mkalamatukio

Jiji la Mwanza katika ubora wake!

Maeneo ya Bwiru, Mwanza

Mawe hayo pichani huwekwa humo yalimo ili kuzuia mmomomonyoka wa ardhi mvua na upepo mkal!















Tanzanian Mayunga Malimi is the winner of Airtel TRACE Music Star grand finale!


You chose Mayunga Nalimi! Tanzania's contestant seduced you and the judges Akon, Lynsha and Devyne Stephens. After a finale full of unexpected developments, Mayunga has been one of the only to keep his calm during his performances. That's probably why he fainted just after he heard final verdict!

Mayunga Malimi has quickly attracted judges' eyes with great live and acapella performances. He also took advantage of Laurna and Jitey failures in the last round of the finale to take the title back home. 

He will now join Akon in the studio to work on his first single.
A new superstar is born! Hongera kijana wetu!
habari kwa hisani ya  Issa Michuzi

HARAKATI ZA KUANZISHWA KWA KARIAKOO FAMILY FOUNDATION (KFF)

 Mwenyekiti wa Kariakoo Family Foundation (KFF) Mohamed Bhinda akiongoza kikao cha Kamati ya Utendaji katika kuandaa rasimu ya katiba ya chama hicho kinachotarajiwa kusajiliwa  hivi karibuni kama taasisi isiyo ya kiserikali kwa nia ya kukutanisha upya wadau wote waliozaliwa, walioishi na wenye asili ya Kariakoo katika Wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam. Mkutano huu umefanyika leo jioni Kinondoni Studio. Kulia kwa Bhinda ni katibu wa chama hicho Senpai Wahid
 Mtunza hazina wa KFF Yahaya Sameja akielezea namna chama hicho cha jamii ya wana Kariakoo kitavyoweza kujiendesha kwa njia za ada, michango na misaada ya wafadhili katika kuendeleza wanachama, ikiwa ni pamoja na kusaidiana katika shida na raha. Kushoto ni Mwenyekiti wa KFF Mohamed Bhinda na kati ni Makamu Mwenyekiti Tatu Lumelezi
 Wana KFF wakipata mlo wa mchana wakati wa mapumziko
Jopo la kamati ya utendaji ya KFF baada ya mkutano wao leo

Ijue historia ya Linda

NI MENGI AMEZUNGUMUZA AMBAYO MIMI NA WEWE HATUKUYAJUA
Kesho Jumatatu katika kipindi cha huyu na yule cha mahojiano na mwanamitindo mbunifu wa LB kutoka Atlanta, Georgia atakapoelezea historia yake yenye milima na mabonde historia ya maisha yake yenye huzuni na furaha wakati mwingine Linda akitokwa na machozi kwa kukumbuka maisha aliyopitia. Je Mume wake Mali walijuana nae wapi? na mengine mengi kuhusu maisha yake ikiwemo kampuni yake ya LB na malengo yake ya kupeperusha bendera ya Tanzania anga za kimataifa. USIKOSE mahojiano yaliyofanywa na mwakilishi wa Vijimambo na kwanza production Michigan Alpha Igogo ambae alitaka kujua undani wa maisha ya mwanadada Linda

Alpha Igogo akifanya mahojiano na Linda jijini Atlanta
Maswali yalikua moto Linda akipumua na kumkumbatia Alpha Igogo baada ya mahojiano kufikia mwisho

Balozi wa IMETOSHA FOUNDATION Henry Mdimu atoa wito kwa vyombo vya habari na jamii!


Balozi Henry Mdimu akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za gazeti la Mwananchi mjini Mwanza.

Henry Mdimu ametoa wito kwa vyombo vya habari na jamii nchini kulichukua suala la ukatili na mauaji kwa watu wenye ualbino kama lao ili kuiondoa nchi yetu katika aibu hii. Aliyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za gazeti la Mwananchi ambao ni wadhamini wa habari wa ujio wa kamati ya Imetosha katika kanda ya ziwa.
Kutoka kushoto ni Salome Gregory, Henry Mdimu Mgaya, Issaya Mwakilasa na Zaytun Biboze.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Balozi Mdimu

Imetosha
Kila sauti inasikika.
PIGA KELELE uunge mkono haki ya KUISHI

Ndugu waandishi wa habari, Mwakilishi wa Tanzania Bloggers Network, mabibi na mabwana…..
Tuko hapa kuueleza Ulimwengu kupitia vyombo mbali mbali vya habari juu ya harakati yetu ya IMETOSHA. Harakati hii hii  imeanzishwa na mimi mwenyewe, Henry Mdimu, mwanahabari mwenzenu ambaye nimeamua kwa moyo mmoja kuwa Balozi wa kujitolea wa harakati za kukomesha mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu  wa ngozi, maarufu kwa jina la Albino.
Mimi na ujumbe wangu tumekuja Mwanza kutambulisha harakati za IMETOSHA na ikiwa sehemu ya kuandaa shughuli zitakazofanyika kanda ya Ziwa ikiwa ni sehemu ya kupambana na mauaji na unyanyasaji wa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Mwezi ujao ujumbe wa IMETOSHA utakuja na kuweka kambi ya kudumu Mwanza itakayozunguka kanda ya Ziwa na kutembelea nyumba kwa nyumba zenye wahanga wa matukio ya mauaji na kutoa elimu kwa jamii kuwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi hayasababishi utajiri.
Pamoja na shughuli tutakazofanya tukiwa Kanda ya Ziwa mwezi wa tano ni pamoja na maetmbezi ya hisani, kutakua na mpira kati ya Simba na Yanga ambapo IMETOSH itavalisha wachezaji Thisrts zake ikiwa ni sehemu ya kutangaza harakati zetu.
Pia tutakua na tamasha litakaloshirikisha wasanii mbalimbali watakaotumbuiza nyimbo mbamimbali zitakazokua na ujumbe wa kukemea na kupinga mauaji na manyanyaso dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Nimeamua kufanya hivi baada ya kushuhudia ndugu zangu wakiteseka kwa muda mrefu. Awali nilishindwa kuanzisha harakati hizi nikiamini kuna vyombo vinavyohusika na utetezi wa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Hrakati hizi zimeanza baada ya kuona kadri muda unavyokwenda matukio yamezidi kuongezeka na hali kuwa mbaya. Nashuhudia ndugu zangu wakinyanyaswa, wakibezwa mtaanai na hata kudhihakiwa huku baadhi ya wanaoshuhudia haya wakicheka tu.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na vyombo vya habari vilimkariri Rasi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania muheshimwa Jakaya Kikwete akisema kesi mbili za mauaji ya watu wenye ulemavuwa ngozi zililipotiwa kwa mwaka 2012 na 2013.
Taarifa hizo ziliongeza kuwa kti ya mwaka 2006 na 2015, watuhumiwa 139 wameshikiliwa na kesi 35 zimeandikishwa. Watuhumiwa 73 waliachiwa huru na wengine 15 wamekutwa na makosa.
Hivyo nimeamua niweke jitihada zangu binafsi niisaidie Serikali yangu katika kuondoa doa hili linaloichafua Nchi  yetu yenye sifa ya Amani duninia nzima. Hivyo nawaomba Watanzania wenzangu mniunge mkono tukishirikiana na Serikali ili mauaji haya yakome.
Kutokana na ushawishi nilionao kama Mwandishi, Mtangazaji wa redio na Blogger naamini nitaleta mabadiliko makubwa katika kuhakikisha haki ya kusihi kwa ndugu zangu inaheshimiwa na kubaki historia. Salamu zangu ziwafikie wanyanyasaji, wauaji na wenye kufanya dhihaka kwa watu wenye ulemavu wa ngozi kuwa IMETOSHA.
Uchunguzi wangu wa awali umebaini ukosefu wa elimu juu ya watu wenye ulemavu wa ngozi hupelekea tatizo hili kukua na hatimaye kuuana kw aimani za kishirikina. Hivyo basi, silaha ya Elimu ni sehemu kubwa ya haraki hizi.
Mimi pamoja na mafariki zangu wanaoniunga mkono tutakwenda Kanda ya Ziwa kutoa Elimu kabla tatizo hili halijaenea Nchi nzima. Swali moja tujiulize kwa nini Kanda ya Ziwa? Tutatoa Elimu kwa njia ya ushauri nasaha, pia wanamuziki  sanaa
Nina mpango wa kwenda kanda ya Ziwa kuhangaika na hili mpaka nione mwisho wake. Na ni rahisi kumaliza hili tatizo kabla halijaenea nchi nzima. Maana Walemavu wa ngozi wako nchi nzima lakini jiulize kwa nini Kanda ya Ziwa tu?
Mimi pamoja na rafiki zangu hawa, tunatoka kuelekea huko kutoa elimu kwa njia ya sanaa, na washauri nasaha. Pia tutakua na team ya wanamuziki wanaoandaa nyimbo mbali mbali za kutoa mafunzo ya kutokomeza ukatili huu.
Wasanii hao ni paoma na Jhikoman, Kassim Mganga, Profesa J, Ray C, Fid Q, Roma Mkatoliki na Dami Msimamo.  Tutaishi na jamii hii kwa muda tukiongea nao kwa lugha yao kwa kutumia wakalimani kwa wsifahamu Kiswahili kuwashawishi waamini hakuna ukweli katika Imani hizo.
Naamini nguvu ya vyombo vya Habari hivyo naomba ushirikaiano wenu katika kuhakikisha tunatokomeza mauaji ya wenzetu ili mwisho wa siku wanunuzi wa viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi wafukuzwe watakaanza kuuliza jinsi ya kufanya mauaji haya.
Harakati za IMETOSHA rasmi zimezinduliwa rasmi tarehe 3/3/2015.
Mungu atubariki.
Ahsanteni
HENRY MDIMU-0715000881 na 0787000880
Balozi wa kujitolea
Harakati za IMETOSHA

SALOME GREGORY 0717367309

Mratibu wa Habari- Harakati za IMETOSHA

Ujumbe mzito wa Imetosha watembelea kituo cha Buhangija mjini Shinyanga!


Ilikua mishale ya saa kumi kamili jioni ujumbe wa harakati za Imetosha ulipowasili katika kituo cha Buhangija cha kulea watoto wenye mahitaji maalumu mjini Shinyanga. Sauti za furaha za watoto zilisikika zikiimba nyimbo za kukaribisha ujumbe wa wana harakati hao ambao wako Mwanza kutambulisha harakati za Imetosha ambazo ni kupambana na kupinga unyanyapaa, ukatili na mauaji kwa watu wenye Ulemavu wa ngozi.

Balozi wa Imetosha Henry Mdimu akinunua mahitaji ya watoto waliopo kituoni hapo kabla ya kufika kituoni hapo.
Huyu ni Irene wa NHIF Shinyanga

Wajumbe wa Imetosha
 Akiongea na watoto kituoni hapo Mwenyekiti wa harakati za Imetosha Masoud Ali (Kipanya) alisema Imetosha inatambua umuhimu wa haki ya kuishi kwa kila binadamu ndio maana Imetosha imeanzisha harakati za kutokomeza mauaji na unyanyapaa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.  “Tunatambua hapa kati yenu kuna vipaji vya aina mbalimbali hivyo pamoja na kupambana na harakati za kupinga na kutokomeza mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi tupo hapa kuwatia moyo kuwa mna uwezo mkubwa ndani yenu hivyo msijidharau” alisema Masoud.

Kipanya akimuimbisha mtoto wa kituoni hapo
Mwl Peter Alali Francis akisisitiza jambo wakati akiongea na ujumbe wa Imetosha

 Alisema“Pamoja na uhaba wa mabweni kituo kinakabiliwa na uhaba wa chakula. Muda mwingine watoto hawa hushindia mlo mmoja. Chakula mlichofikisha leo hapa kitatusogeza maana tulikua tumeishiwa chakula kabisa” alisema Francis. Ujumbe huo wa Imetosha uliwasilisha kambini hapo unga kilo 50, mchele kilo 50, chumvi kilo 5 na mafuta ya kupikia lita 10. 

Mwalimu Mkuu wa Kituo hicho Peter Ajali Francis alishukuru ujio wa wanaharakati wa Imetosha kituoni hapo na kusema kituo hicho kilianzishwa mwaka 1960 kikiwa chini ya Kanisa katoliki.
Kituo hicho kilikua maalumu kwa ajli ya watoto wasiiona na viziwi lakini kutokana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi kuongezeka mwaka 2006 kituo hicho kilianza kupokea watoto wenye ulemavu wa ngozi kutoka sehemu mbalimbali toka kanda ya Ziwa. Kituo kina jumla ya watoto 388 kati ta hao 284 wana ulemavu wa ngozi. Kituo hicho kinakabiliwa na uhaba wa mabweni ambapo chumba chenye uwezo wa kuchukua watoto 50 kinachukua watoto zaidi ya 100 na chenye uwezo wa kuchukua watoto 40 kinachukua watoto zaidi ya 80.


 Zaytun Biboze akiwa amebeba mmoja wa watototo wanaoishi katika ktuo hicho



Masoud Kipanya na Jhikoman wakiwaimbisha watototo wimbo waupenda wa Clap your hands!
Isaya Mwakilasa aka Wakuvwanga akiwachekesha watoto kiuoni Buhangija, Shinyanga


Magunia haya ya unga, mafuta na mchele ndio msaada wa chakula ambao Imetosha ilitoa kwa kituo hicho


Katibu wa Imetosha amabaye ki taaluma ni mwandishi wa habari akimhoji mwalimu Francis Ajali
Wanaharakati wa Imetosha wamepanga kurudi tena mjini Shinyanga mwezi Mei na kukifanya kituo hicho kuwa ngome ya kuanzishia mapambano dhidi ya unyanyapaa, ukatili na mauaji kwa albino.
Picha na Mkala Fundikira habari na Salome Gregoy/ Mkala Fundikira 

EPUSHA AJALI OKOA MAISHA!