mkalamatukio

KAMPUNI YA SIMU YA TIGO YATOA DOLA ZA MAREKANI 150,000 KWA HOSPITALI YA CCBRT KUSAIDIA WATOTO WENYE MIGUU ILIYOPINDA


 Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez  (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa hafla fupi ya kutiliana saini mkataba wa kusisaidia Hospitali hiyo. Kutoka kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT, Erwin Telemans na Daktari Bingwa wa Mifupa wa Hospitali hiyo, Prosper Alute. 

HOSPITALI ya CCBRT, imepokea dola 150,000 (zaidi ya sh. mil. 320) kutoka kwa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo kwa ajili ya kugharamia matibabu ya watototo wanaozaliwa na ulemavu wa nyayo zilizopinda kwa miaka mitatu ijayo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez alisema hiyo si mara ya kwanza kwa kampuni hiyo kugharamia matibabu ya walewavu kwani miaka mitatu iliyopita pia waligharamia matibabu ya watoto wenye ulemavu wa midomo.

"Tuna amini watoto wenye ulemavu wa unyayo uliopinda watapatiwa matibabu mapema, hivyo tunaomba wazazi wenye watoto wao wanaozaliwa na ulemavu huo kujitokeza CCBRT kupatiwa matibabu kwani ni bure na kwa mwaka tunatoa dola 500," alisema Gutierrez.

Kwa upande wa Daktari wa Mifupa wa hospitali hiyo, Prosper Alute akizungumzia ugonjwa huo, alisema unasababishwa na kurithi kutoka kwa wazazi au ndugu na kunywa pombe kupindukia au kutumia dawa zenye viambata kali.

Alisema asilimia 50 ya watoto wanaozaliwa hupata ugonjwa huo kwa miguu yote ambapo tangu kuingia kwa mwaka huu hadi Aprili, watoto 117 wamegundulika kuwa na ugonjwa huo ambao ni sawa na wastani wa watoto 10 kwa wiki.

Alisema ugonjwa huo usipotibiwa kwa haraka unaweza kumsababishia mtoto kutembea kwa shida na wakati mwingine kutotembea kabisa.

Kwa upande wa Joyce Mosha, Mkazi wa Mwenge,  ni mmoja wa wazazi ambaye mtoto wake, Gidion ana miezi miwili alikutwa na tatizo hilo na kufanyiwa upasuaji, alisema mara baada ya kujifungua madaktari waligundua mtoto wake kuwa na tatizo hilo, hivyo waliamua aanze kupatiwa matibabu.

"Namshukuru Mungu alifanyiwa upasuaji mdogo na hivi sasa anaendelea vizuri, alipogunduliwa ana tatizo hilo kwanza walimfunga plasta ngumu (POP) kwa wiki tano na kisha kumfanyia upasuaji mdogo wa mfupa na kumpa viatu maalumu vya kuvaa na vingine huwa anavaa usiku tu wakati wa kulala," alitoa ushuhuda Joyce.
 Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT, Erwin Telemans akizungumza katika hafla hiyo.
 Meneja  Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (wa pili kushoto), akibadilishana hati na Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT baada ya kutiliana saini mkataba wa kusaidi matibabu ya ulemavu wa miguu Dar es Salaam jana. Kushoto ni Daktari Bingwa wa Mifupa wa Hospitali hiyo, Prosper Alute na Meneja Uwajibikaji kwa Jamii, Woinde Shisael.
 Meneja wa Mawasiliano wa Tigo, John Wanyanja (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

 Picha mbalimbali zikionesha miguu iliyopinda.
 Wanahabari wakiwa kwenye hafla hiyo.
Joyce Moshi akiwa amembeba mtoto wake Gedion ambaye anatibiwa katika Hospitali hiyo kutokana na miguu yake kupinda ambapo sasa anaendelea vizuri.

Wapinzani wapinga muhula wa 3 wa Kagame



Rais Paul Kagame wa Rwanda
Zaidi ya raia milioni 7.3 wametia sahihi ombi la kuunga mkono mabadiliko hayo. Nchi hiyo ina jumla ya watu 11.3m.
Wakosoaji wanasema wengi waliounga mkono ombi hilo ni wafungwa ambao hawaruhusiwi hata kupiga kura.
Bwana Kagame ameliongoza taifa hilo tangu mwisho wa mauaji ya kimbari mwaka 1994.
Taifa jirani la Burundi limekumbwa na mgogoro tangu mwezi Aprili wakati rais Pierre Nkurunziza alipotangaza hamu yake ya kuwania muhula mwengine wa tatu.
source BBCswahili

BABA YAKE MSANII STEVE NYERERE AFARIKI!


 Marehemu Francis Festus Mengele, enzi za uhai wake.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Francis Festus Mengele.
 Shangazi wa Msanii, Steve Nyerere, Grace Mengele (katikati), akiwa na wadogo zake Steve Nyerere wakati akiwasili makaburi ya Kinondoni kwa mazishi ya mpendwa wao, Francis Mengele.
 Watoto wa marehemu na dada zake wakiwa kwenye ibada ya maziko makaburi ya Kinondoni.
 Ibada ya maziko ikiendelea.
 Hali ilivyokuwa wakati wa mazishi.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu Francis Mengele 
likishushwa kaburini.
  Jeneza lenye mwili wa marehemu Francis Mengele 
likishushwa kaburini.
 Wasanii mbalimbali wakiwa kwenye mazishi hayo.
 Ni huzuni tupu.
 DC Makonda akiwa udongo kwenye kaburi la Francis Mengele wakati wa mazishi.
 Kaburi likijengwe baada ya kuwekwa mwili wa marehemu kaburini.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa marehemu Francis Mengele.
 Waombolezaji wakiwasili makaburi ya Kinondoni tayari 
kwa mazishi.
 Hali ilivyokuwa makaburini.
 Hali ilivyokuwa makaburini.

Wasanii  mbalimbali wakiwa kwenye maziko hayo.

Na Dotto Mwaibale


WASANII mbalimbali wa filamu na bongo fleva  wamejitokeza kwa wingi katika mazishi ya baba ya msanii mwenzao Steve Mengele 'Steve Nyerere, aliyofanyika juzi makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Msanii Jacob Stephen JB ni miongoni mwa wasanii waliohudhuria mazishi ya marehemu Francis Mengele baba yake na msanii huyo aliyefariki wiki iliyopita kutokana na maradhi ya mapafu.

Wasanii wengine waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na Micky, Vicent Kigosi 'Ray' Elizabeth Michael 'Lulu' Chuchu Hans, Kajala Masanja 'Kajala' , Mtunzi na muongozaji wa filamu Myovela Mswaisa na wengine wengi.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda aliyeongoza mazishi hayo alisema kifo cha Mengele ni pigo kubwa katika wilaya hiyo ya Kinondoni na familia kwa ujumla.

"Mengele alikuwa na mchango mkubwa katika wilaya yetu ya Kinondoni katika kulipa kodi kutokana na biashara zake alizokuwa akizifanya na wingi huu wa watu waliojitokeza katika mazishi yake inaonesha jinsi alivyokuwa akishirikiana na wenzake hasa waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Kimara alikokuwa akisali" alisema Makonda.


Makonda alitumia fursa hiyo kuiomba Manispaa ya Kinondoni ndani ya miezi mitatu kuhakikisha inajenga choo katika makaburi hayo ya Kinondoni kwani ni aibu kwa eneo hilo kukosa choo hivyo kuwafanya wananchi wanaofika kwa ajili ya maziko kukosa huduma ya choo.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com
-0712-727062)

Prof Mark Mwandosya asaka wadhamini Kilimanjaro


Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama akisalimiana na Waziri wa nchi,Ofisi ya Rais(Kazi Maalum) Prof,Mark Mwandosya mara baada ya kufika ukumbi wa mikutano wa mkoa wa Kilimanjaro wakati akiwa njiani kutafuta wadhamini.
Prof,Mwandosya akiteta jambo na RC Gama mara baada ya kukutana.
Prof,Mark Mwandosya akisalimiana na Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi ,Angela Kairuki walipokutana katika ukumbi wa mikutano wa mkoa wa Kilimanjaro.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro akimpatia kipaza sauti Prof Mwandosya asalimie wajumbe waliokuwa katika ukumbi huo.
Profesa Mwandosya akizungumza katika ukumbi huo.
Prof Mwandosya akitoka katika ukumbi wa mikutano wa mkoa wa Kilimanjaromara bada ya kusalimia.
Prof, Mwandosya akiagana na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama mara baada ya kusalimia .
Prof,Mark Mwandosya akiondoka ukumbini hapo kuendelea na safari ya kusaka wadhamini mkoani Arusha.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kaskazini.

Pamoja na kukosa tunzo ya Kili ki mizengwe Christian Bela apagawisha Tabora!

Christian Bella akijimwaga jukwaani.
Masaa machache baada ya kukosa kitatanishi tunzo ya wimbo bora wa mwaka katika Kili Music Awards Christian Bela (King of melodies) alipagawisha wapenzi wa muziki mjini Tabora alipoporomosha bonge la show akiwa na kundi zima la Malaika Band. Christian Bela alitarajiwa na  wadau wa muziki nchini kuwa angebeba tunzo hiyo bila ushindani mkubwa kutokana na wimbo wake wa Nani kama mama ambao aliomshirikisha Ommy Dimpoz kutamba sana katika vituo vyote vya redio na Runinga hapa nchini, lakini kama kawaida ya tunzo hizo zinazosimamiwa na BASATA na kudhaminiwa na kampuni ya utengenezaji bia ya Tanzania TBL zimekuwa zikilalamikiwa kila mwaka huku waanadaaji wakioneka kuweka pamba mbichi masikioni. Tunzo hiyo ya wimbo bora wa mwaka ilienda kwa wimbo wa Mwana wa msanii Ali Kiba. Onesho hilo lilifanyika katika viwanja vya Bwalo la Polisi Tabora.
Bella akifanya yake jukwaani.

Mashabiki wa Malaika Band wakpozi
Hapo sasa!


Baadhi ya mashabiki wakijmwaga!


Music Producer Dula K kulia na msanii Masha Kay kushoto wakiwa na mdau.

Wacha wee Benny Ngwasuma akijiachia



Papaa Allex Ntonge mwaya mwaya!

Picha na habari na Mkala Fundikira TBN CENTRAL ZONE