mkalamatukio

Fwd: DkShein Aendelea na Kampeni Zake na Kusema Ataendeleza Kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa na Kuleta Maendeleo Zaidi kwa Wazanzibar katika Wananchi Wake na Elimu Bure Zanzibar.


Mgombea Urais wa Zanzibar Kupitia Chama cha Mapinduzi pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Viongozi wa CCM Zanzibar alipowasili katika viwanja vya Mpira Konde Kisiwani Pemba kuendelea na Kampeni Kisiwani Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwasalimia Wananchi waliofika katika uwanja wa kunde kuhudhuria mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein.wakati akiwasili katika viwanja hivyo vya mpira Konde Wilaya ya Micheweni Pemba.
Wanachama wa CCM Wakimshangilia Mgombea wao wa Urais Dk Shein, wakati akiwasili katika viwanja vya mpira Konde kwa ajili ya mkutano wake wa Tatu wa Kampeni zake kisiwani Pemba.
Taswira ya wakati wa mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais kupitia CCM katika viwanja vya mpira Konde Pemba kama inavyooneka Mwanachama huyu wa CCM akishangilia akiwa na picha ya Mgombea Urais wa CCM Dk Shein.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndg Hamad Mberwa Hamad akiwahutubia na kutuoa Sere za CCM zilivotelekezwa na kuiletea Maendeleo Zanzibar katika kipindi chake Dk Shein cha miaka mitano na kuwataka kumpa kura kwa mara ya pili kuendeleza mafanikio ya Maendeleo Zanzibar katika sekta mbalimbali za Jamii 

Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein akiwana na Viongozi wakifuatilia mkutano huo wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya mpira Konde kisiwani Pemba ikiwa ni mkutano wake wa tatu kisiwani Pemba akiwa katika kampeni zake.
Katibu wa Idara ya Uenezi Afisi Kuu Zanzibar Ndg Waride Bakari Jabu akiwahutubia Wananchi wa Konde katika mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein uliofanyika katika uwanja wa mpira Konde Kisiwani Pemba.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Ndg Khadija Aboud akiwahutubia Wananchi na Wana CCM kisiwani Pemba wakati wa Mkutano wa Kampeni ya Mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Kisiwani Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein akiwahutubia Wananchi katika viwanja vya mpira Konde Kisiwani Pemba akiwa katika kampeni yake na kuwataka Zanzibar kukipigia kura Chama cha Mapinduzi kwa maendeleo na kudumisha Amani na Utulivu kwa Wananchi wake kwa maendeleo. 
Viongozi wa Jukwaa kuu wakimsikiliza Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, wakati akiwahutubia Wananchi wa Konde Pemba Wilaya ya Micheweni akiwa katika mikutano yake ya kampeni kisiwani Pemba.
Wazee wa CCM Wilaya ya Micheweni wakiwa katika viwanja vya mkutano wa kampeni ya Urais wa Zanzibar wakimsikiliza Dk Shein wakati akiwahutubia na kutowa Sera za CCM kwa wananchiwakati wa mkutano huo uliofanyika katika viwanja vya mpira Konde Wilaya ya Micheweni Pemba.
Wanachama wa CCM wakimshangilia mshangilia Mgombea wa Urais Dk Shein, wakati akiwahutubia Wananchi wa Wilaya ya Micheweni akiwa katika mikutano yake ya Kampeni Kisiwani Pemba.
Mwana CCM Pemba akishangilia wakati wa mkutano huo wa kampeni ya Urais wa Zanzibar katika viwanja vya Konde Pemba.
           Wananchi wakiwa katika viwanja vya mkutano Konde wakifuatilia mkutano huo.

Wanachama wa CCM wakiwa katika viwanja vya mpira Konde wakimsikiliza Mgombea Wao akiwahutubia katika mkutano wa Kampeni ya CCM Pemba.

            WanaCCM wakishangilia wakati wa mkutano huo katika viwanja vya mpira Konde Pemba.

Viongozi wa Jukwaa Kuu wakisimama wakati Dk Shein, akienda kuwahutubia Wananchi wakati wa Mkutano wake wa Tatu wa Kampeni Kisiwani Pemba uliofanyika katika viwanja vya mpira Konde Wilaya ya Micheweni Pemba.

Mgombea Urais wa Zanzinzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akijiandaa kuwahutubia Wanachama wa CCM katika viwanja vya mpira Konde Kisiwani Pemba akiwa katika mikutano yake ya kampeni Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akiwahutubia Wananchi katika viwanja vya mpira konde kisiwani Pemba akiwa katika kampeni za kuomba kura kwa Wananchi kuendelea kuongoza Zanzibar kwa kipindi cha Pili ilin kuendelea maendeleo kwa Wananchi wa Zanzibar na kudumisha Amani na Utulivu kwa wananchi wake,
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akionesha Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa Wananchi wa Wilaya ya Micheweni Pemba wakati wa mkutano wake wa Kampeni na kuwataka kuichagua CCM kuzi kuwaletea maendeleo katika miradi mbalimbali na kuendelea kuongoza Zanzibarb kwa misingi ya Sheria na haki kwa maendeleo ya Wazanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi wa Jimbo la Konde Ndg Omar Seif Abeid, wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi wa Jimbo la Tumbe Ndg Ali Khamis Bakar, wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi wa Jimbo la Micheweni Pemba, Ndg Shamata Shaame Khamis,, wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi wa Jimbo la Wingi Pemba Ndg.Said Omar Said, wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa Jimbo la Wingwi Pemba, Ndg Khamis Shaame Hamad, wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa Jimbo la Konde, Pemba, Ndg Ramadhani Omar Ahmed, wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tumbe Pemba, Ndg Rashid Kassim Abdalla. wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa Jimbo la Micheweni Pemba, Ndg Khamis Juma Omar, wakati wa mkutano huo wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein, katika viwanja vya mpira Konde Pemba.
Wananchi wakishangilia wakati wa kuwatambulisha wagombea Ubunge na Uwakilishi na Udiwani wa Wilaya ya Micheweni Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk. Shein akiwatambulisha Wagombea Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi katika Wilaya ya Micheweni Pemba wakati wa mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar katika viwanja vya mpira Konde Pemba. 
Wananchi wakishangilia wakati wa kuwatambulisha wagombea Ubunge na Uwakilishi na Udiwani wa Wilaya ya Micheweni Pemba.
Shekh akisoma dua baada ya kumalizika kwa mkutano wa kampeni ya Urais wa Zanzibar uliofanyika kastika viwanja vya mpira Konde Pemba Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, akiondoka viwanja vya Konde Pemba baada ya kumaliza mkutano wake wa tatu wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya mpira Konde Pemba, akiongozania na Viongozi wa CCM.

Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot. Zanzinews.com 

MSAFARA WA SUGU WASHAMBULIWA KWA MAWE AKIELEKEA KATIKA KAMPENI ZAKE ZA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA MBEYA


Gari la Mgombea Ubunge jimbo la Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi Sugu likiwa kituo cha Polisi kati jijini Mbeya mara baada ya kushambuliwa kwa mawe na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CCM.
Sugu akiwa kituo cha Polisi na wafuasi wake.Picha Kenneth Ngelesi Mbeya .


Na Emanuel Kahema ,Mbeya


MGOMBEA ubunge  kupitia chadema jimbo la Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi leo  amejikuta katika wakati mgumu baada ya msafara wake kushambuliwa na mawe na wafuasi wanaosadikiwa kuwa ni wa chama   cha mapinduzi CCM na kwamba katika tukio hilo watu wawili wamejeruhiwa akiwemo dereva aliyekuwa akimuendesha mgombea huyo  .

Tukio hilo la kushambuliwa kwa msafara huo, limetokea majira ya saa 11 za jioni katika eneo  la barabarani lililopo katika Kata ya Ghana mtaa wa Mbata jijini hapa  ambapo inasemekana mgombea huyo alikuwa  katika harakati za kampeni kuomba kura kwa wananchi wa Iziwa  ambapo mgombea huyo alikuwa ndani ya gari yake yenye namba za usajili T161 CPP Toyota  Land Cruser VX .

Awali, wafuasi wa chama cha mapinduzi CCM, walikuwa katika mkutano wa hadhara wa kumnadi mgombea wao ngazi ya Udiwani katika kata ya Ghana iliyopo ndani ya Jiji la Mbeya, hivyo wakiwa kwenye harakati hizo inasemekana walishangaa kuona msafara wa sugu ukipita katikati ya mkutano huo hivyo kushindwa kuvumilia na kuanza kurusha mawe huku wengine wakishikana mithili ya kutaka kupigana.

Katika vurugu hizo gari aliyokuwa amepanda mgombea huyo  lilipasuliwa kioo cha mbele na gari ya chama cha mapinduzi CCM wilaya ya Mbeya, ikipasuliwa kioo cha mbele .


Aidha Vurugu hizo zimesababisha   majeruhi wawili ambao wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya akiwemo dereva wa mbunge huyo na mfuasi mmoja wa chadema.

Kutokana na hali hiyo  mgombea huyo wa ubunge mbeya mjini kwa tiketi ya Chadema alilazimika kuikatisha zoezi lake la kuongea na wakazi wa Kata ya Iziwa iliyopo Jijini Mbeya kwa muda, kutokana na kulazimika kuripoti katika kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa maelezo.

Mgombea huyo ilimlazimu kufika kituoni na kuchukuliwa maelezo na baada ya hapo aliruhusiwa kuendelea na shughuli zake za kisiasa lakini gari yake yenye namba za usajili T161 CPP aliyokuwa akiitumia katika kampeni zake ikibaki polisi.

Hata hivyo, mgombea huyo alipomaliza kutoa maelezo  katika kituo cha polisi cha kati cha Wilaya ya Mbeya, aligoma kuzungumza na vyombo vya habari ambavyo vilikuwa kwenye eneo la tukio na kuwataka wafike katika mkutano kwani ndipo atakapotolea ufafanuzi wa suala hilo hilo.

                      (JAMIIMOJABLOG MBEYA )

TAMASHA LA 34 LA KIMATAIFA LA SANAA NA UTAMADUNI KUFANYIKA TAREHE 21-27, 2015, MJINI BAGAMOYO MKOANI PWANI


 Mwenyekiti wa Tamasha la 34 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni, John Mponda (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu tamasha hilo litakalofanyika kuanzia tarehe 21 hadi 27, 2015 katika Kumbi na Viunga vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), mkoani Pwani. Kulia ni Katibu wa Tamasha hilo na Ofisa Biashara, Benjamini Malimbali na Ofisa Habari, Sophia Mtakajimbo.
  Hapa Mwenyekiti wa Tamasha hilo, John Mponda (kulia) akisisitiza jambo kuhusu tamasha hilo. Kushoto ni Ofisa Habari wa Tamasha la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.


TAMASHA la kimataifa la sanaa na utamaduni Bagamoyo liliasisiwa mwaka 1981 na Chuo cha Sanaa Bagamoyo ambacho kwa sasa ni Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo. Lengo kuu la Tamasha kwa wakati huo ilikuwa ni kuwapa nafasi wanafunzi wa chuo cha sanaa kuonyesha kwa vitendo yale waliojifunza kwa mwaka mzima kwa kuwashirikisha wakazi wa Bagamoyo, baada ya Tamasha hilo kufanikiwa uongozi wa chuo uliamua tamasha hilo lifanyike kila mwaka kwa kushirikisha Vikundi mbalimbali vya ndani na nje ya nchi ili kubadilishana Uzoefu  na hivyo kujizolea umaarufu ndani na nje ya Tanzania.

Tamasha la kimataifa la sanaa na utamaduni Bagamoyo mwaka huu litafanyika kwa mara ya 34 kuanzia tarehe 21-27 Septemba katika kumbi na viunga vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo ambao ndio wenyeji na waandaaji wa tamasha hilo kongwe Tanzania.

Maandalizi yote ya Tamasha hili yamekamilika Tamasha la mwaka huu linabeba Kauli mbiu isemayo SANAA NA UTAMADUNI KATIKA UCHAGUZI HURU NA WA AMANI’  Aidha kutakuwa na mada ndogondogo zitakazotolewa kupitia kongamano na warsha zitakazohusu  Haki za binadamu, Rushwa na kupinga Mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino)

Mgeni rasmi katika ufunguzi wa Tamasha atakuwa mzee Rashid Masimbi, aliyekuwa mkuu wa chuo wa kwanza toka taasisi ilivyokuwa chuo cha sanaa,hivyo kwa kutambua mchango wake kwenye sanaa Taasisi imempa heshima ya kuwa mgeni rasmi .

Tamasha la mwaka huu litahusisha Ngoma za Asili, Maigizo, Sarakasi, Mazingaombwe, Muziki wa kisasa na asili, Sanaa za Ufundi  na bidhaa mbalimbali.

Jumla ya vikundi 65 kutoka ndani na nje ya Tanzania vimethibitisha kushiriki,ambapo vikundi 59  ni kutoka ndani ya Tanzania na vikundi 6 kutoka nchi za Kenya, Namibia, Afrika Kusini, Korea na Congo na Zimbabwe.

Kiingilio kwenye tamasha kwa wakubwa shilingi 3000/=,kwa watoto shiling 1000/= na kwa wageni wasio watanzania  shilingi 5000/=

Taasisi inatoa wito kwa wadau mbalimbali wa Sanaa,Makampuni,Taasisi za Serikali na zisizo za Serikali kujitokeza kudhamini tamasha hili muhimu ambalo hufanyika kila mwaka ili kulifanya liwe bora na la kimataifa zaidi , kwa mustakabali wa sanaa na utamaduni wa Mtanzania. 


MAGUFULI APOKELEWA KAMA MFALME KIGOMA,WANANCHI WAKIRI WAZI ATOSHA KUWA RAIS


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kupitia chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia  maelfu ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za Urais,uliofanyika katika uwanja wa Kawawa,mkoani Kigoma jioni ya leo.

 Dkt Mafuli amewaabia wananchi wa Kigoma kwenye mkutano wa kampeni leo jioni kwenye uwanja wa kawawa kuwa Serikali yake kwa sehemu kubwa itakuwa upande wa wananchi wanyonge ili hatimaye wawe na maisha yenye neema,amesema kuwa Serikali yake haitakuwa ya kunyanyasa mama ntile na kudaiwa kodi za hovyo hovyo,amesema kuwa ataimarisha ukusanyaji wa kodi kwenye serikali yake, lakini pia atawabana wafayabiashara  wakubwa ambapo baadhi yao hawalipi kodi

Magufuli amewataka Wananchi kumuamini kwa yale ambayo amekuwa akiyasema kwenye mikutano yake ya kampeni na kuongeza anachoahidi ndicho ambacho atakitekeleza kwenye serikali yake na kwenye maisha yake huwa hataki kutoa ahadi za uongo.

 Aidha hadi jana, tarehe 16 September 2015, Mgombea Urais wa CCM, Dkt. John Pombe Magufuli, alikuwa amekwishafanya kampeni katika mikoa 12 na Majimbo 94. Amekwishafanya mikutano mikubwa ya hadhara 76 na mikutano ya barabarani 381. Amekwishatembea, kwa gari, jumla ya kilomita 13,720. Kwa ujumla amekwishakutana, moja kwa moja, na asilimia zaidi ya 30 ya wapiga kura.
Wananchi na Mabango yao
Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Nguruka kwenye mkutano wa kampeni wa hadhara mapema leo mchana.
Wakazi wa Nguruka waifuatilia Mkutano.
Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli akimkabidhi Ilani ya chama cha CCM kwa Mgombea Ubunge wa Kigoma Kusini,Hasna Mwilima na pia kummwombea kura kwa wananchi mapema leo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika Nguruka mkoani Kigoma.
Wananchi wakisikiliza sera za Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli
Baadhi ya Wananchi wa Uvinza wakiwa wamefunga barabara wakitaka wasikilizwe kero zao na Mgombea Urais wa CCM,Dkt Magufuli alipokuwa akipita mjni humo akielekea Kigoma mjini kwenye mkutano wa hadhara.
Baadhi ya akina mama wakishangilia jambo
Mgombea Ubunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini Peter Selukamba akiwahutubia wananchi wa Kalinzi,mkoani Kigoma kwenye mkutano wa kampeni za Uraisi jioni ya leo.
Baadhi ya wafuasi wa chama cha CCM wakifuatilia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kalinzi,ambapo mgombea Urais wa CCM Dkt Magufulia aliwahutubia wananchi.
Wakazi wa mji wa Nguruka,mkoani Kigoma wakifuatilia mkutano wa hadhara
Wananchi na mabango yao
Kada maarufu na aliyewahi kuwa Katibu MKuu wa CCM,Mh Yusuph Makamba akisalimiana na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kupitia chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli kabla ya kupanda jukwaani na kuwaomba ridhaa wakazi wa kigoma ya kuwaongoza katika awamu ya tano.
Wananchi wakishangilia jambo kweye mkutano wa kampeni za Urais

Wananchi wakifuatilia mkutano wa kampeni
Kada maarufu na aliyewahi kuwa Katibu MKuu wa CCM,Mh Yusuph Makamba akiwahutubia wananchi wa Kigoma na vitongoji vyake jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za Urais,uliofanyka katika uwanja wa Kawawa mkoani Kigoma

Picha zote na Michuzi Jr