajipanga kufanya makubwa zaidi, tukianzia katika kikao cha wanajumuiya wote mara baada ya kuhitimishwa kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo tutakutana pale mango garden siku ya jumapili tarehe 26/7/2015 kuanzia saa 10 jioni ili kuteua viongozi wa muda na kisha kuijadili rasimu ya katiba ya jumuiya yetu ambayo iliratibiwa na mwanajumuiya Yahaya Pori"

Jumuiya hiyo ambayo pia inajiendesha kupitia mitandao ya Facebook na Telegram ambapo wanajumuiya wamejiunga na kujadili mambo yanayoihusu Jumuiya tu. Pia jumuiya inatarajia kufungua akaunti ya benki ili kujiendesha kiufasaha zaidi.
Baadhi ya wanajumuiya wakiwa makaburini kumzika rafiki yao George Nganda.
Msanii wa vichekesho Steve Nyerere na mdau Riziki Nyoni wakifuatilia mazishi 
Majonzi yalitawala!
Mc wa shughuli ya mazishi akiongea jambo

Wanajumuiya wa KINONDONI wakipiga picha ya mwisho katika kaburi la mpendwa wao George Nganda
Toka kulia Issa Mndeme, Evelyin Minja, Emmy Stephen
Toka kulia ni Issa Mndeme, Abdula Kazembe na Yohabu Chikwanda.
Kapumzike kwa amani George!
Picha na habari na Mkala Fundikira