mkalamatukio

Washiriki wa Miss Dar Indian Ocean wajichua vikali kuelekea kilele cha shindano hilo!

Shamila Yusuf


Tazama picha za washiriki wa shindano la urimbwende la Miss Dar Indian Ocean 2014 wakiwa katika mazoezi ya mwisho kabla ya kilele cha shindano hilo jumamosi hii ya tarehe 7/6/2014 katika viwanja vya Nyumbani Lounge ambako bendi inayoundwa vijana wenye vipaji toka Tanzania house of talent (THT) watatumbuiza shindano hilo. Akiongea na blog hii muandaaji wa shindano hilo Bibi Rahma Yusuf anayeanda kupitia kamuni yake ya Rahmat Entertainments alisema maandalizi yote yapo sawa kinachosubiriwa ni ni siku saa na tarehe tu.  Viingilio ni Tsh 10,000/= viti vya kawaida na Tsh 30,000/= kwa viti maalum(VIP), onesho litaanza mnamo saa 2 za usiku mpaka majogoo. Washiriki hao wapo ya mkufunzi wao Miss Husna
Miss Sophia
Miss Mary Shila 
Joyce James 
Monica Nshimba
Miss Sasha Deogratius
Miss Hasnat Hussien
Janet Geofrey

Miss Getrude Massawe
Miss Mariam Salum
Miss Suzzane SAWAYA
Miss Ayaan Abdul
Miss Camilla John

Miss Dar Indian Ocean patakuwa hapatoshi!

Muandaaji wa Miss Dar Indian Ocean Bibi Rahama Yusuph
Baada ya kufanya shindano la vipaji kwa mafanikio makubwa mnamo tarehe 23/5/2014 ambapo washiriki watano waliiingia fainali, sasa shindano la Miss Dar Indian Ocean litafanyika jumamosi ya tarehe 7/6/2014 katika viwanja vya Nyumbani Lounge, kiaina inaelekea waandaaji wamejipanga vema sana nadau na mashabiki wa tasnia hii wameombwa kujitokeza kwa wingi siku ya tukio ambapo wakali wa THT watatumbuiza hafla hiyo.

Baadhi ya wageni waliohudhuria shindano la vipaji Miss Dar Indian Ocean!

Mfanyabiashara Teef Fundikira akiteta kitu na Mkurugenzi wa kampuni ya Aset Bibi Asha Baraka.
Mdau wa tasnia ya urembo Bi Hawa  Mkamba(kulia) akiwa na rafiki yake.
Kutoka kushoto Asha Baraka, Mkurugenzi wa Lino International inayoandaa shindano la Miss Tanzania na Khadija Kalili muandaaji wa Miss Pwani
Mfanyabiashara Bw Hassan akiwa na muandaaji wa Miss Dar Indian Ocean Bibi Rahma Yusuf.


Shindano la Miss Dar Indian Ocean litafanyika jumamosi ya tarehe 7/06/2014 katika ukumbi wa Chichi Hotel, Kinondoni.
Wadau wa urembo wakifuatilia onesho hilo kwa umakini mkubwa! 
Wazee wa kazi: Hashim Lundenga na Bw Bosco Majaliwa
Mkuu wa itifaki na nidhamu Bw Ephraim Makoye
Toka kushoto Hassan, Hidani Ricco na Boy George(Muandaaji wa zamani wa Miss Kinondoni) 

Wajue top five wa vipaji Miss Dar Indian Ocean!

Shindano la urembo la Miss Dar Indian Ocean likiwa linakaribia, siku ya ijumaa  tarehe 23/5/2014 wapenzi wa tasnia ya urembo jijini Dar na wilaya zake walishuhudia mchuano mkali wa kugombea ushindi wa kipaji katika ukumbi wa Chichi hotel ambapo warembo watano kati ya 15, walifanikiwa kuingia fainali ya shindano hilo la kipaji zitakazofanyika siku ya kumtafuta Miss Dar Indian Ocean ambayo ni Jumamosi ya tarehe 7/6/2014 katika ukumbi huo huo maridhawa wa Chichi hotel. Onesho hilo lilihudhuriwa na kamati ya Miss Tanzania pamoja na Miss Tanzania 2012 Salha Israel, pamoja na wadhamini kama CXC na wengine wengi. Dalili zinaonesha show ya Miss Dar Indian Ocean itakuwa si mchezo kwani kwa onesho dogo tu la kipaji ukumbi na jukwaa vilipambwa vilivyo na kampuni maaurfu ya Vayle Springs. Mtandao huu ulipoongea na muandaaji wa shindano hilo Bibi Rahma Yusuf ambaye anaanda shindano hilo kupitia kampuni yake ya Rahmat Entertainments alisema kwa kujiamini "Hii ni trela tu muvi yenyewe ni tarehe 7June ukikosa show hiyo bora uhame mji" Onesho hilo la vipaji lilidhaminiwa na Chichi hotel.
Kutoka kushoto ni Suzzete Fetrick, Mary Amos, Sasha Deogratius, Camilla John na Getrude Massawe, hawa ndio walioingia fainali za Miss Dar Indian Ocean Talent show.
Judges: Kutoka kushoto ni jaji Hassan, Husna Sajent na Iddi Zonki
Kutoka kushoto ni muandaaji wa Miss Mwanza Bw Dotto, Yusuf Omari aka Boy George, Salha Israel na katibu wa Miss Tanzania Bw Bosco Majaliwa wakifuatilia kwa makini shindano la vipaji.

Picha zaidi za semina ya Redds Miss Tanzania!

Kulia ni wakala wa Redds Miss Njombe
Tunachukua notice
Tom Chilala mwenye shati jeupe na Khadija Kalili kushoto kwake


Hidan Ricco na Ephraim Makoye wa kamati ya Miss Tanzania

Kulia ni wakala wa Miss Singida 
Baadhi ya waandaji mawakala wakifuatilia semina kwa umakini
Muandaaji wa Redds Miss Temeke Bw Kisaka na William Malecela wa Blog ya wananchi.

Semina ya mawakala wa Redds Miss Tanzania yafanyika

Mkurugenzi wa Lino International inayoratibu shindano la Miss Tanzania Bw Hashim Lungenga akisisitiza jambo alipokuwa akifungua semina ya mawakala wa Miss Tanzania 2014.
Semina ya kuwafunda mawakala wa Redds Miss Tanzania 2014 ilifanyika kuanzia jana arehe 25/03/2014 katika Hoteli ya Regency ya jijini Dar es Salaam, semina hiyo ambayo hukutanisha kamati ya Miss Tanzania, mawakala na wadhamini hufanyika kila mwaka baada ya uzinduzi rasmi wa shindano hilo kubwa la urembo nchini. Kampuni ya TBL kupitia kinywaji chake baridi cha Redds Premium cold ndiye mdhamini mkuu wa shindano hilo ambalo mchakato wake huanzia katika vituo, wilaya, mkoa na hatimaye na shindano la Taifa yaani Redds Miss Tanzania
Kutoka kushoto ni katibu wa Miss Tanzania Bw Bosco Majaliwa, Mshauri wa ufundi Bw Ramesh Patel, Hashim Lundenga, Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa na mshindi wa pili wa shindano hilo.


Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa

Kutoka kushoto Bw Bosco Majaliwa, Ramesh Patel na Bw Hashim Lundenga
Wakala wa kituo cha Dar na Awetu wa gazeti la KIU

Baadhi ya mawakala wa Miss Higher Learning

Muandaaji wa Redds Miss Njombe, Miss Sylvia

Kutoka kushoto ni Miss Jacky, Tom Chilala wa star T na Khadija kalili wa Tanzania Daima





Mpigie kura Ally Baucha ashinde Kili Music Awards!

Msani machachari Ally Baucha ambaye kupitia wimbo wake Kelele aliomshirikisha Ally Kiba ameteuliwa kushiriki katika kinyang'anyro cha kugombea tuzo za Msanii anayechipukia ambapo amepewa namba 23 na vile vile amepewa namba 26 katika kugombea tuzo ya msanii bora mtumbuizaji wa kiume. Ili kumpigia kura Baucha fuata maelekezo hapo juu.