mkalamatukio

Mfanyakazi wa SWISSPORT Dar es Salaam afariki ghafla!

Salustian Boniface Clement alizaliwa 07/4/1962 na kufariki 29/11/2013.
Familia ya Salustian inasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wao Bw Salustian Clement kilichotokea ghafla siku ya Ijumaa jijini Dar es Salaam. Taarifa za msiba huu ziwafikie Familia ya Oswald Ndibalema waliopo England na popote pengine walipo, familia ya Lwakatere popote walipo pamoja na ndugu na jamaa wote wa marehemu. Marehemu Salustian ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya SWISSPORT ameacha mke na watoto watatu. Mwili wake unatarajiwa kusafirishwa leo kwenda mjini Bukoba yatakayofanyika kesho mchana mjini hapo.
Habari na picha kwa hisani ya Edgar Oswald
Mwili wa Marehemu ulipokuwa ukisafishwa kwenda Airport.

Hapa ni kanisa Katoliki la Chang'ombe jijini Dar ambapo mwili wa marehemu uliagwa.Mungu ailaze roho yake pema peponi Ameen!

Shabiki wa Ajax ajeruhiwa vibaya baada ya kuanguka toka jukwaani

Watoa huduma ya kwanza wakimhudumia shabiki aliyeanguka akishangilia goli la pili.

Mshabiki wa timu ya Ajax Amsterdam ambaye hakutajwa jina, jana alianguka alipokuwa akishangilia bao la  pili la timu yake dhidi ya Fc Barcelona lililofungwa na Danny Hoesen. Inakadiriwa mtu huyo alianguka toka urefu wa futi 16 alikutwa kalala katika dimbwi la damu
Baadae watu wa huduma ya kwanza toka kwa magari mawili ya Ambulance na helikopta moja walimtibu mtu huyo na kumpeleka hospitali. Ajax ilifanikiwa kuifunga Barcelona katika mchezo huo wa Ubingwa wa Ulaya. Lakini haikufahamika hali ya mshabiki aliyeanguka ilikuwa ikiendeleaje.
Amsterdam Arena ionekanavyo kwa nje.


Tabora Funga mwaka Bash kuburudishwa wa na Belle9!

Msanii mkali wa Bongo Flava Belle9 atakuwa ni mmoja wa wasanii watatu watakaoburudisha Tamasha la Club Royal Funga Mwaka Bash litakalofanyika mjini Tabora katika ukumbi maarufu wa New Royal Garden. Akiongelea tamasha hilo mmoja wa wadhamini wa tamasha hilo Mashaka Chura aka Mzee wa maini na Figo mkurugenzi wa Chura Fashion alisema maandalizi yamekamilika, wapenzi wa muziki wa Bongo Flava wanaotarajia kwenda kujiachia Ijumaa hii wajitokeze kwa wingi dukani kwake ambapo kuna pamba mpya na kali za kila aina ili watakapoingia katika tamasha hili la kuuaga mwaka 2013 wawe wametisha. Tamasha hilo pia litashuhudia wasanii Squizer na Ziggy Dee aliyetamba na wimbo wa Eno Mic pia wakitumbuiza ukumbini Royal Garden. Tamasha hili limewajia kwa udhamini wa Serengeti Breweries Ltd, Clouds Media Group, Chura Fashion, Gonala Pharmacy, Millenium Barber shop, Tabora Rest House, Nbs Classic, Mtingoni Company Ltd, Mussoma Batteries, CgFm 89.5, VoT fm 89.0 na Clouds Media Group.

Mama Hawa Haji Kamanga kuzikwa kesho!

Marehemu Bibi Hawa Kamanga 1941-2013
Mama Hawa Kamanga ambaye alifariki leo hii asubuhi mnamo saa 2:40 katika hospitali maalum ya wagonjwa wa Saratani ya Ocean Road ya jijini Dar es Salaam ameacha watoto 6, wa kiume watano na wa kike mmoja. Kati ya hao watatu wanaishi marekani nao ni Haji, Kaela na Hizza. Wengine wawili wa kiume wanaishi Tanzania ambao ni  Zakaria (kaka mkubwa) na Pioka. Na mmoja wa kike  Anna Kange anaishi Holland, Marehemu ameacha wajukuu 11 na kitukuu mmoja. Baada ya wanafamilia kukaa kikao, imeamuliwa kuwa marehemu atazikwa kesho saa 10:00 jioni katika makaburi ya Kisutu na shughuli zote za msiba zipo Sinza Vatican. 

Blog hii imnesikitishwa sana na kifo hiki, mwandishi wa habari hii alipata kumtembelea marehemu alipokuwa amelazwa kwa Dk Mvungi wiki tatu zilizopita. Blog inawapa pole watoto,wajukuu, ndugu, jamaa na marafiki wote wa marehemu!

MUNGU AILAZE ROHO YAKE PEMA PEPONI! AMIN


Chanzo cha habari na picha Hizza Kamanga,Grace Mmari, Houston Texas/ Tausi Khalid Dar, Tanzania.

Bibi afariki saa 48 baada ya kujua wajukuu zake wamefika hospitali kumuona!

Katika hali ya kusikitisha Mama Hawa Haji Kamanga (71) alifariki leo hii saa 2.40 Hospitalini Ocean Road  baada ya kupigania uhai wake kwa siku kadhaa alizokuwa na hali mbaya sana lakini ilielekea alipigana kubaki hai mpaka pale wajukuu zake wawili walipofika toka America siku ya Jumamosi na kwenda moja kwa moja Ocean Rd Hospital kumuona Bibi yao. Wajukuu zake hao Kaela Jr (3)na Hadassah Bianca (1) walipofikishwa wodini Marehemu akaambiwa wajuu zako wamekuja kukuona inasemekana marehemu aliyekuwa na hali mbaya kwa wakati huo alitabasamu na kujaribu kusema kitu lakini hakuweza kutoa sauti, lakini bila shaka alifurahi kujua hatimaye wajukuu zake wamemkuta akiwa hai, na hatimaye akaamua muda ulikuwa sahihi kuacha kupigania uhai wake. Mama Hawa Kamanga ana watoto kadhaa wanaoishi nchini Marekani. Marehemu alilazwa Ocean Road wiki mbili hivi baada ya kuhamishiwa hapo kutokea katika hospitali ya Dk Mvungi ambako alilazwa kwa uchunguzi wa awali. Kwa sasa mipango ya mazishi inafanyika na tutaendelea kufahamishana humu na kwingineko.
    Inna Lillah wa inna illahi Rajiun!

Shabiki wa Arsenal apoteza nyumba baada ya Man United kuishinda Gunners!

Hali mbaya
Robin Van Persie akiwazamisha The Gunners
Shabiki mkereketwa wa timu ya Arsenal (the Gunners) Mganda Henry Dhabasani mkazi wa jijini Kampala alijikuta akipoteza nyumba yake  dhidi Rashid Yiga ambaye aliweka dau la gari ya Toyota Premio na mkewe baada ya kudai Man united ingeifunga Arsenal bila shaka na wazee wa kijadi walikuwepo na kushuhudia dau hilo likipitishwa kwa maandishi kabla ya mchezo huo amabao mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Robin Van Persie alifunga bao pekee la mchezo katika kipindi cha kwanza na kuwasimamisha The Gunners katika mbio zao za kutaka kujikita zaidi katika usukani wa ligi hiyo maarufu na yenye msisimko kuliko zote duniani. Gazeti la Observer la Uganda lilieleza kuwa shabiki huyo Dhabasani mwenye wake watatu na watoto watano alizirahi baaada ya mchezo kwisha. Hata hivyo aliondoshwa katika nyumba yake siku iliyofuata.

[Video] KISOMO CHA MWISHO CHA MAMAA NYAWANA FUNDIKIRA MDA MFUPI KABLA YA MAZISHI

UHARAKA WA MUDA WA KUHAKIKISHA MWILI WA MAREHEMU UNAZIKWA ULIZINGATIWA TU MARA BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUWASILI TABORA MNAMO SAA 12 JIONI. KISOMO CHA MWISHO NA MAOMBI YA MWISHO ILIFANYWA KISHA KUELEKEA KATIKA MAZIKO YA MWILI WA NYAWANA FUNDIKIRA KATIKA MAKABURI YA ITETEMYA AMBAKO IKO IKULU YA MACHIFU WA UKOO WA FUNDIKIRA. 
ILIPOFIKA MUDA WA SAA 1:10 USIKU SHUGHULI YA MAZIKO ILIENDELEA NA KUHAKIKISHA MWILI WA MAREHEMU UMEPUMZISHWA.

*UMATI MKUBWA WA WATU ULITANDA PEMBEZONI MWA BARABARA WAKISHUHUDIA MSAFARA WA KUELEKEA KATIKA MAZISHI, ILIKUWA NI MAAJABU HAIJAWAHI TOKEA HAPO MKOANI*
UMATI WA WATU NJIANI KUELEKEA MAZISHI YA NYAWANA 
[TUNAOMBA RADHI KWA VIDEO HII KWANI HAIJACHUKULIWA KATIKA MAZINGIRA BORA, VIKWAZO VILIKUWA VINGI IKIWEMO MWENDOKASI WA GARI NA GIZA]