mkalamatukio

Kamati ya imetosha yatuma ujumbe mzito kanda ya ziwa!


Balozi Henry Mdimu akiongea na vyombo vya habari
Taasisi isiyo ya ki serikali ya Imetosha Foundation inayopinga unyanyapaa, ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino kwa njia ya elimu, inatarajia kutuma ujumbe mzito kanda ya ziwa hapo kesho kwa maandalizi ya ujio wa timu nzima ya taasisi hiyo iliyojikita kwenye kubadilisha mtazamo (mind set) wa watu juu ya janga hili. Ujumbe huo utaongozwa na mwenyekiti wa taasisi hiyo Bw Masoud Kipanya, Balozi Henry Mdimu Mgaya na katibu Salome Gregory,wajumbe watakaongozana na viongozi hao ni pamoja na Mkala Fundikira, Isaya Mwakilasa (wakuvwanga aka Baba Andunje) Zaytun Biboze, Kelvina John na msanii wa muziki wa reggae Jhikoman Manyika.

Mwenyekiti Masoud Kipanya akiongea katika kilele cha matembezi ya hamasa yaliyofanyika jijini Dar
Dhumuni la safari hiyo itakayoupeleka ujumbe huo mpaka mkoani Shinyanga ni kwenda kujitambulisha kwa viongozi wa serikali na usalama wa mikoa na za kanda hiyo iliyoathiriwa sana na janga la ukatili na mauaji ya watu wenye ualbino. Taasisi ya Imetosha imepanga kwenda kanda ya ziwa baadaye mwezi ujao ambapo timu itaenda maeneo yaliyoathiriwa na kutoa elimu kwa wakazi wa maeneo hayo kuwa si kweli kwamba ukiwa na kiungo cha mtu mwenye ualbino utapata mafanikio, elimu hizo zitatolewa kwa njia ya filamu mbali mbali, michezo ya kuigiza na matamasha ya muziki.
Hoteli ya Green Palm utakapofikia ujumbe wa Imetosha Foundation jijini Mwanza aka the Rock City.
Ujumbe huu ukiwa mjini Mwanza utakuwa chini ya udhamini wa hoteli ya Green Palm iliypo maeneo ya Bwiru, vile vile kampuni ya Mwananchi communication ltd (MCL) inayozalisha gazeti bora la Mwananchi na mengineyo itachapisha habari zote kuhusiana na msafara huo wa Imetosha kanda ya ziwa. Meneja wa hotel 

Isaya Mwakilasa wa (Orijino komedi) Henry Mdimu na familia ya Isaya aka Wakuvwanga
ya Green Palm Bw Juma Herman ameuambia mtandao huu kuwa "imekuwa rahisi kwetu (Green Palm Hotel) kudhamini makazi na usafiri kwa taasisi hiyo kwa kuwa inachofanya ni kitu chema basi nasi tumeona ni vema tuwatie nguvu kwa kuwapatia malazi na usafiri wa ndani kwa kipindi chote watakachokuwa jijini Mwanza, kwa kweli sasa imetosha ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino" aliongeza.
Wakiongea na mtandao huu kwa nyakati tofauti Mwenyekiti Masoud Kipanya na Balozi Henry Mdimu walisema  wanashukuru sana kwa kitendo cha Green Palm na Mwananchi communictaion na kuwa ni vya kuigwa na makampuni mengine ili kuiwezesha taasisi hiyo kufikia malengo yake. Taasisi ya Imetosha haina vyanzo vya fedha hivyo kutegemea wahisani kama Green Palm Hotel na Mwananchi communication.
Maktaba Baadhi ya wajumbe wa Imetosha wakijiandaa kwenda katika mchezo wa Simba na Yanga

WANAFUNZI WA CARMAN AINSWORTH HIGH SCHOOL WATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON DC.

 Wanafunzi wa Carman Ainsworth High School iliyopo Michigan watembelea ubalozi wa Tanzania Washington DC, na kupata fursa ya kuonana na Mhe balozi Liberata Mulamula.
Baadhi ya wanafunzi wakimsikiliza kwa makini Mhe, balozi Leberata Mulamula.
Mhe, balozi Liberata Mulamula akitoa historia fupi ya Tanzania.
   Mhe, balozi Liberata Mulamula akiwashukuru wageni wake kwa kuchagua ubalozi wa Tanzania kama sehemu mojawapo ya ziara yao hapa mjini Washington DC.
Picha na habari kwa hisani ya Mubela Bandio wa Changamoto blog

Siku Mh Al Shaymaar Kweigir alipoweka uheshimiwa pembeni na kusema IMETOSHA!


Mh Al Shaymaar akicheza wimbo wa Imetosha na balozi Mdimu pamoja na  baadhi ya watu waliohudhuria matembezi ya uhamasishaji wimbo huo uliimbwa na msanii wa reggae Jhikoman Manyika  .
Siku ya matembezi ya uhamasishaji dhidi ya mauaji ya watu wenye ualbino yaliyofanika kutoka viwanja vya Biafra mpaka viwanja vya leaders mbunge wa viti maalum Mh Al Shaymaar Kweigir aliamua kuuvua uheshimiwa kwa muda na kujichanganya na wadau wengine walijitokeza kiwanjani hapo kwa kucheza kwa hisia kubwa yenye kuinesha kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Imetosha foundation za kuelimisha na hatimaye kutokomeza kabisa unyanyapaa, ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino duniani! Matembezi na tamasha viliandaliwa na Imetosha foundation kwa dhamini toka IPTL, Legendary Music, EFM Radio, TDL, Coca Cola, Ultimate security na Flexible studios
Mwenyekiti wa Imetosha foundation akimpongeza Mh Al Shaymaar baada ya matembezi.










MC mkongwa Mzee Mdachi akiwa katika pose!

Nyie chukueni selfie mie nimevutiwa na ya jukwaani!
Rose Manumba na Jamila wakiwakilisha!
Monica Joseph kulia akiongea na baadhi ya wadau wa harakati za Imetosha

Emmanuel Masaka akijiuliza Nitumie camera gani hapa????

Kelvina na Jestina  wa Jestina George blog
Wajumbe  wa Imetosha foundation!
Picha zote na Mkala Fundikira wa keronyingi blog

Winga Adam Johnson atuhumiwa kubaka binti mdogo!

Mchezaji wa kiungo wa kilabu cha Sunderland Adam Johnson amesimamishwa na kilabu chake baada ya kukamatwa na polisi kwa tuhuma za kujamiiana na msicha mwenye umri wa miaka (15).

Winga huyo mwenye miaka (27) anasadikika kupokea pauni 50,000 (Tsh milioni 1370) kwa wiki alikamatwa nyumbani kwake na polsi toka Durham katika hekalu lake lenye thamani pauni 1.8m mnamo siku ya jumatatu na baadae kupatiwa dhamana.

Kilabu cha Sunderland kimethibitisha kuwa kimemsimisha Johnson kupisha upelelezi, na hatua hiyo itaanza kazi jumanne ambapo Sunderland itacheza na Hull City katika mfululizo wa ligi kuu ya England Barclays Pemier league. Sunderland ilimsaini Johnson kwa pauni 10m toka Manchester city mwaka 2012. Imeelezwa kuwa winga huyo mwenye mtoto mmoja amekuwa akipenda kushobokewa na wasichana na ni mpenda starehe wa hali ya juu. 

Adam Johnson akiwa na mpenzi wake mwaka2012 Man City ilipotwaa ubingwa England.
Hapa akishangilia goli dhidi ya watani wa jadi New Castle
Hii ndio nyumba ambamo Adam Johnsona alikamatiwa na polisi wa Durham
Imetafsiriwa na Mkala Fundikira 
habari na picha mailonlinefootball

Tafrija ya Tanzania bloggers yafana Serena hotel!

Mwenyekiti wa Mtandao wa mabloga Tanzania Bw Joachim Mushi (The habari blog) akisisitiza jambo wakati akiwakaribisha wageni waalikwa na mgeni rasmi.
Mgeni rasmi katibu mtendaji wa MCT Bw Kajubi Mukajanga na Blogger Othman Maulid(Zanzibar leo) 
Kutoka kushoto Mkala Fundikira(keronyingi blog), Jennifer Zighilla(Chingaone blog) na Joshua Fanuel 
Mgalula Fundikira, Peter Moe na Mkala Fundikira 
Mrs Issa Michuzi, Shamim na mdau
Kutoka kushoto Rahel Pallangyo, Chingaone, Malunde na Monica Joseph Monfinance
Malunde1, Mgalula Fundikira, Faraji Swai na Mdau
Mgalula Fundikira, Henry Mdimu (Balozi IMETOSHA MOVEMENT) Mkala Fundikira na Rahel Pallangyo
Malunde1 akisalimiana na Mgeni rasmi Bw Mukajanga.


Mdau, Malunde na Jo Mwaisango(Mbeya yetu)


Msanii Jhikoman alikuwepo pia

Wakala wa Mdhamini Vodacom, NMB na Raha
William Malecela( Blog ya wananchi)
Afisa uhusiano wa Vodacom Bw Kevin Twissa akihutubia hafla hiyo

Toka kushoto ni Mgeni rasmi Bw Kajubi D Mukajanga, Joachim Mushi, Issa Michuzi, Othman Maulid, Josh Fanuel na Henry Mdimu.
Chingaone,Josh Fanuel na Father Kidevu
Mwakilishi kutoka USA embnassy ya Tanzania
Msanii Jhikoman akitumbuiza na wimbo wa Ushirkina na John Kitime (Cheka na Kitime blog)
Jhikoman akipiga gitaa
Mkala Fundikira, Woinde Shizza na Faraji Swai
Mgeni rasmi akikata Ndafu
Mkala na Rose Ndauka(Bongo movie star)
Freddy, Khadija Kalili(Bongo weekend) na Mkala
Rose Ndauka, Mkala na mwenyekiti Mushi
Mabloga wafanya dhihaka miongoni mwao

Mdau na Rose Ndauka
Adela kavishe (dallykavisheblog)
Mdau na Chingaone
Zainul Mzige(Mo Blog) na Woinde Shizza.
Picha zote kwa hisani ya mkalamatukio blog