Washiriki wa Miss Tabora walipotembelea mabaki ya ngome ya Mtemi Isikie mwana Kiyungi!

Washiriki wa Miss Tabora walipotembelea mabaki ya ngome ya Mtemi Isikie mwana Kiyungi!


Huu ulikuwa mlango mkuu wa kuingilia katika ngome ya Mtemi Isike mwana Kiyungi iliyoitwa Isyunula mnamo 1890.
Katika kuwajengea uelewa mpana warembo wa Redds Miss Tabora 2013 wikiendi iliyopita walipelekwa Kwihara lilipo tembe la mvumbuzi maarufu duniani Dr David Livingstone na pia walipata fursa ya kutembelea mabaki ya iliyokuwa ngome (Ikulu) ya Mtemi maarufu wa Unyanyembe Mtemi Isike mwana Kiyungi ambaye alipigana na Wajerumani na kuwashinda kwa miaka 5 mpaka wajerumani walipotuma mamluki wa Kiarabu kuisoma ngome hiyo ndipo walipofanikiwa kuishambulia kwa mizinga ambapo Mtemi huyo shujaa wa Unyanyembe kabla ya kukamatwa na Wajerumani akakusanya familia yake wakiwemo wake zake na jeshi lake wakajifungia ndani akajiripua na baruti na kufa, kwani aliona bora kufa kuliko kukamatwa na wakoloni. Mungu amlaze mahala pema peponi shujaa huyu!
Mzee Kibisuka Kasuka Said Fundikira ndiye aliyetoa maelezo kwa warembo wa Redds Miss Tabora 2013 juu ya ngome hiyo
Mzee Kibhisuka akiwahadithia wrembo jambo fulani. 
Warembo wakimsikiliza kwa makini.

Hapa wakitazama ulipo mlima baada ya kuambiwa kitu juu ya mlima huo.

Hapa wakitoka eneo ilipo ngome ya Isyunula.

Mrembo Kurwa akiuliza swali la mwisho kwa mwenyeji wao!