mkalamatukio

Hatimaye George Nganda azikwa na mamia ya watu!


Mama wa marehemu(mwenye nguo nyeupe)
Kijana George Nganda aliyefariki majuzi kuamkia juzi hatimaye leo hii majira ya saa 9 mchana alipumzishwa katika nyumba yake ya milele katika makaburi ya Kinondoni Fm. Mazishi hayo yaliyohudhuriwa na mamia ya watu wakiwemo wana jumuiya ya Kinondoni ambao katika umoja wao walijitolea kumsitiri kijana mwenzao rafiki yao mpendwa wao Bw George Nganda (38) kwa kuchangia sanduku, sanda na mashada. Akiongea na mtandao huu mmoja wa wajumbe wa jumuiya hiyo Bi Anna Samuel (Dada) alisema inasikitisha kumpoteza rafiki yetu mpendwa lakini tunakubali kuwa sisi tulimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi. 

Akizungumzia jumuiya yao ya wana Kinondoni mjumbe Abdul Kazembe alisema "Jumuiya imefarijika kuchangia mazihi ya mwenzetu aliyetutoka ghafla lakini huu ni mwanzo tu jumuiya inajipanga kufanya makubwa zaidi, tukianzia katika kikao cha wanajumuiya wote mara baada ya kuhitimishwa kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo tutakutana pale mango garden siku ya jumapili tarehe 26/7/2015 kuanzia saa 10 jioni ili kuteua viongozi wa muda na kisha kuijadili rasimu ya katiba ya jumuiya yetu ambayo iliratibiwa na mwanajumuiya Yahaya Pori"

Jumuiya hiyo ambayo pia inajiendesha kupitia mitandao ya Facebook na Telegram ambapo wanajumuiya wamejiunga na kujadili mambo yanayoihusu Jumuiya tu. Pia jumuiya inatarajia kufungua akaunti ya benki ili kujiendesha kiufasaha zaidi.
Baadhi ya wanajumuiya wakiwa makaburini kumzika rafiki yao George Nganda.
Msanii wa vichekesho Steve Nyerere na mdau Riziki Nyoni wakifuatilia mazishi 
Majonzi yalitawala!
Mc wa shughuli ya mazishi akiongea jambo

Wanajumuiya wa KINONDONI wakipiga picha ya mwisho katika kaburi la mpendwa wao George Nganda
Toka kulia Issa Mndeme, Evelyin Minja, Emmy Stephen
Toka kulia ni Issa Mndeme, Abdula Kazembe na Yohabu Chikwanda.
Kapumzike kwa amani George!
Picha na habari na Mkala Fundikira

WANAHABARI WAPEWA SEMINA KUHUSU MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA


Kaimu Mkurugenzi Magonjwa Yasiyoambukiza wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Auson Rwehimbiza (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kwenye semina ya siku moja kuhusu magonjwa yasiyoambukiza. Kulia ni Meneja Mradi Shirikisho la Vyama vya Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza (TANCDA)

Na Dotto Mwaibale

MAISHA ya watu katika nchi zinazoendelea, yapo hatarini kutokana na asilimia 50 ya magonjwa yasiyoambukiza kusababisha vifo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, wakati wa semina ya magonjwa yasiyoambukiza iliyondaliwa mahususi kwaajili ya wanahabari yenye lengo la kukamilisha mkakati pamoja na mpango kazi 2015/2020, Kaimu Mkurugenzi Magonjwa yasiyoambukiza, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Auson Rwehimbiza aliyataja magonjwa yasiyoambukiza ni moyo na mishipa ya damu, kisukari, kansa na magonjwa sugu ya mfumo wa hewa.

Alisema magonjwa hayo yanazidi kuongezeka nchini hasa kwa jamii ya watu waishio mjini na kuongeza kuwa watu wazima wenye umri wa miaka 80 kuwa na magonjwa hayo kwa asilimia 1 hadi 3 na msukumo wa juu wa damu kwa asilimia 5 hadi 10.

"Tathmini ya mwaka 2012 iliyohusisha watu wazima katika wilaya 50, inaonesha viwango vya ugonjwa wa kisukari viliongezeka kwa asilimia 9, huku asilimia 27 kwa msukumo wa juu wa damu," alisema Dk. Rwehimbiza.

Alisema ongezeko hilo limetokana na kuongezeka kwa utandawazi, ukuaji wa miji, kutofanya mazoezi ya mwili, ulaji usiofaa, utumiaji wa tumbaku pamoja na unywaji wa pombe kupita kiasi.

Aidha, alisema Tanzania ilianza kujihususha na magonjwa yasiyokuambukiza kuanzia mwaka 2009 hadi 2015, kwa kuandaa mpango mkakati na mpango kazi ambao ulihusisha utekelezaji wa mpango wa taifa wa kisukari kwa kushirikiana na chama cha wagonjwa wa kisukari nchini.  

"Hadi sasa utekelezaji wa mpango wa taifa wa kuanzisha  kliniki za magonjwa yasiyoambukiza umefikia asilimia 75 katika hospitali za mikoana wilaya na vituo vya afya,". Nakuongeza kuwa asilimia 75 ya elimu zinazotolewa na watoa huduma wa afya katika hospitali za mikoa, wilaya na vituo vya Afya.

Anaongeza kuwa, shirika la afya duniani WHO, liliandaa mpango mkakati ambao ulidhamiria kupunguza viwango vya sasa vya vifo vitokanavyo na magonjwa hayo kwa asilimia 25 ifikapo mwaka 2025 na kupendekeza mapendekezo ya hiari lengo ikiwa kufanikiwa kwa mkakati huo.
Kaimu Mkurugenzi Magonjwa Yasiyoambukiza wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Auson Rwehimbiza (kulia), akimuelekeza jambo Ofisa Habari wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Catheline Sungura wakati wa semina hiyo.
Ofisa Habari wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Catheline Sungura (kushoto), akielekeza jambo kwenye semina hiyo.
Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa kwenye semina hiyo.

Semina ikiendelea.

George Nganda afariki dunia!


George Nganda (38) mkazi na mzaliwa wa Kinondoni B Mtaa wa Isere alifariki dunia juzi usiku kuamkia jana baada ya kuugua mapafu. Akiongea na mtandao huu Bw Ivan Minja ratibu wa Kundi la wakazi na waliokuwa wakazi wa Kinondoni ameeleza kusikitishwa na kifo cha ghafla cha kijana mwenzao ambaye wamekuwa wote katika mitaaa ya Kinondoni, Bw Minja alisema "Kama jumuiya ya wana Kinondoni tunatoa pole nyingi kwa wafiwa nikimaanisha familia ya marehemu lakini pia pole ziende kwa wanachama wote wa Kundi la Kinondoni katika  mitandao ya Facebook na Telegram. aliendelea kuesma "George alikuwa rafiki yetu na tutamkosa sana baada ya kututoka. aliongeza "Kama jumuiya tumekuwa tukihimizana kuchanga pesa kidogo ili tumzike mwenzetu aliyetangulia mbele za haki na kwa kweli michango inaenda vizuri sana, labda nichukue fursa hii kuwapongeza wanachama wote ambao wametoa michango na miwahimize ambao hawajatoa watoe ili pesa hizo zisaidie shughuli za msiba na hatimaye mazishi.

Marehemu George Nganda ambaye hakuacha mke wala mtoto atazikwa kesho saa kumi katika makaburi ya Mwembe jini

Fastjet yafadhili ziara ya waandishi wa habari wa Tanzania nchini Zimbabwe


IMG_2835
Pichani ni Mhudumu wa Mapango ya Chinhoyi Cephas Sithole akitoa maelezo kwa timu ya waandishi wa habari waliombatana na wadau wa utalii kutoka nchini Afrika Kusini kwenye ziara hiyo ya kutembelea vivutio vya utalii nchini Zimbabwe katika mapango Chinhoyi.(Picha zote na Zainul Mzige).

Waandishi wa habari kutoka vyombo 5 vya habari vya magazeti ya Tanzania ikiwemo mtandao wa habari wa modewjiblog ambao ni Justin Damiana (The African), Frank Aman (The Guardian), Zainul Mzige (modewjiblog), Mariam Said (Daily News) pamoja na Timothy Kitundu (East Africa Business Week) walipata mwaliko kutoka Mamlaka ya Utalii ya Zimbabwe (ZTA) kufanya utalii katika mapango ya Chinhoyi, Ziwa Kariba, Shamba la ufagaji wa Mamba, Hifadhi ya Taifa ya Kariba, Bandari ya Zambezi pamoja na ukuta wa bwawa la Kariba unaotengenisha nchi ya Zambia na Zimbabwe.
Safari ya kuelekea nchini Zimbabwe ilidhaminiwa na Shirika la usafiri wa Anga wenye gharama nafuu Fastjet Tanzania ikiwa ni moja ya mipango yao ya kuimarisha safari zake za kutoka Dar es Salaam-Lusaka na Harare.
Safari hiyo ilikuwa maalum kwa ajili kuhudhuria maonyesho ya naneya Kimataifa ya Utalii Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) ambayo yameanza kurindima jijini Harare katika ukumbi wa Harare International Conference Centre (HICC).
IMG_2873
Mungoza watalii katika mapango ya Chinhoyi katika mkoa wa Chinhoyi nchini Zimbabwe, Aleck Makumire akitoa maelezo wa timu ya waandishi wa habari kabla ya kushuka kwenye mapango hayo wakati wa ziara maalum ya kutembelea vivutio vya Utalii nchini humo.
IMG_2896
Mungoza watalii katika mapango ya Chinhoyi katika mkoa wa Chinhoyi nchini Zimbabwe, Aleck Makumire akiwa ndani ya mapango ya Chinhoyi akitoa maelezo kwa waandishi wa habari wa Tanzania katika ziara yao ya kutembelea vivutio vya utalii nchini humo.
IMG_2921
Waandishi wa habari kutoka Tanzania waliosafirishwa na Shirika la ndege lenye gharama nafuu nchini Fastjet kuhudhuria maonyesho ya Kimataifa ya Utalii ya Shanganai yanayoendelea nchini Zimbabwe. Kutoka kushoto ni Timothy Kitundu (East Africa Business Week), Mariam Said (Daily News) pamoja na Justin Damiana (The African) wakiwa wameketi kwenye mapango ya Chinhoyi huku wakibadilishana mawazo na wadau wa utalii kutoka Afrika Kusini.
IMG_2933
Wakirejea kutoka kwenye mapango hayo ambayo chini yana maji ambayo hayatembei wala kukauka. (pichani kwa chini yakionekana kuwa na rangi ya bluu lakini ukichota ni meupe).
IMG_2943
Mwandishi wa habari Timothy Kitundu (East Africa Business Week) akitoka kudhuru mapango hayo wakati wa ziara ya kutembelea vivutio vya utalii.
IMG_2951
Rumbidzai Mudzengerere wa Mamlaka ya Utalii ya Zimbabwe (ZTA) akifurahia ukodak wa kamre ya modewjiblog akitokea ndani ya mapango ya Chinhoyi. Kulia ni Mwambata wa Waziri wa Utalii anayehusika na masuala ya uhamiaji kwa Afrika nchini Zimbabwe, Sherry Sibanda.
IMG_2956
Picha ya pamoja na wenyeji wetu.
IMG_3052
Ziara ya waandishi kutembelea kanisa la Mtakatifu Barbara.
This delightful little round church situated above Kariba town on the hill known as Kariba Heights, was built by workers and engineers employed by Impresit, the Italian company contracted to build the Kariba dam wall. The church is dedicated to St Barbara, who is the patron saint of engineers/construction workers.
On the outside walls of the church is a dedication in Latin to the memory of the construction workers killed during the building of Kariba Dam and a plaque with the names of those who lost their lives is found inside. The church has beautiful stained glass windows and an open-air design which is perfectly suited to the hot climate of Kariba. A bell tower at the back of the church still contains the original bell constructed by hand by Italian workers at the time and hoisted into place with a crane.
Read the detailed story about the church bell of Santa Barbara at this link: The Bell of Santa Barbara Church: A Modern Legend in the Making
IMG_3086
Picha ya kumbukumbu nje ya kanisa hilo.
IMG_3096
IMG_3102
Kulia ni Meneja mwendeshaji wa mtandao wa habari wa modewjiblog, Zainul Mzige akiwa ameambatana na waandishi wenzake kwenye ziara hiyo.
IMG_3115
Sehemu ya muonekano wa Ziwa Kariba kwa juu zinapopaki boti za utalii za watu binafsi na makampuni.
IMG_3151
Kutoka kushoto ni Timothy Kitundu, Mariam Said na Justin Damian wakipata ukodak wakati wa ziara hiyo ya Kariba.
IMG_3179
Muonekano wa Ziwa Kariba.
IMG_3186
Muonekano wa ukuta wa bwawa la Kariba unaotengenisha nchi ya Zambia na Zimbabwe.
IMG_3192
Meneja mwendeshaji wa mtandao wa habari wa modewjiblog, Zainul Mzige akitazama ukingo wa ukuta huo wakati wa ziara ya Kariba nchini Zimbabwe.
IMG_3249
Mkurugenzi Mtendaji wa Going Places Tours & Travel ya Zambia, Rachel Ward akipozi na Mwambata wa Waziri wa Utalii anayehusika na masuala ya uhamiaji kwa Afrika nchini Zimbabwe, Sherry Sibanda kwenye meli kubwa ya kitalii inayotumika kutembeza watalii ambayo inalaza zaidi ya watu 50 huku ikiwa na sehemu ya ukumbi wa burudani na wakati mwingine hukodiwa kama ukumbi wa harusi ndani ya maji pamoja na baadhi ya vyumba maalum kwa wanandoa wanaoenda mapumzikoni (Honey moon).
IMG_3327
Sherry Sibanda na Captain wa muda Zainul Mzige wakipata ukodak ndani ya meli hiyo.
IMG_3329
Captain wa muda Frank Aman akipozi kwa ukodak.
IMG_3332
Captain wa muda Timothy Kitundu ndani ya meli.
IMG_3339
Muonekano wa Meli hiyo.
IMG_3407
Usalama Kwanza: Mariam Said (Daily News) akivaa boya kabla ya kuanza safari ya kuzunguka ziwa Kariba na kulia ni Victoria Siphiwe Mamvura Gava akisaidiwa kuvaa boya na Nahodha ya boti hiyo.
IMG_3430
Kutoka kushoto ni Victoria Siphiwe Mamvura Gava, Cherry Sibanda na Mariam Said wakiwa wamepumzika huku wakipitia baadhi ya vipeperusha vya boti za kitalii zinazokodishwa kwa ajili ya kupumzika katika ziwa la Kariba.
IMG_3465
Kundi jingine likiwa kwenye ziara ya ziwa Kariba likiongozwa na Rumbidzai Mudzengerere wa Mamlaka ya Utalii ya Zimbabwe (ZTA).
IMG_3497
Kituo cha mafuta katika Bandari ya Marine Land kikiwa ndani ya Ziwa Kariba.
IMG_3520
IMG_3571
Boti ya Matusadona inayokodishwa kwa watalii ambapo kila kichwa ni $5000 kwa usiku mmoja ambayo ina uwezo wa kubeba watu saba pamoja na mpishi maalumu kwa ajili ya kuwapikia chakula.
IMG_3586
IMG_3637
Viboko ndani ya Ziwa Kariba.
IMG_3650
Wanahabri wakirejea baada ya ziara ya kuzunguka Ziwa Kariba.
IMG_3739
Timu ya waandishi wa habari kutoka Tanzania wakipiga picha katika shamba la Mamba la Padenga ambalo ni shamba kubwa la ufugaji wa Mamba kuliko yote kusini mwa Afrika.
IMG_3730
Baadhi ya Mamba wakiwa mapumziko ndani ya shamba hilo.
IMG_3741
Mmoja wa Mamba akiwa ametega Nzi wajae ndani ya mdomo wake.

Na Modewjiblog team, Harare