Adam Fundikira alinibebesha mkoba wa kaseti-Hamisi Dakota

Adam Fundikira alinibebesha mkoba wa kaseti-Hamisi Dakota

Hamisi Dakota
Meneja wa bendi ya Mapacha Watatu Hamisi Dakota alisema Adam Fundikira ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa Club Royal ya Tabora alikuwa ni mtu muhimu sana katika maisha yake akiwa anakua hapa Tabora katika miaka ya thamanini ambapo ambapo ameeleza alivyokuwa akiruka ukuta wa nyumbani kwao usiku wakati wazazi wake wakiwa wamelala ili kumuwahi Adam ambebee mkoba wa kaseti na kupata ubwete wa kuingia Disco bure. Adam alikuwa Dj katika ukumbi wa Honey Pot(Mwana Isungu) ambayo kwa sasa inaitwa Club Royal.

Awali Dakota aliwaita jukwaani Mkala Fundikira na Adam Fundikira na kusema "Nimewaita hawa hapa jukwaani kwa kuwa hawa wanatoka katika familia ya ki chifu ya Fundikira ambayo ndio ilikuwa mtawala wa mkoa huu kabla ya uhuru ingawa palikuwa na utawala wa kikoloni kama wasimamizi, hivyo nimewaita kwa heshima kwani usipowaheshimu watemi(Machifu) unaweza ukashitukia vyombo vinaungua bila ya sababu za msingi. Aliwahi kuja Totoo Ze Bingwa akaunguza vyombo hapa Tabora, ni vema tunapoenda katika miji ya watu tupige hodi" Dakota aliyesema hayo usiku wa alhamisi ya tarehe 2 April2013 ambapo bendi ya Mapacha watatu ilitumbuiza katika ukumbi wa Frankman Palace.

Dakota akisistiza jambo.

Adfun Smiler na Mratibu wa Miss Tabora 2013

Mkala Fundikira na Hamisi Dakota