mkalamatukio

Azam yailaza Rhino Fc!

Timu ya Azam Fc ya jijini Dar es Salaam leo hii imeilaza timu ya Rhino Rangers ya mjini Tabora kwa goli 2 kwa sifuri kwa magoli ya Gaudence Mwaikimba kwa shuti kali lililopita kulia mwa lango la kipa wa Rhino Fc mnamo dakika ya 56,baada ya kazi nzuri ya wachezaji wa Azam Fc upande wa kulia mwa uwanja.
Baadhi ya maelfu  ya mashabiki wa soka mjini Tabora wakifuatilia kwa makini mchezo kati ya Azam Fc na Rhino Rangers uliofanyika jioni ya leo katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.
Huku Rhino Rangers ikijaribu kusawazisha bao hilo la Mwaikimba ilijikuta ikongezwa bao la pili kupitia mchezaji wa kiungo Seif Kalihe mnamo dakika ya 77 ya mchezo huo uliodorora. Timu ya Rhino Rangers itabidi ijilaumu kwa kutocheza kwa kujituma kama ambavyo ilicheza katika mchezo dhidi ya Simba ambapo waliweza kuibana Simba na kutoka nayo sare ya goli 2-2. Mchezo ujao wa Rhino utakuwa dhidi ya JKT Oljoro wikiendi ijayo mjini Arusha katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid.   
Patashika langoni mwa Azam
Basi la wachezaji wa Rhino Rangers likitoka uwanjani baada ya mchezo wao dhidi ya Azam Fc kwisha.

Utamliliaje mtu leo, kesho umtukane?

OMMY Dimpoz akilia jukwaani baada ya kulemewa na majonzi ya kifo cha Ngwair tarehe 31/05/2013 Tabora.
Siku chache baada ya kifo cha Albert Mangwea (Ngwair) kulitokea  sintofahamu baada ya msanii Ommy Dimpoz kushutumiwa na gazeti moja la kidaku kuwa alimtukana Ngwair kuwa kafa masikini (kibwege) alipokuwa akipokea tunzo yake pale Milimani city katika kilele cha Kilimanjaro Music Awards. Ninachokumbuka alisema "Sisi wasanii wa Tanzania tumechoka kufa masikini huku tukiwa na majina makubwa" na akatoa wito kwa makampuni makubwa yawape kipaumbele wasanii wa Tanzania katika suala zima la promosheni za bidhaa zao kitu ambacho kitainua kipato cha wasanii wa Tanzania badala ya kutumia wacheza mpira wa nje kama Lionel Messi. Hali ilikuwa mbaya sana kwa Ommy Dimpoz huku akilaaniwa na kusiwa huku na kule na hasa katika mitandao ya kijamii. Kabla ya Kili Music Awards huko Tabora katika kilele cha Redds Miss Tabora 2013 Ommy alitoa kauli hiyo mbele ya Mh William Ngeleja na alimuomba awasaidie kupeleka kilio chao(wasanii) bungeni ili ziunde sheria nzuri zenye kulinda maslahi ya wasanii!


Totenham wawastaajabisha Real Madrid kwa dau la kumuuza Gareth Bale!

Gazeti la michezo lenye ukaribu na kilabu cha Real Madrid leo hii limedai kuwa Mwenyekiti wa Totenham Hotspurs ya jijini London, Uingereza Bw Daniel Levy amewapa bei ya kumnunua mshambuliaji Gareth Bale kuwa ni Euro145 Milioni au kwa maneno mengine ni Pauni 125 Milioni ya Malkia wa Uingereza. Bei hiyo imewastua sana Madrid kwani hawakutegemea kabisa Bw Levy anaefahamika vema kutoa bei zisizoendana na uhalisia ambapo awali aliwasumbua sana Man United kuwanunua Michael Carrick na Dimitar Bernatov. Bei hiyo pia imelistua sana gazeti la Marca ambalo limetoa kichwa cha habari UNA LOCURA ikiwa na maana Crazy au "wazimu"



Wakati huo huo ripoti toka Spain katika gazeti la Marca zimeeleza kuwa Daniel Levy ameshapokea ofa ya Pauni 85 milioni toka klabu ya PSG ya ufaransa inayomilikiwa na matajiri wa kiarabu. Pia taarifa hiyo ilisema katika ofa zote Muhimu ni ile iliyotolewa na klabu ya Manchester United ya England ingawa chanzo hicho hakikueleza ni kiasi gani Man United wameofa kwa klabu hiyo yenye makazi yake kaskazini mwa jiji la London.

Twanga yazindua albam ya 12 na kuadhimisha miaka 15 ya kuzaliwa!


Dansa Mandela akifanya yake jukwaani.
 Bendi kongwe ya jijini Dar es Salaam, The African Stars (Twanga pepeta sugu) Kisima cha burudani nchini Tanzania, jana katika viwanja vya leaders club walizindua albam yao ya 12 iendayo kwa jina Nyumbani ni nyumbani, vile vile bendi hiyo iliadhimisha miaka 15 tangu kuzaliwa rasmi mwaka 1998.


Rapa Diof na Dogo Rama wakiwasha moto
Vipaji vingi; Kalala Junior akiimba moja ya nyimbo wlizozindua jana.

Saleh Kupaza akpaaza sauti yake jukwaaani
Na Hadija Kalili wa Bongo weekend Blog
Mope akiwa na shabiki mtasha wa Twanga
Hadija na Matinda
Hapo sasa hapo.........




AMigo Las Baba naa Sofii

Kiongozi wa bendi Mamaa Luiza Mbutu aki pose!

Historia yajirudia Miss Kanda ya Kati 2013

Maua Kimambo Karlstrom Miss Tabora namba mbili 2011.
Miss Tabora namba mbili Sabrina Juma.
 Historia imejirudia tena baada ya warembo wawili wa Redds Miss Tabora 2013 Sabrina Juma na Anastazia Donald kufanikiwa kuingia katika shindano la Taifa (Redds Miss Tanzani 2013) warembo hao wamefuata nyayo za warembo Maua Kimambo aka Maua Karlstrom na Delilah Patrick washiriki wa Miss Tabora 2011 ambao nao waliingia Miss Tanzania baada ya shindano kali la Miss kanda ya kati mwaka 2011. Katika shindano hilo la Redds Miss central zone 2013 lililofanyika mjini Dodoma katika ukumbi wa Kilimani club Ijumaa ya tarehe 14/06/2013 mrembo Happiness Ruta ambaye pia ni Miss Dodoma 2013 alifanikiwa kunyakua taji la Redds Miss Central zone akfuatiwa na mrembo Sabrina Juma aliyeshika nafasi ya pili, huku Miss Singida 2013 akishika nafasi ya tatu. Hata hivyo majaji wakiongozwa na Bw Hashim Lundenga mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania waliona wachukue warembo wanne kwenda Miss Tanzania badala ya watatu baada ya Miss Tabora Anastazia Donald ambaye alishika nafasi ya nne kuweka ushindani mkali na kuwalazimisha majaji kufikiri mara mbili na kuamua kuchukua warembo wanne kitu ambacho Chief Judge Hashim Lundenga alikiri haijawahi kutokea huko nyuma.

Top five.

Miss Tabora 2013 Anastazia Donald.

Delilah Patrick, Miss Tabora namba tatu mwaka 2011

Washiriki wa Miss Tabora walipotembelea mabaki ya ngome ya Mtemi Isikie mwana Kiyungi!


Huu ulikuwa mlango mkuu wa kuingilia katika ngome ya Mtemi Isike mwana Kiyungi iliyoitwa Isyunula mnamo 1890.
Katika kuwajengea uelewa mpana warembo wa Redds Miss Tabora 2013 wikiendi iliyopita walipelekwa Kwihara lilipo tembe la mvumbuzi maarufu duniani Dr David Livingstone na pia walipata fursa ya kutembelea mabaki ya iliyokuwa ngome (Ikulu) ya Mtemi maarufu wa Unyanyembe Mtemi Isike mwana Kiyungi ambaye alipigana na Wajerumani na kuwashinda kwa miaka 5 mpaka wajerumani walipotuma mamluki wa Kiarabu kuisoma ngome hiyo ndipo walipofanikiwa kuishambulia kwa mizinga ambapo Mtemi huyo shujaa wa Unyanyembe kabla ya kukamatwa na Wajerumani akakusanya familia yake wakiwemo wake zake na jeshi lake wakajifungia ndani akajiripua na baruti na kufa, kwani aliona bora kufa kuliko kukamatwa na wakoloni. Mungu amlaze mahala pema peponi shujaa huyu!
Mzee Kibisuka Kasuka Said Fundikira ndiye aliyetoa maelezo kwa warembo wa Redds Miss Tabora 2013 juu ya ngome hiyo
Mzee Kibhisuka akiwahadithia wrembo jambo fulani. 
Warembo wakimsikiliza kwa makini.

Hapa wakitazama ulipo mlima baada ya kuambiwa kitu juu ya mlima huo.

Hapa wakitoka eneo ilipo ngome ya Isyunula.

Mrembo Kurwa akiuliza swali la mwisho kwa mwenyeji wao!

Warembo wa Redds Miss Tabora 2013 waenda kuzuru tembe la Dr Livingstone

Mzee Hamisi 
Kamati ya Redds Miss Tabora 2013 jana iliwapeleka warembo wao katika kijiji cha Kwihara kilometa 12 hivi toka Tabora mjini ambako walizuru tembe la Dr David Livingstone ambaye alikuwa mvumbuzi wa mambo mbali mbali ikiwemo vyanzo vya mito barani Afrika. Washiriki hao walikieleza kituo cha tv cha Clouds kuwa wamefurahishwa na ziara hiyo kwani imewaongezea uelewa juu ya mambo ya kale husasan David Livingstone . Wikiendi ijayo warembo hao wamepangiwa kutembelea nyumba za watoto yatima na wodi ya watoto katika Hospitali ya Kitete ya mjini Tabora.


Bango hili linaonesha tarehe, siku na mwaka aliopita  Livingstone 

Mrembo Cornencia akijitwisha kibuyu

Mrembo Faidha Hamis akijaribu mkufu uliotengenezwa kwa simbi.

Hapa wakimsikiliza Mzee Hamisi

Mrembo Sabrina Juma

TABASAMU

Cornencia akihojiwa na TBC

Pili Issa (Matron) kushoto akimshikia Mic, Cornencia. aliyekuwa akihojiwa na Nidudu Iddy wa Clouds Tv

Anastazia akihojiwa na clouds Tv