mkalamatukio

WATANZANIA WAFANYA VIZURI MBIO ZA NGORONGORO MARATHONI 2015


Waziri mkuu Mstaafu , Fredrick Sumaye akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine mbalimbali wakiwemo waandaji buda mfupi kabla ya kuanza kwa mbio za Km 21 Katika gate la kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro,
Waziri mkuu Msaatfu Fredirick Sumaye akikimbia sambamba na rais wa shirikisho la riadha Tanzania,RT,Athony Mtaka(Kushoto kwake) mkuu wa mkoa wa Arusha ,Daud Ntibenda,pamoja na mkuu wa wilaya ya Karatau Omary Kwaang kuashiria kuanza kwa mbio za Ngorongoro Marathoni.
Maratibu wa Mbio , Meta Paul akiwa na mmoja wa wasiamamizi ,Leila wakati wakiwaandaa wanariadha kuanza mbio za Km 21 katika lango la kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro.
Mbio zikianza rasmi.
Baaadhi ya washiriki katika mbio hizo ,walikuwemo pia wadhamini kama Maremga Investment,hapa Marenga mwenye truck suit nyeusi akijaribu kukimbiza upepo.
Awawli mbio zikiwa bado ndio zimeanza kundi la wakimbiaji lilionekana wote wanakimbia kwa karibu.
Muda ulivyosonga na hatua ndivyo zilivyo ongezeka.
Hatimaye wakaanza kuachana mmoja baada ya mmoja,
Wengine wakaamua kwenda pamoja ili kupeana moja.
wengine wakafunguka zaidi.
Hatimaye wakapatikana wakimbiaji watatu wakaongoza hadi mwisho wa mbio na hawa ni ,Joseph Theofily(katikati),George Gerald (kulia) na Emanuel Giniki.
Mkimbiaji raia wa Kenya ambaye jina lake halikufahamika mara moja akijaribu kuonesha umahiri wake katika mbio hizo.
Msichana pekee aliyekuwa akiongoza ni Failuna Abdi .
Nyuma ya Failuna alikuwepo Nathalia Elisante.
Mshindi wa kwanza katika Mbio za Ngorongoro Maratahoni 2015 ,Joseph Theofily akimaliza mbio hizo katika uwanja wa Mazingira Bora akitumia muda wa 1:03:09.
Mshindi wa Pili katika mbio hizo ,George Gerald akihitimisha mbio hizo akitumia muda wa 1:03:36
Mshindi wa tatu ,Emanuel Giniki akikalimilisha mbio kwa muda wa 1:03:42.
Giniki akijaribu kupoza koo mara baada ya kumaliza mbio.
Mkimbiaji wa klabu ya riadha ya Holili,Osward Moris akihitimisha mbio.
Mshindi wa kwanza kwa kina dada Failuna Abdi akihitimisha mbio katika nafasi ya kwanza baada ya kutumia muda wa 1 :10:25
Mgeni rasmi katika mbio hizo ,Waziri mkuu Mstaafu ,Fredirck Sumaye akiingia uwanjani huku akihitimisha mbio za km 21 .

WANARIADHA wa Tanzania Joseph Theofily wa klabu ya riadha ya Holili ya mkoani Kilimanjaro na Failuna Abdi wa klabu ya riadha ya Winning Spirit ya jijini Arusha wamefanikiwa kupeperusha vyema Bendera ya taifa baada ya kuibuka washindi wa kwanza katika mbio za kimataifa za
Ngorongoro Marathoni kwa upande wa wanaume na wanawake.

Mwanariadha Theofily alifanikiwa kumaliza mbio za km 21 akitumia muda wa saa 1:03:09 na kujinyakulia kitita cha sh Mil, 1. mbele ya wakongwe wengine kutoka nchi za Kenya ,Uganda na Malawi huku Gabriely Gerald wa klabu ya Winning Spirit ya jijini Arusha akishika nafasi ya pili akimaliza mbio akitumia saa 1:03:36 na kujinyakulia kitita cha sh laki 5.

Emanuel Giniki alifanikiwa kushika nafasi ya tatu na kujinyakulia zawadi ya sh 250,000,nafasi ya nne ikichukuliwa na Ezekiel Therop huku mwanariadha Mohamed Msenduki wa klabu ya Wining Spirit ya jijini Arusha akimaliza nafasi ya tano.

Mwanariadha wa kike Failuna aliyerejea hivi karibuni kutoka nchini Brazil kushiriki mashindano ya mbio za Km 15 ambazo alifanikiwa kumaliza mbio hizo katika nafasi ya saba,aliwaongoza wakongwe kama Banuelia Bryton ,Marry Naali Jackline sakilu na Catherine Range akimaliza mbio katika nafasi ya kwanza kwa kutumia muda wa saa
1:10:25.

Failuna aliyejinyakulia zawadi ya kitita cha kiasi cha sh Mil,1. alifuatiwa kwa karibu na mpinzani wake Nathalia Elisante aliyetumia muda wa 1:14:40 na kuzawadiwa kitita cha sh 500,000 huku nafasi ya tatu  ikichukuliwa na Magdalena Crispine aliyetumia muda wa 1:15:56, nafasi ya nne na tano ikienda kwa Anjelina Tsere na Merry Naali.

Mbio za kimataifa Ngorongoro Marathoni zinafanyika zikiwa na lengo la kuwawezesha watoto wa jamii ya kimasai kupata elimu ikiwemo kumalizia shule ya Endulen iliyoko Ngorongoro na kutangaza urithi wa utalii kupitia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro huku ikishirikisha pia mbio za Kilomita tano kwa wafanyakazi wa taasisi mbalimbali pamoja na  Km 2.5 kwa wanafunzi.


Kwa picha zaidi ingia hapa,

www.dixonbusagaga.blogspot.com

MKUTANO MKUBWA WA NENO LA MUNGU WA WASABATO WATANZANIA WAISHIO NCHINI MAREKANI WATOTO WATENGEWA SEHEMU YAO.

 Watoto wakiwa sehemu yao chini ya uangalizi maalumu huku wazazi wao wakihudhuria mkutano mkubwa wa neno la Mungu unaondelea DMV kwa siku nne ikiwa leo Jumampili April 19, 2015 ndio hitimisho la mkutano huo.
 Watoto wakiangalia vipindi vya watoto kwenye luninga.
 Msimamizi wa watoto Tanya Muganda akielekeza jambo.
 Tanya Muganda akiwapatia zawadi watoto

Jiji la Mwanza katika ubora wake!

Maeneo ya Bwiru, Mwanza

Mawe hayo pichani huwekwa humo yalimo ili kuzuia mmomomonyoka wa ardhi mvua na upepo mkal!















Tanzanian Mayunga Malimi is the winner of Airtel TRACE Music Star grand finale!


You chose Mayunga Nalimi! Tanzania's contestant seduced you and the judges Akon, Lynsha and Devyne Stephens. After a finale full of unexpected developments, Mayunga has been one of the only to keep his calm during his performances. That's probably why he fainted just after he heard final verdict!

Mayunga Malimi has quickly attracted judges' eyes with great live and acapella performances. He also took advantage of Laurna and Jitey failures in the last round of the finale to take the title back home. 

He will now join Akon in the studio to work on his first single.
A new superstar is born! Hongera kijana wetu!
habari kwa hisani ya  Issa Michuzi

HARAKATI ZA KUANZISHWA KWA KARIAKOO FAMILY FOUNDATION (KFF)

 Mwenyekiti wa Kariakoo Family Foundation (KFF) Mohamed Bhinda akiongoza kikao cha Kamati ya Utendaji katika kuandaa rasimu ya katiba ya chama hicho kinachotarajiwa kusajiliwa  hivi karibuni kama taasisi isiyo ya kiserikali kwa nia ya kukutanisha upya wadau wote waliozaliwa, walioishi na wenye asili ya Kariakoo katika Wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam. Mkutano huu umefanyika leo jioni Kinondoni Studio. Kulia kwa Bhinda ni katibu wa chama hicho Senpai Wahid
 Mtunza hazina wa KFF Yahaya Sameja akielezea namna chama hicho cha jamii ya wana Kariakoo kitavyoweza kujiendesha kwa njia za ada, michango na misaada ya wafadhili katika kuendeleza wanachama, ikiwa ni pamoja na kusaidiana katika shida na raha. Kushoto ni Mwenyekiti wa KFF Mohamed Bhinda na kati ni Makamu Mwenyekiti Tatu Lumelezi
 Wana KFF wakipata mlo wa mchana wakati wa mapumziko
Jopo la kamati ya utendaji ya KFF baada ya mkutano wao leo

Ijue historia ya Linda

NI MENGI AMEZUNGUMUZA AMBAYO MIMI NA WEWE HATUKUYAJUA
Kesho Jumatatu katika kipindi cha huyu na yule cha mahojiano na mwanamitindo mbunifu wa LB kutoka Atlanta, Georgia atakapoelezea historia yake yenye milima na mabonde historia ya maisha yake yenye huzuni na furaha wakati mwingine Linda akitokwa na machozi kwa kukumbuka maisha aliyopitia. Je Mume wake Mali walijuana nae wapi? na mengine mengi kuhusu maisha yake ikiwemo kampuni yake ya LB na malengo yake ya kupeperusha bendera ya Tanzania anga za kimataifa. USIKOSE mahojiano yaliyofanywa na mwakilishi wa Vijimambo na kwanza production Michigan Alpha Igogo ambae alitaka kujua undani wa maisha ya mwanadada Linda

Alpha Igogo akifanya mahojiano na Linda jijini Atlanta
Maswali yalikua moto Linda akipumua na kumkumbatia Alpha Igogo baada ya mahojiano kufikia mwisho

Balozi wa IMETOSHA FOUNDATION Henry Mdimu atoa wito kwa vyombo vya habari na jamii!


Balozi Henry Mdimu akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za gazeti la Mwananchi mjini Mwanza.

Henry Mdimu ametoa wito kwa vyombo vya habari na jamii nchini kulichukua suala la ukatili na mauaji kwa watu wenye ualbino kama lao ili kuiondoa nchi yetu katika aibu hii. Aliyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za gazeti la Mwananchi ambao ni wadhamini wa habari wa ujio wa kamati ya Imetosha katika kanda ya ziwa.
Kutoka kushoto ni Salome Gregory, Henry Mdimu Mgaya, Issaya Mwakilasa na Zaytun Biboze.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Balozi Mdimu

Imetosha
Kila sauti inasikika.
PIGA KELELE uunge mkono haki ya KUISHI

Ndugu waandishi wa habari, Mwakilishi wa Tanzania Bloggers Network, mabibi na mabwana…..
Tuko hapa kuueleza Ulimwengu kupitia vyombo mbali mbali vya habari juu ya harakati yetu ya IMETOSHA. Harakati hii hii  imeanzishwa na mimi mwenyewe, Henry Mdimu, mwanahabari mwenzenu ambaye nimeamua kwa moyo mmoja kuwa Balozi wa kujitolea wa harakati za kukomesha mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu  wa ngozi, maarufu kwa jina la Albino.
Mimi na ujumbe wangu tumekuja Mwanza kutambulisha harakati za IMETOSHA na ikiwa sehemu ya kuandaa shughuli zitakazofanyika kanda ya Ziwa ikiwa ni sehemu ya kupambana na mauaji na unyanyasaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Mwezi ujao ujumbe wa IMETOSHA utakuja na kuweka kambi ya kudumu Mwanza itakayozunguka kanda ya Ziwa na kutembelea nyumba kwa nyumba zenye wahanga wa matukio ya mauaji na kutoa elimu kwa jamii kuwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi hayasababishi utajiri.
Pamoja na shughuli tutakazofanya tukiwa Kanda ya Ziwa mwezi wa tano ni pamoja na maetmbezi ya hisani, kutakua na mpira kati ya Simba na Yanga ambapo IMETOSH itavalisha wachezaji Thisrts zake ikiwa ni sehemu ya kutangaza harakati zetu.
Pia tutakua na tamasha litakaloshirikisha wasanii mbalimbali watakaotumbuiza nyimbo mbamimbali zitakazokua na ujumbe wa kukemea na kupinga mauaji na manyanyaso dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Nimeamua kufanya hivi baada ya kushuhudia ndugu zangu wakiteseka kwa muda mrefu. Awali nilishindwa kuanzisha harakati hizi nikiamini kuna vyombo vinavyohusika na utetezi wa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Hrakati hizi zimeanza baada ya kuona kadri muda unavyokwenda matukio yamezidi kuongezeka na hali kuwa mbaya. Nashuhudia ndugu zangu wakinyanyaswa, wakibezwa mtaanai na hata kudhihakiwa huku baadhi ya wanaoshuhudia haya wakicheka tu.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na vyombo vya habari vilimkariri Rasi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania muheshimwa Jakaya Kikwete akisema kesi mbili za mauaji ya watu wenye ulemavuwa ngozi zililipotiwa kwa mwaka 2012 na 2013.
Taarifa hizo ziliongeza kuwa kti ya mwaka 2006 na 2015, watuhumiwa 139 wameshikiliwa na kesi 35 zimeandikishwa. Watuhumiwa 73 waliachiwa huru na wengine 15 wamekutwa na makosa.
Hivyo nimeamua niweke jitihada zangu binafsi niisaidie Serikali yangu katika kuondoa doa hili linaloichafua Nchi  yetu yenye sifa ya Amani duninia nzima. Hivyo nawaomba Watanzania wenzangu mniunge mkono tukishirikiana na Serikali ili mauaji haya yakome.
Kutokana na ushawishi nilionao kama Mwandishi, Mtangazaji wa redio na Blogger naamini nitaleta mabadiliko makubwa katika kuhakikisha haki ya kusihi kwa ndugu zangu inaheshimiwa na kubaki historia. Salamu zangu ziwafikie wanyanyasaji, wauaji na wenye kufanya dhihaka kwa watu wenye ulemavu wa ngozi kuwa IMETOSHA.
Uchunguzi wangu wa awali umebaini ukosefu wa elimu juu ya watu wenye ulemavu wa ngozi hupelekea tatizo hili kukua na hatimaye kuuana kw aimani za kishirikina. Hivyo basi, silaha ya Elimu ni sehemu kubwa ya haraki hizi.
Mimi pamoja na mafariki zangu wanaoniunga mkono tutakwenda Kanda ya Ziwa kutoa Elimu kabla tatizo hili halijaenea Nchi nzima. Swali moja tujiulize kwa nini Kanda ya Ziwa? Tutatoa Elimu kwa njia ya ushauri nasaha, pia wanamuziki  sanaa
Nina mpango wa kwenda kanda ya Ziwa kuhangaika na hili mpaka nione mwisho wake. Na ni rahisi kumaliza hili tatizo kabla halijaenea nchi nzima. Maana Walemavu wa ngozi wako nchi nzima lakini jiulize kwa nini Kanda ya Ziwa tu?
Mimi pamoja na rafiki zangu hawa, tunatoka kuelekea huko kutoa elimu kwa njia ya sanaa, na washauri nasaha. Pia tutakua na team ya wanamuziki wanaoandaa nyimbo mbali mbali za kutoa mafunzo ya kutokomeza ukatili huu.
Wasanii hao ni paoma na Jhikoman, Kassim Mganga, Profesa J, Ray C, Fid Q, Roma Mkatoliki na Dami Msimamo.  Tutaishi na jamii hii kwa muda tukiongea nao kwa lugha yao kwa kutumia wakalimani kwa wsifahamu Kiswahili kuwashawishi waamini hakuna ukweli katika Imani hizo.
Naamini nguvu ya vyombo vya Habari hivyo naomba ushirikaiano wenu katika kuhakikisha tunatokomeza mauaji ya wenzetu ili mwisho wa siku wanunuzi wa viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi wafukuzwe watakaanza kuuliza jinsi ya kufanya mauaji haya.
Harakati za IMETOSHA rasmi zimezinduliwa rasmi tarehe 3/3/2015.
Mungu atubariki.
Ahsanteni
HENRY MDIMU-0715000881 na 0787000880
Balozi wa kujitolea
Harakati za IMETOSHA

SALOME GREGORY 0717367309

Mratibu wa Habari- Harakati za IMETOSHA