mkalamatukio

HARAKATI ZA KUANZISHWA KWA KARIAKOO FAMILY FOUNDATION (KFF)

 Mwenyekiti wa Kariakoo Family Foundation (KFF) Mohamed Bhinda akiongoza kikao cha Kamati ya Utendaji katika kuandaa rasimu ya katiba ya chama hicho kinachotarajiwa kusajiliwa  hivi karibuni kama taasisi isiyo ya kiserikali kwa nia ya kukutanisha upya wadau wote waliozaliwa, walioishi na wenye asili ya Kariakoo katika Wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam. Mkutano huu umefanyika leo jioni Kinondoni Studio. Kulia kwa Bhinda ni katibu wa chama hicho Senpai Wahid
 Mtunza hazina wa KFF Yahaya Sameja akielezea namna chama hicho cha jamii ya wana Kariakoo kitavyoweza kujiendesha kwa njia za ada, michango na misaada ya wafadhili katika kuendeleza wanachama, ikiwa ni pamoja na kusaidiana katika shida na raha. Kushoto ni Mwenyekiti wa KFF Mohamed Bhinda na kati ni Makamu Mwenyekiti Tatu Lumelezi
 Wana KFF wakipata mlo wa mchana wakati wa mapumziko
Jopo la kamati ya utendaji ya KFF baada ya mkutano wao leo

Ijue historia ya Linda

NI MENGI AMEZUNGUMUZA AMBAYO MIMI NA WEWE HATUKUYAJUA
Kesho Jumatatu katika kipindi cha huyu na yule cha mahojiano na mwanamitindo mbunifu wa LB kutoka Atlanta, Georgia atakapoelezea historia yake yenye milima na mabonde historia ya maisha yake yenye huzuni na furaha wakati mwingine Linda akitokwa na machozi kwa kukumbuka maisha aliyopitia. Je Mume wake Mali walijuana nae wapi? na mengine mengi kuhusu maisha yake ikiwemo kampuni yake ya LB na malengo yake ya kupeperusha bendera ya Tanzania anga za kimataifa. USIKOSE mahojiano yaliyofanywa na mwakilishi wa Vijimambo na kwanza production Michigan Alpha Igogo ambae alitaka kujua undani wa maisha ya mwanadada Linda

Alpha Igogo akifanya mahojiano na Linda jijini Atlanta
Maswali yalikua moto Linda akipumua na kumkumbatia Alpha Igogo baada ya mahojiano kufikia mwisho

Balozi wa IMETOSHA FOUNDATION Henry Mdimu atoa wito kwa vyombo vya habari na jamii!


Balozi Henry Mdimu akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za gazeti la Mwananchi mjini Mwanza.

Henry Mdimu ametoa wito kwa vyombo vya habari na jamii nchini kulichukua suala la ukatili na mauaji kwa watu wenye ualbino kama lao ili kuiondoa nchi yetu katika aibu hii. Aliyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za gazeti la Mwananchi ambao ni wadhamini wa habari wa ujio wa kamati ya Imetosha katika kanda ya ziwa.
Kutoka kushoto ni Salome Gregory, Henry Mdimu Mgaya, Issaya Mwakilasa na Zaytun Biboze.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Balozi Mdimu

Imetosha
Kila sauti inasikika.
PIGA KELELE uunge mkono haki ya KUISHI

Ndugu waandishi wa habari, Mwakilishi wa Tanzania Bloggers Network, mabibi na mabwana…..
Tuko hapa kuueleza Ulimwengu kupitia vyombo mbali mbali vya habari juu ya harakati yetu ya IMETOSHA. Harakati hii hii  imeanzishwa na mimi mwenyewe, Henry Mdimu, mwanahabari mwenzenu ambaye nimeamua kwa moyo mmoja kuwa Balozi wa kujitolea wa harakati za kukomesha mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu  wa ngozi, maarufu kwa jina la Albino.
Mimi na ujumbe wangu tumekuja Mwanza kutambulisha harakati za IMETOSHA na ikiwa sehemu ya kuandaa shughuli zitakazofanyika kanda ya Ziwa ikiwa ni sehemu ya kupambana na mauaji na unyanyasaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Mwezi ujao ujumbe wa IMETOSHA utakuja na kuweka kambi ya kudumu Mwanza itakayozunguka kanda ya Ziwa na kutembelea nyumba kwa nyumba zenye wahanga wa matukio ya mauaji na kutoa elimu kwa jamii kuwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi hayasababishi utajiri.
Pamoja na shughuli tutakazofanya tukiwa Kanda ya Ziwa mwezi wa tano ni pamoja na maetmbezi ya hisani, kutakua na mpira kati ya Simba na Yanga ambapo IMETOSH itavalisha wachezaji Thisrts zake ikiwa ni sehemu ya kutangaza harakati zetu.
Pia tutakua na tamasha litakaloshirikisha wasanii mbalimbali watakaotumbuiza nyimbo mbamimbali zitakazokua na ujumbe wa kukemea na kupinga mauaji na manyanyaso dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Nimeamua kufanya hivi baada ya kushuhudia ndugu zangu wakiteseka kwa muda mrefu. Awali nilishindwa kuanzisha harakati hizi nikiamini kuna vyombo vinavyohusika na utetezi wa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Hrakati hizi zimeanza baada ya kuona kadri muda unavyokwenda matukio yamezidi kuongezeka na hali kuwa mbaya. Nashuhudia ndugu zangu wakinyanyaswa, wakibezwa mtaanai na hata kudhihakiwa huku baadhi ya wanaoshuhudia haya wakicheka tu.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na vyombo vya habari vilimkariri Rasi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania muheshimwa Jakaya Kikwete akisema kesi mbili za mauaji ya watu wenye ulemavuwa ngozi zililipotiwa kwa mwaka 2012 na 2013.
Taarifa hizo ziliongeza kuwa kti ya mwaka 2006 na 2015, watuhumiwa 139 wameshikiliwa na kesi 35 zimeandikishwa. Watuhumiwa 73 waliachiwa huru na wengine 15 wamekutwa na makosa.
Hivyo nimeamua niweke jitihada zangu binafsi niisaidie Serikali yangu katika kuondoa doa hili linaloichafua Nchi  yetu yenye sifa ya Amani duninia nzima. Hivyo nawaomba Watanzania wenzangu mniunge mkono tukishirikiana na Serikali ili mauaji haya yakome.
Kutokana na ushawishi nilionao kama Mwandishi, Mtangazaji wa redio na Blogger naamini nitaleta mabadiliko makubwa katika kuhakikisha haki ya kusihi kwa ndugu zangu inaheshimiwa na kubaki historia. Salamu zangu ziwafikie wanyanyasaji, wauaji na wenye kufanya dhihaka kwa watu wenye ulemavu wa ngozi kuwa IMETOSHA.
Uchunguzi wangu wa awali umebaini ukosefu wa elimu juu ya watu wenye ulemavu wa ngozi hupelekea tatizo hili kukua na hatimaye kuuana kw aimani za kishirikina. Hivyo basi, silaha ya Elimu ni sehemu kubwa ya haraki hizi.
Mimi pamoja na mafariki zangu wanaoniunga mkono tutakwenda Kanda ya Ziwa kutoa Elimu kabla tatizo hili halijaenea Nchi nzima. Swali moja tujiulize kwa nini Kanda ya Ziwa? Tutatoa Elimu kwa njia ya ushauri nasaha, pia wanamuziki  sanaa
Nina mpango wa kwenda kanda ya Ziwa kuhangaika na hili mpaka nione mwisho wake. Na ni rahisi kumaliza hili tatizo kabla halijaenea nchi nzima. Maana Walemavu wa ngozi wako nchi nzima lakini jiulize kwa nini Kanda ya Ziwa tu?
Mimi pamoja na rafiki zangu hawa, tunatoka kuelekea huko kutoa elimu kwa njia ya sanaa, na washauri nasaha. Pia tutakua na team ya wanamuziki wanaoandaa nyimbo mbali mbali za kutoa mafunzo ya kutokomeza ukatili huu.
Wasanii hao ni paoma na Jhikoman, Kassim Mganga, Profesa J, Ray C, Fid Q, Roma Mkatoliki na Dami Msimamo.  Tutaishi na jamii hii kwa muda tukiongea nao kwa lugha yao kwa kutumia wakalimani kwa wsifahamu Kiswahili kuwashawishi waamini hakuna ukweli katika Imani hizo.
Naamini nguvu ya vyombo vya Habari hivyo naomba ushirikaiano wenu katika kuhakikisha tunatokomeza mauaji ya wenzetu ili mwisho wa siku wanunuzi wa viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi wafukuzwe watakaanza kuuliza jinsi ya kufanya mauaji haya.
Harakati za IMETOSHA rasmi zimezinduliwa rasmi tarehe 3/3/2015.
Mungu atubariki.
Ahsanteni
HENRY MDIMU-0715000881 na 0787000880
Balozi wa kujitolea
Harakati za IMETOSHA

SALOME GREGORY 0717367309

Mratibu wa Habari- Harakati za IMETOSHA

Ujumbe mzito wa Imetosha watembelea kituo cha Buhangija mjini Shinyanga!


Ilikua mishale ya saa kumi kamili jioni ujumbe wa harakati za Imetosha ulipowasili katika kituo cha Buhangija cha kulea watoto wenye mahitaji maalumu mjini Shinyanga. Sauti za furaha za watoto zilisikika zikiimba nyimbo za kukaribisha ujumbe wa wana harakati hao ambao wako Mwanza kutambulisha harakati za Imetosha ambazo ni kupambana na kupinga unyanyapaa, ukatili na mauaji kwa watu wenye Ulemavu wa ngozi.

Balozi wa Imetosha Henry Mdimu akinunua mahitaji ya watoto waliopo kituoni hapo kabla ya kufika kituoni hapo.
Huyu ni Irene wa NHIF Shinyanga

Wajumbe wa Imetosha
 Akiongea na watoto kituoni hapo Mwenyekiti wa harakati za Imetosha Masoud Ali (Kipanya) alisema Imetosha inatambua umuhimu wa haki ya kuishi kwa kila binadamu ndio maana Imetosha imeanzisha harakati za kutokomeza mauaji na unyanyapaa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.  “Tunatambua hapa kati yenu kuna vipaji vya aina mbalimbali hivyo pamoja na kupambana na harakati za kupinga na kutokomeza mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi tupo hapa kuwatia moyo kuwa mna uwezo mkubwa ndani yenu hivyo msijidharau” alisema Masoud.

Kipanya akimuimbisha mtoto wa kituoni hapo
Mwl Peter Alali Francis akisisitiza jambo wakati akiongea na ujumbe wa Imetosha

 Alisema“Pamoja na uhaba wa mabweni kituo kinakabiliwa na uhaba wa chakula. Muda mwingine watoto hawa hushindia mlo mmoja. Chakula mlichofikisha leo hapa kitatusogeza maana tulikua tumeishiwa chakula kabisa” alisema Francis. Ujumbe huo wa Imetosha uliwasilisha kambini hapo unga kilo 50, mchele kilo 50, chumvi kilo 5 na mafuta ya kupikia lita 10. 

Mwalimu Mkuu wa Kituo hicho Peter Ajali Francis alishukuru ujio wa wanaharakati wa Imetosha kituoni hapo na kusema kituo hicho kilianzishwa mwaka 1960 kikiwa chini ya Kanisa katoliki.
Kituo hicho kilikua maalumu kwa ajli ya watoto wasiiona na viziwi lakini kutokana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi kuongezeka mwaka 2006 kituo hicho kilianza kupokea watoto wenye ulemavu wa ngozi kutoka sehemu mbalimbali toka kanda ya Ziwa. Kituo kina jumla ya watoto 388 kati ta hao 284 wana ulemavu wa ngozi. Kituo hicho kinakabiliwa na uhaba wa mabweni ambapo chumba chenye uwezo wa kuchukua watoto 50 kinachukua watoto zaidi ya 100 na chenye uwezo wa kuchukua watoto 40 kinachukua watoto zaidi ya 80.


 Zaytun Biboze akiwa amebeba mmoja wa watototo wanaoishi katika ktuo hicho



Masoud Kipanya na Jhikoman wakiwaimbisha watototo wimbo waupenda wa Clap your hands!
Isaya Mwakilasa aka Wakuvwanga akiwachekesha watoto kiuoni Buhangija, Shinyanga


Magunia haya ya unga, mafuta na mchele ndio msaada wa chakula ambao Imetosha ilitoa kwa kituo hicho


Katibu wa Imetosha amabaye ki taaluma ni mwandishi wa habari akimhoji mwalimu Francis Ajali
Wanaharakati wa Imetosha wamepanga kurudi tena mjini Shinyanga mwezi Mei na kukifanya kituo hicho kuwa ngome ya kuanzishia mapambano dhidi ya unyanyapaa, ukatili na mauaji kwa albino.
Picha na Mkala Fundikira habari na Salome Gregoy/ Mkala Fundikira 

EPUSHA AJALI OKOA MAISHA!


Ujumbe wa Imetosha Foundation wawasili Mwanza!


Salome Gregory akifuatiwa na Balozi Mdimu na Issaya Mwakilasa wakiteremka toka katika ndege iliyowasafirisha toka Dar mpaka Mwanza.

Picha ya kumbukumbu toka kushoto ni Issaya Wakuvwanga, Zaytuni Biboze, Salome Gregory, Henry Mdimu na Mkala Fundikira, Mwanza airport.
Ujumbe wa taasisi ya Imetosha inayojishughulisha na utoaji elimu juu ya kumaliza unyanyapaa,  ukatili na mauaji kwa watu wenye ualbino nchini uliwasili jijini Mwanza leo hii saa 2 asubuhi kwa ziara ya siku 3 ambapo kati siku hizo tatu ujumbe huo utakutana na viongozi wa ki serikali na usalama wa baadhi ya mikoa na wilaya za kanda ya ziwa ikiwemo Mwanza na Shinyanga. Lengo la mikutano hiyo ni kamati kujitambulisha kwa viongozi hao na kuwaeleza nini Imetosha inatarajia kufanya katika kanda hii mwezi ujao ambako pamekuwa na matukio mengi ya ukatili na mauaji kwa watu wenye ualbino nchini Tanzania. 

 Vile vile kamati itakuwa na siku moja ambapo itatembelea vyombo ya habari vya jijini hapa kabla ya kurejea Dar es Salaam.

Habari na picha na Mkala Fundikira wa Mkalamatukio/keronyingi blog

Kamati ya imetosha yatuma ujumbe mzito kanda ya ziwa!


Balozi Henry Mdimu akiongea na vyombo vya habari
Taasisi isiyo ya ki serikali ya Imetosha Foundation inayopinga unyanyapaa, ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino kwa njia ya elimu, inatarajia kutuma ujumbe mzito kanda ya ziwa hapo kesho kwa maandalizi ya ujio wa timu nzima ya taasisi hiyo iliyojikita kwenye kubadilisha mtazamo (mind set) wa watu juu ya janga hili. Ujumbe huo utaongozwa na mwenyekiti wa taasisi hiyo Bw Masoud Kipanya, Balozi Henry Mdimu Mgaya na katibu Salome Gregory,wajumbe watakaongozana na viongozi hao ni pamoja na Mkala Fundikira, Isaya Mwakilasa (wakuvwanga aka Baba Andunje) Zaytun Biboze, Kelvina John na msanii wa muziki wa reggae Jhikoman Manyika.

Mwenyekiti Masoud Kipanya akiongea katika kilele cha matembezi ya hamasa yaliyofanyika jijini Dar
Dhumuni la safari hiyo itakayoupeleka ujumbe huo mpaka mkoani Shinyanga ni kwenda kujitambulisha kwa viongozi wa serikali na usalama wa mikoa na za kanda hiyo iliyoathiriwa sana na janga la ukatili na mauaji ya watu wenye ualbino. Taasisi ya Imetosha imepanga kwenda kanda ya ziwa baadaye mwezi ujao ambapo timu itaenda maeneo yaliyoathiriwa na kutoa elimu kwa wakazi wa maeneo hayo kuwa si kweli kwamba ukiwa na kiungo cha mtu mwenye ualbino utapata mafanikio, elimu hizo zitatolewa kwa njia ya filamu mbali mbali, michezo ya kuigiza na matamasha ya muziki.
Hoteli ya Green Palm utakapofikia ujumbe wa Imetosha Foundation jijini Mwanza aka the Rock City.
Ujumbe huu ukiwa mjini Mwanza utakuwa chini ya udhamini wa hoteli ya Green Palm iliypo maeneo ya Bwiru, vile vile kampuni ya Mwananchi communication ltd (MCL) inayozalisha gazeti bora la Mwananchi na mengineyo itachapisha habari zote kuhusiana na msafara huo wa Imetosha kanda ya ziwa. Meneja wa hotel 

Isaya Mwakilasa wa (Orijino komedi) Henry Mdimu na familia ya Isaya aka Wakuvwanga
ya Green Palm Bw Juma Herman ameuambia mtandao huu kuwa "imekuwa rahisi kwetu (Green Palm Hotel) kudhamini makazi na usafiri kwa taasisi hiyo kwa kuwa inachofanya ni kitu chema basi nasi tumeona ni vema tuwatie nguvu kwa kuwapatia malazi na usafiri wa ndani kwa kipindi chote watakachokuwa jijini Mwanza, kwa kweli sasa imetosha ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino" aliongeza.
Wakiongea na mtandao huu kwa nyakati tofauti Mwenyekiti Masoud Kipanya na Balozi Henry Mdimu walisema  wanashukuru sana kwa kitendo cha Green Palm na Mwananchi communictaion na kuwa ni vya kuigwa na makampuni mengine ili kuiwezesha taasisi hiyo kufikia malengo yake. Taasisi ya Imetosha haina vyanzo vya fedha hivyo kutegemea wahisani kama Green Palm Hotel na Mwananchi communication.
Maktaba Baadhi ya wajumbe wa Imetosha wakijiandaa kwenda katika mchezo wa Simba na Yanga