mkalamatukio

Voice of Tabora ( Vot fm 89.0fm) kurusha live shughuli za mazishi ya Nyawana Fundikira

Mac Denny akiwa na baadhi ya wafanyakazi wenzake wa VOT fm 89.0  redio walipokuwa wakiwasilisha ubani wao kwa Baba mdogo wa marehemu Bw Adam Fundikira
Kituo cha redio cha Voice of Tabora kimejitolea kurusha Live shuhuli zote za mazishi ya marehemu Nyawana Fundikira ambaye aliwahi kufanya kazi katika kituo hicho kwa miaka kadhaa. Kituo hicho cha redio kinamilikiwa na Mh Aden Rageh mbunge wa Tabora mjini. Familia ya marehemu imepongeza hatua hiyo ya VoT fm kwani wapenzi wengi wa Mamaa Nyawana ambao hawatoweza kufika Tabora kumzika wataweza kufuatilia mazishi yake bila wasiwasi. Hongera Voice of Tabora 89.0 fm
 Fundi mitambo Dj Faster akiandaa urushaji Live shuhuli ya maziko ya Nyawana

Gari la matangazo live la Vot fm 89.0

Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu wakimsikiliza ustaadh nyumbani kwa Baba mkubwa wa marehemu Nyawana Gongoni, Tabora.


SAFARI YA MWILI WA MAMAA NYAWANA FUNDIKIRA TOKA DAR KUELEKEA TABORA


Msanii wa kundi la taarabu la mashauzi classic Thabit Abdul akiwa amebeba jeneza la mwili wa marehemu msanii Nyawana Fundikila pamoja na wausika wengine kwa ajili ya kupereka kwenye gari iliyomsafirisha kwenda tabora kwa ajili ya maziko

Kisomo cha Marehemu Nyawana Leo Tabora!

Ndugu, Jamaa na Marafiki Wakiwa Katika Kisomo cha Marehemu Nyawana Leo Tabora
Shekhe Katika Kisomo cha Marehemu Nyawana Leo Tabora!
DJ Fimbo (aliyevaa prova ya njano)Mmoja wa wafanyakazi wa kituo cha redio VoT FM ambacho marehemu alishawahi fanyia kazi
Ndugu, jamaa na marafiki katika wakati mgumu wa maombolezo
majonzi mazito

Nyawana kuzikwa kesho Tabora!

NYAWANA |Mama wa matashititi enzi za uhai wake
MULARD | MUME WA ZAMANI WA NYAWANA [CHANZO CHA PICHA]

Mwanamuziki maarufu wa Taarabu marehemu Nyawana Fundikira anatarajiwa kuzikwa kesho mchana au jioni kutegemeana na uwasili wa mwili wa marehemu mkoani Tabora. Ambapo baada ya kufanyiwa yale yote muhimu mkoani Dar mwili wake utasafirishwa kwa njia ya gari mpaka mjini Tabora kwa mazishi.



Mazishi yake yatafanyika kijijini kwao Itetemya yalipo makaburi na Ikulu ya familia ya kichifu ya Fundikira na Mtemi Isike Mwana Kiyungi. Nyawana Fundikira ambaye ameacha watoto wawili Said Murad (22) na Queen Murad (15) ambao alijaliwa kuwapata katika ndoa yake yake ya kwanza na Bw. Omar Khamis Murad (pichani). Murad mwanamichezo maarufu sana mjini Tabora ni meneja wa uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.

Breaking news! Mwanamuziki wa Taarabu Nyawana Fundikira afariki dunia mchana huu!

Mama Nyawana enzi za uhai wake
Mwanamuziki wa muziki wa taarab Nyawana Isale au Maarufu Nyawana Fundikira aka Mamaa Matashtiti amefariki leo hii mchana jijini Dar es Salaam alipokuwa akikimbizwa hospitalini baada kuzidiwa Inafahamika kuwa ameugua Malaria kwa siku kadhaa, kwa habari zaidi kuhusu kifo chake na mazishi tutaendela kujuzana humu na kwingineko. RIP mwanawane Nyawana!

Picha kwa hisani ya taarabuzetublog!

Duniani kuna mambo!

Hawa nao wakatoa yao kali chini ya bahari.

Baadhi ya watu wamekuwa wakipenda siku yao muhimu katika maisha yao iwe ya kukumbukwa daima. Kwa mfano wengi wamefunga ndoa zao katika mazingira ya ajabu na wengine wamekwenda mbali zaidi na kuamua kufunga pingu za maisha wakiwa uchi wa mnyama. Bi harusi Shelley Davie na Bwana harusi Josh Hughes wa Melbourne, Australia wao walitoa kali zaidi pale walipooana wakiwa uchi kabisa.

Josh Hughes na Shelley Davie wakifunga pingu za maisha uchi.

Galaxy Ace/Galaxy s4 and JVC Camcorder for sale!

Samsung Galaxy S4

Samsung Galaxy Ace i9500
Jvc Camcoder GR-D329E Mini Dv tape
For details please call Mpemba on 0712 831052