mkalamatukio

RAIS MSTAAFU MHESHIMIWA ALI HASSAN MWINYI AWASILI JIJINI WASHINGTON DC.


 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akiambata na mama Sitti Mwinyi wawasili jijini Washington DC tayari kwa tamasha maalum la Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Mkuu wa utawala Lilly Munanka wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC, mara alipowasili hotelini.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na mmoja wa wafanyakazi wa ubalozi Edward Taji.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Afisa wa Ubalozi Swahiba Mndeme.
  Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Afisa wa Ubalozi Emmanuel Swere.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na mmoja wa wafanyakazi wa ubalozi John Anbiah
     Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akiwa ameongozana na mama Sitti   Mwinyi na baadhi ya msafara wake katika hoteli waliyofikia.
                                  PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI
Click here to Reply or Forward 1.43 GB (9%) of 15 GB used Manage Terms - Privacy Last account activity: 12 hours ago Details

BALOZI MPYA WA ANGOLA ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON DC.


 Mhe, balozi wa Angola Agostinho Tavares akipokelewa na afisa wa ubalozi  Swahiba Mndeme alipotembelea ubalozi .
 Mhe, balozi Liberata Mulamula akiwa na furaha baada ya mgeni wake kufika ofisini .
 Mhe balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja na mgeni wake balozi wa Angola Agostinho Tavares.
 Mhe Balozi wa Angola nchini Marekani Agostinho Tavares akiweka sahihi  kitabu cha wageni.
 Mhe balozi wa Angola chini Marekani Agostinho Tavares akimsikiliza kwa makini mwenyeji wake balozi Liberata Mulamula alipokua akijitambulisha .
Mhe balozi Libarata Mulamula na balozi wa Angola nchini marekani Agostinho Tavares pamoja na afisa wa ubalozi Swahiba Mndeme walipokua wakibadilishana mawazo. 

Picha kwa hisani ya camera ya ubalozi

             

Ujumbe wa Imetosha ukiwa Metro Fm 99.4 Mwanza!


Kutoka kushoto ni Juma Herman (meneja wa Green Palm Hotel), Issaya Mwakilasa aka Wakuvwanga, Jhikolabwino Manyika, Kelvina John, Mwenyekiti Masoud Kipanya na Tonny Alphonce(Mtangazaji Metro fm 99.4

Siku ya Ijumaa ya tarehe 17/04/2015 ujumbe wa Imetosha Foundation ukiongozwa na Mwenyekiti Masoud Kipanya ulifanya mahojiano katika kituo cha redio cha Metro Fm 99.4 kwenye kipindi cha Pambazuko la Metro fm 99.4 ikiwa ni katika mfululizo wa kujitambulisha kanda ya ziwa kwa taasisi hiyo inayopinga mauaji kwa watu wenye ualbino kwa njia ya elimu. Msanii wa vichekesho (comedian) Wakuvwanga ambaye ni mjumbe wa taasisi hiyo alitoa kali alipoulizwa angependekeza adhabu gani kwa watakaopatikana na hatia ya kuua watu wenye ualbino? akajibu "Kwa kuwa hawa si watu bali ni wanyama kutokana na vitendo vyao viovu basi napendekeza serikali iwapeleke Mikumi national park iwafungie ndani ya senyenge ili watalii wawe wanaenda kuwaona kama wanavyoenda kuwaona Simba na wanyama wengine! Kipindi hicho maridhawa kiliendeshwa na watangazaji Tonny Alphonce na Katumba Madua
Mtangazaji wa kipindi cha Pambazuko la Metro Fm, Tonny Alphonce akimuuliza swali Masoud Kipanya.
Masoud Kipanya akijibu swali toka kwa mtangazaji wa Metro Fm 99.4zaji Tonny Alphonce.
Tonny akimpiga swali Wakuvwanga, anayesikiliza kwa umakini wa hali ya juu, soma uone jibu lake!
Kutoka kushoto ni Katumba Madua, Wakuvwanga na  msanii wa muziki wa Reggae Jhikoman

Moja ya studio za Metro Fm 99.4 ambazo wanazo tatu katika jengo hilo lililopo kati kati ya jiji la Mwanza
Picha ya Pamoja ndani ya Metro fm 99.4 toka kushoto ni Juma Herman, Mkala Fundikira, Kelvina John, George Binagi, Tonny Alphonce, Rosier, Sophia George, Wakuvwanga Masoud na Katumba Madua
Jhikoman kushoto, Rosier(receiptionist) na Masoud
Masoud akibadilishana mawazo na Sophia George wa Metro fm 99.4 ya Mwanza wiki iliyopita ujumbe wa Imetosha Foundation ulipotembelea studio za kituo hicho cha redio

Mtandao huu unaomba radhi kwa kuchelewa kurusha habari hii kwa wakati muafaka kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu. Ahsante!

WATANZANIA WAFANYA VIZURI MBIO ZA NGORONGORO MARATHONI 2015


Waziri mkuu Mstaafu , Fredrick Sumaye akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine mbalimbali wakiwemo waandaji buda mfupi kabla ya kuanza kwa mbio za Km 21 Katika gate la kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro,
Waziri mkuu Msaatfu Fredirick Sumaye akikimbia sambamba na rais wa shirikisho la riadha Tanzania,RT,Athony Mtaka(Kushoto kwake) mkuu wa mkoa wa Arusha ,Daud Ntibenda,pamoja na mkuu wa wilaya ya Karatau Omary Kwaang kuashiria kuanza kwa mbio za Ngorongoro Marathoni.
Maratibu wa Mbio , Meta Paul akiwa na mmoja wa wasiamamizi ,Leila wakati wakiwaandaa wanariadha kuanza mbio za Km 21 katika lango la kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro.
Mbio zikianza rasmi.
Baaadhi ya washiriki katika mbio hizo ,walikuwemo pia wadhamini kama Maremga Investment,hapa Marenga mwenye truck suit nyeusi akijaribu kukimbiza upepo.
Awawli mbio zikiwa bado ndio zimeanza kundi la wakimbiaji lilionekana wote wanakimbia kwa karibu.
Muda ulivyosonga na hatua ndivyo zilivyo ongezeka.
Hatimaye wakaanza kuachana mmoja baada ya mmoja,
Wengine wakaamua kwenda pamoja ili kupeana moja.
wengine wakafunguka zaidi.
Hatimaye wakapatikana wakimbiaji watatu wakaongoza hadi mwisho wa mbio na hawa ni ,Joseph Theofily(katikati),George Gerald (kulia) na Emanuel Giniki.
Mkimbiaji raia wa Kenya ambaye jina lake halikufahamika mara moja akijaribu kuonesha umahiri wake katika mbio hizo.
Msichana pekee aliyekuwa akiongoza ni Failuna Abdi .
Nyuma ya Failuna alikuwepo Nathalia Elisante.
Mshindi wa kwanza katika Mbio za Ngorongoro Maratahoni 2015 ,Joseph Theofily akimaliza mbio hizo katika uwanja wa Mazingira Bora akitumia muda wa 1:03:09.
Mshindi wa Pili katika mbio hizo ,George Gerald akihitimisha mbio hizo akitumia muda wa 1:03:36
Mshindi wa tatu ,Emanuel Giniki akikalimilisha mbio kwa muda wa 1:03:42.
Giniki akijaribu kupoza koo mara baada ya kumaliza mbio.
Mkimbiaji wa klabu ya riadha ya Holili,Osward Moris akihitimisha mbio.
Mshindi wa kwanza kwa kina dada Failuna Abdi akihitimisha mbio katika nafasi ya kwanza baada ya kutumia muda wa 1 :10:25
Mgeni rasmi katika mbio hizo ,Waziri mkuu Mstaafu ,Fredirck Sumaye akiingia uwanjani huku akihitimisha mbio za km 21 .

WANARIADHA wa Tanzania Joseph Theofily wa klabu ya riadha ya Holili ya mkoani Kilimanjaro na Failuna Abdi wa klabu ya riadha ya Winning Spirit ya jijini Arusha wamefanikiwa kupeperusha vyema Bendera ya taifa baada ya kuibuka washindi wa kwanza katika mbio za kimataifa za
Ngorongoro Marathoni kwa upande wa wanaume na wanawake.

Mwanariadha Theofily alifanikiwa kumaliza mbio za km 21 akitumia muda wa saa 1:03:09 na kujinyakulia kitita cha sh Mil, 1. mbele ya wakongwe wengine kutoka nchi za Kenya ,Uganda na Malawi huku Gabriely Gerald wa klabu ya Winning Spirit ya jijini Arusha akishika nafasi ya pili akimaliza mbio akitumia saa 1:03:36 na kujinyakulia kitita cha sh laki 5.

Emanuel Giniki alifanikiwa kushika nafasi ya tatu na kujinyakulia zawadi ya sh 250,000,nafasi ya nne ikichukuliwa na Ezekiel Therop huku mwanariadha Mohamed Msenduki wa klabu ya Wining Spirit ya jijini Arusha akimaliza nafasi ya tano.

Mwanariadha wa kike Failuna aliyerejea hivi karibuni kutoka nchini Brazil kushiriki mashindano ya mbio za Km 15 ambazo alifanikiwa kumaliza mbio hizo katika nafasi ya saba,aliwaongoza wakongwe kama Banuelia Bryton ,Marry Naali Jackline sakilu na Catherine Range akimaliza mbio katika nafasi ya kwanza kwa kutumia muda wa saa
1:10:25.

Failuna aliyejinyakulia zawadi ya kitita cha kiasi cha sh Mil,1. alifuatiwa kwa karibu na mpinzani wake Nathalia Elisante aliyetumia muda wa 1:14:40 na kuzawadiwa kitita cha sh 500,000 huku nafasi ya tatu  ikichukuliwa na Magdalena Crispine aliyetumia muda wa 1:15:56, nafasi ya nne na tano ikienda kwa Anjelina Tsere na Merry Naali.

Mbio za kimataifa Ngorongoro Marathoni zinafanyika zikiwa na lengo la kuwawezesha watoto wa jamii ya kimasai kupata elimu ikiwemo kumalizia shule ya Endulen iliyoko Ngorongoro na kutangaza urithi wa utalii kupitia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro huku ikishirikisha pia mbio za Kilomita tano kwa wafanyakazi wa taasisi mbalimbali pamoja na  Km 2.5 kwa wanafunzi.


Kwa picha zaidi ingia hapa,

www.dixonbusagaga.blogspot.com

MKUTANO MKUBWA WA NENO LA MUNGU WA WASABATO WATANZANIA WAISHIO NCHINI MAREKANI WATOTO WATENGEWA SEHEMU YAO.

 Watoto wakiwa sehemu yao chini ya uangalizi maalumu huku wazazi wao wakihudhuria mkutano mkubwa wa neno la Mungu unaondelea DMV kwa siku nne ikiwa leo Jumampili April 19, 2015 ndio hitimisho la mkutano huo.
 Watoto wakiangalia vipindi vya watoto kwenye luninga.
 Msimamizi wa watoto Tanya Muganda akielekeza jambo.
 Tanya Muganda akiwapatia zawadi watoto