Ujumbe wa Imetosha Foundation wawasili Mwanza!

Ujumbe wa Imetosha Foundation wawasili Mwanza!


Salome Gregory akifuatiwa na Balozi Mdimu na Issaya Mwakilasa wakiteremka toka katika ndege iliyowasafirisha toka Dar mpaka Mwanza.

Picha ya kumbukumbu toka kushoto ni Issaya Wakuvwanga, Zaytuni Biboze, Salome Gregory, Henry Mdimu na Mkala Fundikira, Mwanza airport.
Ujumbe wa taasisi ya Imetosha inayojishughulisha na utoaji elimu juu ya kumaliza unyanyapaa,  ukatili na mauaji kwa watu wenye ualbino nchini uliwasili jijini Mwanza leo hii saa 2 asubuhi kwa ziara ya siku 3 ambapo kati siku hizo tatu ujumbe huo utakutana na viongozi wa ki serikali na usalama wa baadhi ya mikoa na wilaya za kanda ya ziwa ikiwemo Mwanza na Shinyanga. Lengo la mikutano hiyo ni kamati kujitambulisha kwa viongozi hao na kuwaeleza nini Imetosha inatarajia kufanya katika kanda hii mwezi ujao ambako pamekuwa na matukio mengi ya ukatili na mauaji kwa watu wenye ualbino nchini Tanzania. 

 Vile vile kamati itakuwa na siku moja ambapo itatembelea vyombo ya habari vya jijini hapa kabla ya kurejea Dar es Salaam.

Habari na picha na Mkala Fundikira wa Mkalamatukio/keronyingi blog